Mendelian Inheritanc
Member
- Dec 25, 2011
- 86
- 11
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CDM Kata ya Segerea Jeff Moshi amewataka wale wote wanaopigania haki katika nchi hii, wanafunzi vyuo vikuu,walimu na wafanyakazi sehemu mbalimbali, madaktari pamoja na wanaharakati wanaopinga ufisadi,anawatia moyo kwa kuwakumbusha kile alichowahi kukisema Mandela Popote pale hakuna njia rahisi ya ukombozi, na wengi wetu itabidi tupitie tena na tena kwenye bonde la uvuli wa mauti kabla ya kufikia kilele cha mafanikio Aidha mwanafalsafa wa Morocco, aliyefia Zanzibar mwaka 1313 alisema Tutakapokufa msitutafute kwenye makaburi yaliyopambwa kwa kupakwa chokaa, bali tutafuteni kwenye mioyo ya watu tuliowatumikia
Aidha, wapo watanzania wanaokemea maovu, lakini wanakumbana na vitisho.Wanaharakati hawa pia wasikate tama, kwa kuwa kama alivyosema mwanafalsafa wa ujerumani, Arthur Schopenhauner (1788-1860), Ukweli wowote hupitia ngazi tatu, kwanza, ngazi ya kukejeliwa, pili ngazi ya kupingwa na hata ikibidi kumwaga damu, na tatu, kukubalika kwa kuwa ukweli hujisimamia wenyewe
Vilevile, watanzania tubadilike tuondoe woga, Tunatakiwa tuwe na ujasiri.Mwanamama mpigania haki wa Burma Aung Suu Kyi alipotoka gerezani alipokuwa amefungwa kwa kupigania haki alisema gereza pekee na la ukweli na halisi ni woga, na uhuru pekee wa ukweli na halisi ni uhuru dhidi ya woga. Mwenyekiti huyo wa BAVICHA Segerea aliyazungumza hayo jana. Nawasilisha!!!!!!
Aidha, wapo watanzania wanaokemea maovu, lakini wanakumbana na vitisho.Wanaharakati hawa pia wasikate tama, kwa kuwa kama alivyosema mwanafalsafa wa ujerumani, Arthur Schopenhauner (1788-1860), Ukweli wowote hupitia ngazi tatu, kwanza, ngazi ya kukejeliwa, pili ngazi ya kupingwa na hata ikibidi kumwaga damu, na tatu, kukubalika kwa kuwa ukweli hujisimamia wenyewe
Vilevile, watanzania tubadilike tuondoe woga, Tunatakiwa tuwe na ujasiri.Mwanamama mpigania haki wa Burma Aung Suu Kyi alipotoka gerezani alipokuwa amefungwa kwa kupigania haki alisema gereza pekee na la ukweli na halisi ni woga, na uhuru pekee wa ukweli na halisi ni uhuru dhidi ya woga. Mwenyekiti huyo wa BAVICHA Segerea aliyazungumza hayo jana. Nawasilisha!!!!!!