Echisute
JF-Expert Member
- Oct 16, 2018
- 635
- 633
Leo tar. 09.07.2026 majira ya saa 3 asubuhi, kata ya Ilolangulu wilaya ya Uyui mkoa wa Tabora kuna tangazo limetangazwa likawataka wakazi wote pamoja na vitongoji vyake kesho asubuhi majira ya saa 4 waache shughuli zao zote waende kumlaki Ridhiwan Kikwete eti kwa sababu atakuwa anazindua shule mpya ya secondary hapo katani.
Tangazo limeenda mbali na kusisitiza marufuku ya mtu yeyote kuonekana akirandaranda bila kuwa eneo la tukio au kufunguliwa kwa aina yoyote ya biashara kabla ya huo ugeni kuondoka hapo katani! Onyo limetolewa kwa mfanyabiashara yeyote atakayekiuka masharti ya hilo tangazo kutozwa faini ya Tsh. 50,000/=
My take: Naomba chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) mtoe elimu kwa wananchi wote nchi nzima mkilaani na kukemea matamshi ya vitisho kama haya na kuwajengea wananchi uelewa wa kutambua haki zao za kufanya shughuli zao za kiuchumi bila kuathiriwa na matamshi ya kisiasa kama haya.
Tangazo limeenda mbali na kusisitiza marufuku ya mtu yeyote kuonekana akirandaranda bila kuwa eneo la tukio au kufunguliwa kwa aina yoyote ya biashara kabla ya huo ugeni kuondoka hapo katani! Onyo limetolewa kwa mfanyabiashara yeyote atakayekiuka masharti ya hilo tangazo kutozwa faini ya Tsh. 50,000/=
My take: Naomba chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) mtoe elimu kwa wananchi wote nchi nzima mkilaani na kukemea matamshi ya vitisho kama haya na kuwajengea wananchi uelewa wa kutambua haki zao za kufanya shughuli zao za kiuchumi bila kuathiriwa na matamshi ya kisiasa kama haya.