Sisi wengine tukifa itakuwa vigumu sana kwa watu kujua humu.
Tunamwombea apumzike kwa amani..Nilimjua kuwa Marehemu ni member wa JF alikuwa analalamika kuwa amepigwa BAN na nilipomuuliza kuwa anatumia ID gani akaniambia hawezi kuniambia, ingawa nilitamani kuijua ID yake kwani nilimwambia ID yangu ya hapa JF lakini akakataa kuniambia ID yake. Kwa hiyo sikuweza kumlazimisha, nilijaribu kutaka kuijua lakini sikuweza kufanikiwa mda mwingi alikuwa ana browse kwenye simu yake. Kwa hiyo nilishindwa kuijua.
Mi nikikaribia kuondoka ntawajulisha.
RIP kwa waliotangulia.
Namkumbuka Kandambilimbili(RIP)!
Huenda siku moja atarudi atujulishe kama huko alipo kuna JF au kitu kinachofanana nayo!
Mi nikikaribia kuondoka ntawajulisha.
RIP kwa waliotangulia.
Well said bak... It's like he left with all the wisdom in that forumMimi huwa namkumbuka sana yule mwenzetu aliyejiita Mpenzi wa Islam. Huyu alinigusa sana kwa jinsi alivyokuwa mpole na kutumia lugha ya kistaarabu katika majadiliano katika jukwaa la dini. Pamoja na baadhi ya wachangiaji walikuwa wakitumia matusi na kashfa nzito nzito dhidi ya dini ya Kiislam, Mpenzi wa Islam hata siku moja hakukashifu, kumtukana mtu/dini au kutumia lugha ambazo si za kistaarabu bali alijibu kwa kujaribu kuwaelewesha wachangiaji hao. Nilipenda sana kusoma michango yake na hadi nikamuomba urafiki hapa jamvini. Nilipenda sana kukutana naye na tayari nilishapanga kumtafuta pindi nafasi ingeruhusu lakini kabla ya kufanikiwa kufanya hivyo akafariki. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu na wengine wote waliowahi kuwa wanachama wa jamvi hili mahali pema peponi~AMEN.
...kifo ni fardhi, hakiepukiki!
Hata mimi nipo radhi id yangu kuwa revealed siku ya ahadi (roho ikiacha mwili.)
Kuna ninaofahamiana nao alhamdulillah, na kwa wale tusofahamiana inshaallah
panapo majaaliwa...
Niliumia sana siku ya msiba wa mwenzangu Felix Chambi aka Makene niliyepotezana nae miaka mingi kisha kuja kusoma; https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/9206-felix-makene-afariki-dunia.html na haswa kwakujua kumbe naye alikuwa member mwenzetu tukijibishana hoja & viroja humu.
Hivi kwanini tunaogopa kujuana?
kuna member nilikua nawapenda sana siku lkn siku hizi siwaoni,na walionesha sana kuipenda sana JF ndo nikapata mawazo kuwa huwenda wako kama mm na labda wamefariki hivyo hakuna wakutujulisha.Kwa kweli kuna member humu nawapenda sana kwa michao na picha niliyojijengea juu yao hivyo japo sijui hata wanafananaje nawezaa kulia nikisia wametutoka.So ni mawazo kama haya ndo yamekua chanzo cha hii thread..
Hapo blue amina.
Kila nafsi itaonja umauti, mwenyezi mungu awapumzishe kwaa amani wote waliotangulia mbele ya haki.
Kweli kunaumuhimu wa kufahamiana na baadhi ya member, ambaye yuko tayari itakuwa poa, nipo Mbeya.
Kweli aisee, hivi kuna Member wa JF huku KAZIMZUMBWI?
Kama yupo basi tukutane pale kwa Mzee Mambaligwa karibu na ule muembe uliokuwa ukitumika kwa shughuli za Mkole na Ngoweko.
Pale kuna kijiwe kizuri sana cha Kahawa. Nitakuwa nimevaa Kanzu ya nyeupe na Makubazi na Mawani yenye fremu za plastic.