[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Polisi Marekani wakandamiza waandamanaji, watumia mabomu ya kutoa machozi[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD]
Mwamko wa wananchi wa Marekani ulioanza kwa jina la harakati ya "Wall Street" umeingia katika sura mpya baada ya polisi wa nchi hiyo kuweka wazi zaidi dhati yao halisi ya ukandamizaji dhidi ya raia.
Maandamano ya wananchi wa Oakland huko California ya kupinga mfumo wa kibepari nchini Marekani yamekandamizwa na polisi wa nchi hiyo waliotumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji hao waliokuwa wamepiga kambi katika eneo hilo.
Televisheni ya Euro News imeripoti kuwa mamia ya watu wameandamana huko Oakland kupinga kutiwa mbaroni wenzao walioshiriki kwenye harakati ya kupinga ubepari ya "Wall Street" na taarifa zinasema kwamba ukandamizaji huo wa polisi uliendelea hadi katikati ya usiku.
Watu 85 wameripotiwa kutiwa mbaroni na polisi katika maandamano hayo. Huku hayo yakiripotiwa, msemaji wa Baraza la Uhusiano wa Kiislamu la Marekani amesema kuwa, polisi wa Marekani FBI wanafanya njama za kuwazushia kesi za uongo Waislamu wa nchi hiyo.
Ibrahim Hooper ameiambia televisheni ya Press TV kuwa polisi wa FBI wanazifuata-fuata sana jamii za Waislamu nchini humo bila ya kosa wala dalili zozote za kufanya uhalifu.
Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, Waislamu nchini Marekani nao wamejiunga katika harakati ya "Wall Street" ya kupinga mfumo wa kibepari ambapo wanaharakati hao wanasema kuwa, asilimia moja ya Wamarekani inawadhulumu asilimia 99 ya wananchi wa nchi hiyo.
Source:
Polisi Marekani wakandamiza waandamanaji, watumia mabomu ya kutoa machozi[/TD]
[/TR]
[/TABLE]