Wananchi wilayani Same mkoani Kilimanjaro wameonesha imani yao kwa mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi( CCM) Dk Samia Suluhu Hassan wakieleza kuwa watampatia ushindi wa kishindo. - Wakizungumza leo Septemba 30 kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea huyo wilayani Same Wananchi hao wamesema ,Dk Samia ametimiza mengi aliyoahidi hivyo haowaoni sababu ya kumnyima kura kwenye uchaguzi mkuu ujao.