Wamama acheni tabia ya kuwatukana watoto wenu matusi ya nguoni

Dam55

JF-Expert Member
Oct 8, 2015
5,592
11,831
Habari wapendwa,

Kwa dhati ya Moyo wangu nawatakia pasaka njema yenye furaha na amani.

Kuna hii tabia ya wanawake hasa wamama, kwa kweli nisingependa siku hii ya pasaka ikapita huku nikiwa na duku duku rohoni. Wamama acheni tabia ya kuwatukana watoto wenu matusi ya nguoni. Hivi we mama ndio kusema kwamba una hasira sana ama ni vipi hadi unafikia hatua kumtukana mtoto wako uliye mzaa tena tusi linalokuhusu wewe mwenyewe. Huoni kama unamtolea razi mwanao.

Tabia hii imeshamiri sana kwa sasa halafu mnalalamika kuwa watoto hawana akili shuleni, wahuni, watukanaji, hawana nidhamu n.k wakati mmewalaani wenyewe.
Halafu unajidai na we ni mama kweli? Mama gani wewe usiye na haya hata kidogo mtoto wako wa kumzaa unathubutu kumtajia alipotokea? Umechanganyikiwa wewe.

Sijaoa na wala bado sijabahatika kupata mtoto ila nikija kuoa halafu siku nikamkuta anamtukana mtoto mitusi wallah ndoa inavunjika siku hiyo hiyo. Wanawake acheni huu ujinga, mbona wazazi wetu hawakuwahi kututukana namna hiyo hii tabia nyie mmepata wapi? Au ndo kweli nyie wanawake ni mashetani. Na kama ni hivyo basi ni wanawake wa kizazi hiki tu ndo mashetani mana mama zetu hawakuwa na tabia kama hizi. Au ndo mnatukana watu wazima kwa kisingizio cha watoto? Maana haiwezekani kabisa umtukane mwanao namna hiyo.

Samahani kwa niliowakwaza ila ujumbe wangu umefika.

Acheni kuwalaani watoto wenu kwa makusudi, mtoto anapokosea anaelekezwa na sio kutukanwa mitusi.

Ahsante.
 
Hebu punguza jazba wewe. Hiyo ni khulka ya mtu na sio wanawake wote.

Pia labda nikuulize hatua gani unazozichukua kukomesha hiyo tabia au kuja kupiga makelele huku ndio unaona umeshaikomesha.
 
mkuu samahani kidogo.. hv mwanzoni batani K ilikuwa haifanyi kazi mpaka uka'replace na l ... halaf haraka zako zimefanya ndoa umeiita ndio... ha!!! ha!!!! ha!!!! ha!!!!
back to the thread.. matusi hayo ni kutokana na watoto wenyewe.. mtoto haelewi mpaka unataman m'badilishane aone karaha unazopata!!!
 
Kumtukana mtt hakumfundishi tabia njema hata kama amefanya kosa gani ni bora umwadhibu tu
 
mkuu samahani kidogo.. hv mwanzoni batani K ilikuwa haifanyi kazi mpaka uka'replace na l ... halaf haraka zako zimefanya ndoa umeiita ndio... ha!!! ha!!!! ha!!!! ha!!!!
back to the thread.. matusi hayo ni kutokana na watoto wenyewe.. mtoto haelewi mpaka unataman m'badilishane aone karaha unazopata!!!
Ahsante kwa kusahihisha mkuu, wameniudhi sana watu wa namna hii.
 
Hao wengi ni wale wamama wa uswahilini,stress za maisha zinasababisha iwe single mother au wenye ndoa zao wakivurugwa huko hasira wanamalizia kwa watoto wao,unaweza kuta anatukana kwa style ya kuhadithia kilichomkuta mpaka huyo mtoto akapatikana.
 
Hebu punguza jazba wewe. Hiyo ni khulka ya mtu na sio wanawake wote.

Pia labda nikuulize hatua gani unazozichukua kukomesha hiyo tabia au kuja kupiga makelele huku ndio unaona umeshaikomesha.
Khulka au ujinga??? Inawezekanaje mtu kuwa na khulka ya matusi, kama sio upungufu wa akili kumbe nini.?
 
mkuu samahani kidogo.. hv mwanzoni batani K ilikuwa haifanyi kazi mpaka uka'replace na l ... halaf haraka zako zimefanya ndoa umeiita ndio... ha!!! ha!!!! ha!!!! ha!!!!
back to the thread.. matusi hayo ni kutokana na watoto wenyewe.. mtoto haelewi mpaka unataman m'badilishane aone karaha unazopata!!!
Sasa kama haelewi ndo atukanwe mitusi.
Sasa kama watu wazima tu na hawaelewi kama huyo hapo juu anataka nimpe mfano wa matusi, sasa mtoto je atakuwaje??
 
Kwanzaa unaanzaje kumtusi mtoto wako..
Hiyo ndo naisikia leo, ila kuna watoto ni nunda balaa lakini kumtusi sio dawa ni kuongeza tatizo
 
Back
Top Bottom