Wananchi Nyasa wamshukuru Rais Magufuli

Wananchi Nyasa wamshukuru Rais Magufuli

elivina shambuni

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2018
Posts
461
Reaction score
295
1576690802838.png


Wananchi wa Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma wamemshukuru sana Rais John Pombe Magufuli kwa kuwaajengea hospitali ya Kisasa baada ya kutaabika kwa miaka yote wakiwa katika mazingira magumu sana kwa kufuata huduma ya Afya katika hospitali ya Wilaya ya Mbinga.

Shukran hiyo imepokelewa na Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo alipokuwa katika ziara ya Kikazi wilayani humo kukagua miradi ya maendeleo inayo simamiwa na Ofisi yake.

Katika ziara hiyo Waziri huyo wa TAMISEMI amewapongeza viongozi na wananchi wa Wilaya hiyo kwa kuhakikisha hospitali hiyo inakamilika vyema.

Aidha, Jafo amewataka wananchi hao watambue kwamba ujenzi wa hospitali hiyo pamoja na vituo vingine virat vya Afya, ujenzi wa miundombinu ya shule, na ujenzi wa barabara ya Lami kutoka Mbinga hadi Bambabay ni upendo wa moyoni wa Dkt. John Pombe Magufuli kwani ameamua kuwatoa katika kisa cha matatizo walichokuwa nacho kwa miaka yote.

Jafo amewaagiza viongozi kusimamia miradi yote iliyoletwa wilayani humo ili miradi hiyo ikamilike kwa lengo la kuwaletea wananchi unafuu wa kupata huduma mbalimbali za kijamii.

1576690817344.png
 
View attachment 1296540

Wananchi wa Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma wamemshukuru sana Rais John Pombe Magufuli kwa kuwaajengea hospitali ya Kisasa baada ya kutaabika kwa miaka yote wakiwa katika mazingira magumu sana kwa kufuata huduma ya Afya katika hospitali ya Wilaya ya Mbinga.

Shukran hiyo imepokelewa na Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo alipokuwa katika ziara ya Kikazi wilayani humo kukagua miradi ya maendeleo inayo simamiwa na Ofisi yake.

Katika ziara hiyo Waziri huyo wa TAMISEMI amewapongeza viongozi na wananchi wa Wilaya hiyo kwa kuhakikisha hospitali hiyo inakamilika vyema.

Aidha, Jafo amewataka wananchi hao watambue kwamba ujenzi wa hospitali hiyo pamoja na vituo vingine virat vya Afya, ujenzi wa miundombinu ya shule, na ujenzi wa barabara ya Lami kutoka Mbinga hadi Bambabay ni upendo wa moyoni wa Dkt. John Pombe Magufuli kwani ameamua kuwatoa katika kisa cha matatizo walichokuwa nacho kwa miaka yote.

Jafo amewaagiza viongozi kusimamia miradi yote iliyoletwa wilayani humo ili miradi hiyo ikamilike kwa lengo la kuwaletea wananchi unafuu wa kupata huduma mbalimbali za kijamii.

View attachment 1296541
Kwani kujenga hiyo miundombinu ni upendo toka moyoni mwa raisi au ni wajibu wa serikali?
 
Back
Top Bottom