Usijilaumu sana, zama zinabadilika haraka sana zama za kina Ole Konchellah, Ole Saibul,Lepillal Ole Molloimet, Benedict Lesuritia, Edward Mbarnot,Edward Lowassa na mpendwa wetu Edward Sokoine na wengine wa rika hizo waliingia siasa kabla haijawa biashara.Sasa hivi kuingia siasa bila kubebwa na MTU mwenye musuli sio rahisi, sio suala LA kabila wala Tanzania.Hivi umewahi kujiuliza kama Marekani wanalalamika chaguzi zao kuingiliwa kwetu ikoje, ni kura zetu kweli zinazisimika viongozi na kama huna kitu na huna MTU wa kukubeba waweza shinda uchaguzi? Kina Nyerere, Lumumba, Nkuruma, Nasser bado wapo Afrika? Bora huyu wakwetu ingalau ana ujasiri hata wa kusema ukweli. Usikate tamaa historia huwa inajirudia ,kwani hata kina Nyerere, Mandela nk sio mashujaa wa kwanza Afrika, Mungu, wakati , uhitaji utawanyanyua wengine yaweza kuwa akina Julius Malema Afrika kusini, Ole Sendeka au wewe kwa Wamasai .Usikate tamaa wala usihofu, wala kwa sasa ambapo watu karibia wrote mpaka maprofesa wanafikiria kwa kutumia matumbo yao na sio vichwa vyao usitegemee Masai awe tofauti sana.Sasa Masai anahitaji bodaboda ya kuzunguka mbugani, anahitaji gari,nyumba ya kisasa,wapo wanaovaa chain za dhahabu ,wanahitaji miziki, wanakula kuku, mayai na samaki nk kifupi wanahitaji mapesa mengi ikiwa inachangiwa na shule za kisasa au kizungu wanazosoma. Life style