Wanajeshi watanda wilaya ya Tandahimba Mtwara

Wanajeshi watanda wilaya ya Tandahimba Mtwara

yaser

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
1,361
Reaction score
299
Yakiwa yamebaki masaa tu kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini mwetu, wananchi wa wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara wameanza kuingiwa hofu na wengine wakiamua kuyakimbia makazi yao na kuhamia nchi ya jirani ya Msumbiji baada ya wanajeshi na magari yao ya kijeshi kutanda katika wilaya hiyo.

Hili suala limeibua maswali na woga mwingi sana miongoni mwa wananchi wa wilaya hiyo wengine wakihoji mbona chaguzi kadhaa zimepita haijawahi kutokea hali hiyo? Alipoulizwa mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendegu amesema wapo pale kuimarisha amani.

Kwa upande mwingne mbunge anayegombea jimbo hilo amesema amepewa rushwa ya shiling milion 160 ila amekataa na sasa anapata vitisho kila muda.

Chanzo: Azam Two (Habari).
 
Alilopanga MUNGU mwanadamu katu hawezi kupangua, wanatandahimba kapigeni kura msubiri matokeo (Follow the rules and wait to win) hamna sababu ya kuutamani Ukimbizi kirahisi ivyo. God be with U.
 
CCM ni janga ila Mungu yupo pamoja nanyi wanatandahimba,msiwe na hofu
 
Yakiwa yamebaki masaa tu kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchin mwetu, wananchi wa wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara wameanza kuingiwa hofu na wengine wakiamua kuyakimbia makazu yao na kuhamia nchi ya jiran ya msumbiji baada ya wanajeshi na magari yao ya kijeshi kutanda katika wilaya hiyo. Hili suala limeibua maswai na woga mwing sana miongon mwa wananchi wa wilaya hiyo wengine wakihoji mbona chaguzi kadhaa zimepita haijawahi kutokea hali hioy?? Alipoulizwa mkuu wa mkoa wa mtwara Halima Dendegu amesema wapo pale kuimarisha amani.
Kwa upande mwingne mbunge anayegombea jimbo hilo amesema amepewa rushwa ya shiling milion 160 ila amekataa na sasa anapata vitisho kila muda.
Source: Azam two habar.

Haitawasaidia kitu ndio kwanza wanaongeza petrol kwenyecmoto unao waka jangwani na kipigo cha ccm kipo pale pale....ukawa hoyeeeeeeeeeeeee
 
Ccm wameanza mchezo mchafu wa kuanza kuvunja amani ya nchi, hivi mgombea akihöngwa kiasi hicho cha pesa ndio wapeleke hiyo mizinga na vifaru km c uhuni?
 
Hawajaelewa hawa ccm.... Wanapoteza kura zao wazeee na akina mama... Vijana kazini kama kawa...kura tunalindaa kwa staili mpya...
 
Jana kuna Polisi aliuawawa huko Shirati Rorya wakati wa kufunga kampani ya CHADEMA kwa uonevu wa kipuuzi,Polisi leteni tu fujo ila mjue tunakaa wote mtaani.
 
Police naombeni pigeni wale wote watakaojifanya wanaleta uvunjifu wa amani wa kwanza ni huyo Ruhi
 
Mbona sehemu nyingi kuna upinzani mkubwa kana mbeya na moshi lakini hatuoni wanajeshi wala polisi wakifanya vurugu?
Tatizo ni huyo Mbwiga aliyehamishiwa huko
 
Sitegemei safari hii Khatan atadhurumiwa haki yake ya ubunge kirahisi kama awamu zilizopita.
 
Mnaoiamini C.C.M Mpaka Dakika Hii Kwamba C.C.M Italeta Maendeleo Nawashauri MKAJISALIMISHE HOSPITAL YA MILEMBE KABLA TATIZO LAKO HALIJAKUWA KUBWA.Ukianza Tiba Mapema Nasikia Ugonjwa Wa Kichaa Huweza Kutibika.
 
Mnaoiamini C.C.M Mpaka Dakika Hii Kwamba C.C.M Italeta Maendeleo Nawashauri MKAJISALIMISHE HOSPITAL YA MILEMBE KABLA TATIZO LAKO HALIJAKUWA KUBWA.Ukianza Tiba Mapema Nasikia Ugonjwa Wa Kichaa Huweza Kutibika.

Kamuuloze Msigwa CCM na Lowassa bora kuamini nn? Yeye atakupa jibu
 
Jamani watanzania wenzangu vifaru vya nini Mtwara? Hali ni mbaya kiasi hicho, katika hali ya kushtua wana Mtwara tumeona jeshi la wananchi kupita mitaani na vifaa vya kivita, sasa najiuliza tunaenda vitani? Au tunaenda kupiga kura ?
Watu wameshakuwa na hofu ya amani, huku mna tuhubiria amani..
 
Kama siyo muhalifu au mfanya vurugu hofu ya nini? Jeshi lipo katika shughuli zake za kulinda amani na wewe endelea na shughuli zako bila kusababisha uvunjifu wa amani.
 
.....tunaona jinsi jw inavyotumika.....ktk issues ya kijeshi mfano kuzindua uwanja wa denge wa kijeshi inakuwaje mtu anaongelea masuala ya kura?.tena kwa kuwapiga vijembe wapinzani wake wa kisiasa........heri wale vijana waliojaribu kumpindua nyerere.....walikuwa na akili sana.
 
Imasemekana watanzania wa huko wanaanza kuwa wakimbizi msumbiji
 
JWTZ Hawa hawana shida ila hawa polisi ndiyo wako na shida mingi
 
Back
Top Bottom