Katika kile ambacho kinaelezwa ni kubanwa kwa CCM, chama hicho kikongwe sasa kimekuwa kikijaribu kila mbinu kujinasua katika kibano cha UKAWA.Kuna taarifa kwamba CCM inawanunua baadhi ya viongozi wa UKAWA kwa kuwarubuni na kuwapa propaganda za uongo kuhusu UKAWA. Huku kikiwa kinayatumia mapungufu yalipo ndani ya UKAWA.
Moja ya propaganda ni kuhusu taarifa za kwamba Edward Lowassa amewanunua viongozi wa UKAWA kwa maslahi binafsi.Taarifa hizi zinaeleza kwamba kuna viongozi watajitoa kutoka miongoni mwa UKAWA na kudai kwamba viongozi wa juu hawawatendei haki. Tayari hilo limefanyika NCCR Mageuzi ingawa linaonekana halina nguvu.Mtoa taarifa kutoka ndani ya CCM katika timu ya kampeni anayemuunga mkono Lowassa anasema,''huu mkakati ni kama utashindikana kwa sababu ukiangalia wananchi tayari wameshaamua''.
Mtoa taarifa wa habari hizi ni kiongozi mwandamizi wa CCM ambaye huzunguka na mgombea urais wa CCM, Dkt John Pombe Magufuli na hakutaka kutajwa jina lake kuhofia usalama wake.Tayari baadhi ya viongozi wa NCCR Mageuzi wamejiondoa kutoka miongoni mwa UKAWA, kwa madai kwamba, mwenyekiti wa chama hicho hawasikilizi. Mtoa taarifa kutoka ndani ya CCM anasema, ''suala la NCCR Mageuzi linahitaji busara sana, tayari walishakaa na wakaamua kuhusu majimbo leo wanajitokeza walikuwa wapi?'' akongeza, ''Hii ni kuwaumiza wananchi ambao wapo tayari kwa ajili ya mabadiliko''. Huku akiongea kwa kujiamini anaongeza, ''mimi niko huku(yaani CCM) kwa sababu nahofia usalama wangu ila namuunga mkono Lowassa na wananchi walio wengi''.Akaongeza kwamba mbinu za Lowassa zinabadilika sana na hatabiriki ndiyo maana CCM wanashindwa na kila wanapojaribu inajulikana.
Huku akisisitiza kwa njia ya simu, alisema, hakuna sababu ya wananchi na wapenda mabadiliko kukata tamaa', unapoona haya na kusikia haya ujue mwisho wa adui unakaribia''. Akaongeza kwamba ni muhimu sana kwa wakati kama huu kuwa wamoja.Chama cha NCCR Mageuzi kimetoa tamko kutotambua waliojiengua kwa kusema kwamba hawakufuata taraibu ndani ya chama na kwamba wanatumika, na kimewataka wananchi kujitokeza kumpigia kura Edward Lowassa.
Aidha kutakuwa na umoja utakao undwa kutokana na wanaojiengua na umoja huo utakaoitwa UKAWA utakuwa na baadhi ya wanaUKAWA waliojiengua kutoka UKAWA na utahamasisha ili kuungwa mkono na wananchi huku ukiratibiwa kwa karibu na vituo vya habari vya STARTV na TBC. Miongoni mwa watu watakao unga mkono umoja huo ni Dr Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CHADEMA. Maneno ya kimkakati ni Mbeya, Dar Es Salaam na mengine watakayoona yanafaa.Anaongeza, ''tafadhi nyinyi waandishi waambieni wananchi na wapenda mabadiliko wasitetereke kabisa, haya yote yatapita na ndiyo misuko suko ya mabadiliko''. ''Sasa hivi wamemwachia January Makamba, ndiyo kila kitu sasa unaona tunavyoyumba''(wao CCM), alisema.
Iwapo hilo litashindikana wataunda umoja wa vyama vingine vya upinzani vikihusisha ACT Wazalendo, UDP na vyama vingine ikiwa ni mkakati wa kuiokoa CCM, kwa kugawa kura na kuwachanganya wananchi ili wakate tamaa ya kupiga kura.Mlinzi mmoja wa timu ya Magufuli aliyejulikana kwa jina moja la Juma amemwambia mwandishi wa habari hizi kwamba hali ya chama hicho kikongwe ni mbaya na hasa katika masuala ya kifedha na kusababisha kuomba msaada kwa marafiki zake wa nje(hakutaja ni nchi gani).''Nakuambia hivi hatushindi waandishi pengine mmeshajua hili kwamba hatushindi, tunalazimisha tu''. Alisema kwamba wingi wa watu katika mikutano ya CCM ni kwakuwa wanasomba watu na Malori na kuwapa hongo(baadhi) kuanzia shilingi 5,000-10,000.
Moja ya propaganda ni kuhusu taarifa za kwamba Edward Lowassa amewanunua viongozi wa UKAWA kwa maslahi binafsi.Taarifa hizi zinaeleza kwamba kuna viongozi watajitoa kutoka miongoni mwa UKAWA na kudai kwamba viongozi wa juu hawawatendei haki. Tayari hilo limefanyika NCCR Mageuzi ingawa linaonekana halina nguvu.Mtoa taarifa kutoka ndani ya CCM katika timu ya kampeni anayemuunga mkono Lowassa anasema,''huu mkakati ni kama utashindikana kwa sababu ukiangalia wananchi tayari wameshaamua''.
Mtoa taarifa wa habari hizi ni kiongozi mwandamizi wa CCM ambaye huzunguka na mgombea urais wa CCM, Dkt John Pombe Magufuli na hakutaka kutajwa jina lake kuhofia usalama wake.Tayari baadhi ya viongozi wa NCCR Mageuzi wamejiondoa kutoka miongoni mwa UKAWA, kwa madai kwamba, mwenyekiti wa chama hicho hawasikilizi. Mtoa taarifa kutoka ndani ya CCM anasema, ''suala la NCCR Mageuzi linahitaji busara sana, tayari walishakaa na wakaamua kuhusu majimbo leo wanajitokeza walikuwa wapi?'' akongeza, ''Hii ni kuwaumiza wananchi ambao wapo tayari kwa ajili ya mabadiliko''. Huku akiongea kwa kujiamini anaongeza, ''mimi niko huku(yaani CCM) kwa sababu nahofia usalama wangu ila namuunga mkono Lowassa na wananchi walio wengi''.Akaongeza kwamba mbinu za Lowassa zinabadilika sana na hatabiriki ndiyo maana CCM wanashindwa na kila wanapojaribu inajulikana.
Huku akisisitiza kwa njia ya simu, alisema, hakuna sababu ya wananchi na wapenda mabadiliko kukata tamaa', unapoona haya na kusikia haya ujue mwisho wa adui unakaribia''. Akaongeza kwamba ni muhimu sana kwa wakati kama huu kuwa wamoja.Chama cha NCCR Mageuzi kimetoa tamko kutotambua waliojiengua kwa kusema kwamba hawakufuata taraibu ndani ya chama na kwamba wanatumika, na kimewataka wananchi kujitokeza kumpigia kura Edward Lowassa.
Aidha kutakuwa na umoja utakao undwa kutokana na wanaojiengua na umoja huo utakaoitwa UKAWA utakuwa na baadhi ya wanaUKAWA waliojiengua kutoka UKAWA na utahamasisha ili kuungwa mkono na wananchi huku ukiratibiwa kwa karibu na vituo vya habari vya STARTV na TBC. Miongoni mwa watu watakao unga mkono umoja huo ni Dr Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CHADEMA. Maneno ya kimkakati ni Mbeya, Dar Es Salaam na mengine watakayoona yanafaa.Anaongeza, ''tafadhi nyinyi waandishi waambieni wananchi na wapenda mabadiliko wasitetereke kabisa, haya yote yatapita na ndiyo misuko suko ya mabadiliko''. ''Sasa hivi wamemwachia January Makamba, ndiyo kila kitu sasa unaona tunavyoyumba''(wao CCM), alisema.
Iwapo hilo litashindikana wataunda umoja wa vyama vingine vya upinzani vikihusisha ACT Wazalendo, UDP na vyama vingine ikiwa ni mkakati wa kuiokoa CCM, kwa kugawa kura na kuwachanganya wananchi ili wakate tamaa ya kupiga kura.Mlinzi mmoja wa timu ya Magufuli aliyejulikana kwa jina moja la Juma amemwambia mwandishi wa habari hizi kwamba hali ya chama hicho kikongwe ni mbaya na hasa katika masuala ya kifedha na kusababisha kuomba msaada kwa marafiki zake wa nje(hakutaja ni nchi gani).''Nakuambia hivi hatushindi waandishi pengine mmeshajua hili kwamba hatushindi, tunalazimisha tu''. Alisema kwamba wingi wa watu katika mikutano ya CCM ni kwakuwa wanasomba watu na Malori na kuwapa hongo(baadhi) kuanzia shilingi 5,000-10,000.