Goliath mfalamagoha
JF-Expert Member
- Aug 3, 2012
- 602
- 2,505
BARUA YA WAZI KWA WANA WA UKONGA NA MONDULI
Na Kibona Dickson
(Mwanaharakati Huru)
Wana wa Ukonga na wana wa Monduli.
Mimi Mzalendo na Mtanzania mwenzenu.Ninawasalimu sana.
Ninawaandikia ninyi kwa sababu 2015 mlimshinda adui aliyeshindwa kutuletea maendelea kwa zaidi ya miaka 50 ya Uhuru.Adui huyu ni sisiem.Mwaka 1995,hayati MWALIMU Nyerere alimfananisha Kokoro linalovua kila kitu,hata vitu viovu.Taifa limejaa ukatili na uonevu mkubwa wa enzi za kikoloni kule Afrika ya kusini.
Hiyo ndiyo sisiem ambayo mliikataa 2015 kwa aibu katika Sanduku la kura,mkachagua chama mnachokipenda kwa kishindo.Chama chenye ghilba na ulaghai kilichojaa hadaa katika awamu ya tano kinajiita sisiem mpya.
Ni sisiem mpya yenye kutumia ulaghai,vitisho na mamilioni ya fedha kuhakikisha madiwani na wabunge wanajiuzulu kwa hoja ya kuunga mkono juhudi.Chama cha SISIEM kinataka kulazimishwa kupendwa kwa ghilba na vitisho.
Wana wa Ukonga na Monduli;Niliwahi andika leo nitanukuu tena "Huu ni wendawazimu wa kisiasa kuachia dhamana uliyokabidhiwa wananchi ili kuunga mkono mtu mwingine aliyekabidhiwa dhamana na wananchi kama wewe" mwisho wa kunukuu.
Wana wa Ukonga na Minduli;Wana ccm na wana chadema na vyama vingine uunganeni kukataa aina hizi za siasa zinazojengeka katika taifa letu;siasa chafu zinazoshadidiwa na nguvu ya pesa na vitisho chini ya chama kinachoitwa SISIEM mpya.
SISIEM mpya inayotumia mabavu na hoja ya nguvu ili ikue na kwa njia ya kukataa ushindani wa kisiasa.SISIEM impya inayozidi kubebwa na Polisi.SISIEM mpya inayotaka kuendekeza siasa za ukiritimba na kuhodhi madaraka kwa njia za ulaghai,vitisho na mabavu.SISIEM mpya inayotumia ukosefu wa ajira kuangamiza vyama vya siasa.
Wana Ukonga na wana Monduli,uamuzi wenu usiojali itikadi za vyama uwe ni kukataa aina ya siasa ambazo chama kinaitwa SISIEM mpya kinajaribu kuzileta katika taifa letu.
Mtu aliyepewa dhamana kisha akajiuzulu mwenye,Msimpe tena ridhaa aliyoikataa kwa kujiuzulu.
Ninamaanisha,Julius Kalanga na Mwita waitara waaibishwe na SISIEM.Ninyi wana Ukonga na Monduli,mna uwezo wa kufanya hayo mkipiga kura na kuzilinda.
Hakuna CCM mpya.Ukweli CCM ni ileile ambayo hayati Nyerere alisema "ni kokoro"
DICKSON KIBONA.
Mwanaharakati Huru.
Kibonadickson@gmail.com
Sent using Jamii Forums mobile app
Na Kibona Dickson
(Mwanaharakati Huru)
Wana wa Ukonga na wana wa Monduli.
Mimi Mzalendo na Mtanzania mwenzenu.Ninawasalimu sana.
Ninawaandikia ninyi kwa sababu 2015 mlimshinda adui aliyeshindwa kutuletea maendelea kwa zaidi ya miaka 50 ya Uhuru.Adui huyu ni sisiem.Mwaka 1995,hayati MWALIMU Nyerere alimfananisha Kokoro linalovua kila kitu,hata vitu viovu.Taifa limejaa ukatili na uonevu mkubwa wa enzi za kikoloni kule Afrika ya kusini.
Hiyo ndiyo sisiem ambayo mliikataa 2015 kwa aibu katika Sanduku la kura,mkachagua chama mnachokipenda kwa kishindo.Chama chenye ghilba na ulaghai kilichojaa hadaa katika awamu ya tano kinajiita sisiem mpya.
Ni sisiem mpya yenye kutumia ulaghai,vitisho na mamilioni ya fedha kuhakikisha madiwani na wabunge wanajiuzulu kwa hoja ya kuunga mkono juhudi.Chama cha SISIEM kinataka kulazimishwa kupendwa kwa ghilba na vitisho.
Wana wa Ukonga na Monduli;Niliwahi andika leo nitanukuu tena "Huu ni wendawazimu wa kisiasa kuachia dhamana uliyokabidhiwa wananchi ili kuunga mkono mtu mwingine aliyekabidhiwa dhamana na wananchi kama wewe" mwisho wa kunukuu.
Wana wa Ukonga na Minduli;Wana ccm na wana chadema na vyama vingine uunganeni kukataa aina hizi za siasa zinazojengeka katika taifa letu;siasa chafu zinazoshadidiwa na nguvu ya pesa na vitisho chini ya chama kinachoitwa SISIEM mpya.
SISIEM mpya inayotumia mabavu na hoja ya nguvu ili ikue na kwa njia ya kukataa ushindani wa kisiasa.SISIEM impya inayozidi kubebwa na Polisi.SISIEM mpya inayotaka kuendekeza siasa za ukiritimba na kuhodhi madaraka kwa njia za ulaghai,vitisho na mabavu.SISIEM mpya inayotumia ukosefu wa ajira kuangamiza vyama vya siasa.
Wana Ukonga na wana Monduli,uamuzi wenu usiojali itikadi za vyama uwe ni kukataa aina ya siasa ambazo chama kinaitwa SISIEM mpya kinajaribu kuzileta katika taifa letu.
Mtu aliyepewa dhamana kisha akajiuzulu mwenye,Msimpe tena ridhaa aliyoikataa kwa kujiuzulu.
Ninamaanisha,Julius Kalanga na Mwita waitara waaibishwe na SISIEM.Ninyi wana Ukonga na Monduli,mna uwezo wa kufanya hayo mkipiga kura na kuzilinda.
Hakuna CCM mpya.Ukweli CCM ni ileile ambayo hayati Nyerere alisema "ni kokoro"
DICKSON KIBONA.
Mwanaharakati Huru.
Kibonadickson@gmail.com
Sent using Jamii Forums mobile app