GE2025 Wananchi wa Buchosa washuhudia Makala ya miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa na Mbunge wao Eric Shigongo

GE2025 Wananchi wa Buchosa washuhudia Makala ya miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa na Mbunge wao Eric Shigongo

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mamia ya wananchi wa Kata za Nyakaliro na Irenza walijitokeza kwa wingiJulai 3, 2025, kushuhudia makala za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Jimbo la Buchosa, chini ya uongozi wa Mbunge wao Eric Shigongo

Zoezi hilo limeendelea kufanyika katika kata hizo ambapo wananchi waliwasilishiwa kazi mbalimbali zilizotekelezwa kupitia video halisi, ikiwemo ujenzi wa shule, barabara, zahanati, huduma za maji safi, chuo cha ufundi, pamoja na mipango ya uwezeshaji kwa vijana na wanawake.

Miradi hiyo imetekelezwa kwa ushirikiano kati ya Mbunge huyo na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuunga mkono juhudi za kuleta maendeleo katika maeneo ya pembezoni kama Buchosa

Lengo la zoezi hilo ni kufikisha taarifa za maendeleo kwa uwazi, kwa kuwaonesha wananchi hatua zilizofikiwa kwa njia ya video kutoka maeneo husika, hivyo kuimarisha uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi.

Zoezi hilo linaendelea kufanyika katika kata mbalimbali za jimbo hilo, likiwa ni sehemu ya kuhakikisha kila mwananchi anashiriki kikamilifu katika safari ya maendeleo ya Buchosa

Soma pia:
Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

20250705_101446.jpg
 
Ila wanasiasa nyie sijui mnawaonaje wale mnaosema waliwachagua,yaani ni kama vijikatuni mnavyowachukulia kwa sababu kama kweli hayo mnayoyaonyesha yamefanyika si wanayaona na wanayatumia tayari?au yamefanyika kwenye michoro kwenye makaratasi tu bado hayajwa vitu?

Picha na video za kazi gani?ikiwa ni lazima waone picha ni kwamba hayo hamjayafanya na hizo picha zitathibitishwaje kama hazikupigwa sehemu nyengine na siyo hapo Buchosa?
 
Mamia ya wananchi wa Kata za Nyakaliro na Irenza walijitokeza kwa wingiJulai 3, 2025, kushuhudia makala za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Jimbo la Buchosa, chini ya uongozi wa Mbunge wao Eric Shigongo

Zoezi hilo limeendelea kufanyika katika kata hizo ambapo wananchi waliwasilishiwa kazi mbalimbali zilizotekelezwa kupitia video halisi, ikiwemo ujenzi wa shule, barabara, zahanati, huduma za maji safi, chuo cha ufundi, pamoja na mipango ya uwezeshaji kwa vijana na wanawake.

Miradi hiyo imetekelezwa kwa ushirikiano kati ya Mbunge huyo na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuunga mkono juhudi za kuleta maendeleo katika maeneo ya pembezoni kama Buchosa

Lengo la zoezi hilo ni kufikisha taarifa za maendeleo kwa uwazi, kwa kuwaonesha wananchi hatua zilizofikiwa kwa njia ya video kutoka maeneo husika, hivyo kuimarisha uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi.

Zoezi hilo linaendelea kufanyika katika kata mbalimbali za jimbo hilo, likiwa ni sehemu ya kuhakikisha kila mwananchi anashiriki kikamilifu katika safari ya maendeleo ya Buchosa

View attachment 3394663
Kuna mtu mmoja aliwahi kuniambia kuwa nchi hii kuna mambo ya ajabu kabisa.
Kiongozi anakuja kuwataarifu wenyeji juu ya mradi ambao wananchi wamejengewa.Ina maana wananchi hawauoni?
Ni sawa tu na enzi za wapelelezi kabla ya ukoloni walipokuja na kudai wamegundua mlima Kilimanjaro au ziwa Victoria.
 
Alafu huyu babu Shigo sijui kawaje hapa kuna mawili pengine hatukumjua vizuri au kabadilikia ukubwani sasa ndio nini alafu kwani muda wa kampeni tayari?
 
Huyo lazima apite anawadai CCM hela nyingi sana baada ya kudai sana wakamtuliza na ubunge.
 
Back
Top Bottom