Waliowahi kudrill maji ya chini nipeni uzoefu hapa.

Waliowahi kudrill maji ya chini nipeni uzoefu hapa.

IKIRIRI

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2018
Posts
2,734
Reaction score
3,027
1.bei ikoje kwa uchimbaji wa machine au Mkono.
2.wahusika wanao chimba wanapatikana wapi?
3.unawezaje kupata maji baridi?
4.changamoto zake zikoje
 
Kama upo Dar es Salaam fika sabasaba utapata majibu kwenye Banda la wizara ya maji. Au Chuo cha maji Ubungo pale kuna wakala wa serikali wa kuchimba visima.
 
1.bei ikoje kwa uchimbaji wa machine au Mkono.
2.wahusika wanao chimba wanapatikana wapi?
3.unawezaje kupata maji baridi?
4.changamoto zake zikoje
3..kipo kifaa cha kutoka urusi kinauzwa milioni saba kinapima umbali maji yalipo na kiasi cha chumvi kilichopo
 
uchimbaji wa mashine unapima kwa mita. ..ila kisima kirefu kuanzia m80 ni sh 12m
 
1.bei ikoje kwa uchimbaji wa machine au Mkono.
2.wahusika wanao chimba wanapatikana wapi?
3.unawezaje kupata maji baridi?
4.changamoto zake zikoje

Bei hazifanani kwasababu kuna maeneo maji yako chini sana na mengine hayako chini.. pia kabla hujachimba hakikisha unafanya survey kwanza kujua aina ya maji ya eneo lako sababu si kila maji yanayopatikana chini yanafaa kwa matumzi ya binadam.. wachimbaji wanapatikana kila sehemu ila kwa uhakika zaidi nenda pale DDCA ubungo maji watakushauri na kukupa huduma
 
1.bei ikoje kwa uchimbaji wa machine au Mkono.
2.wahusika wanao chimba wanapatikana wapi?
3.unawezaje kupata maji baridi?
4.changamoto zake zikoje
Kwanza kafanye geological survey!hii bei inategemea na eneo lililopo!ili upate kujua unachimba mita ngapi kupata maji!!na bei ya kuchimba haipo constant,unaweza kuambiwa kwa mita ni kias flani pamoja na PVC na gravel!
Kingine cha Tahadhari,si kila ukichimba maji lazima uyapate!!unaweza ukaambiwa kuna maji ukachimba ukakosa!!na kupata maji barid inawezekana kuzingatia na eneo lenyewe!
 
Tafuta ktk majirani zako kama 3 ili ujue wamepata maji mita ngapi
Maelewano ya uchimbaji yanategemea unachimba mita ngapi
Mimi kwangu maji yalipatikana mita 40 akaongeza mita 20 za ziada incase kutakuwa na draught napata maji matamu baridi
Kuna jamaa anaitwa Ahmed ndio amechimba kisima cha Msikiti wa Magomeni Kichangani, pale Mapipa keepleft ya Kawawa Rd + Morogoro Road, yuko vizuri ila inabidi ucheze nae bumper to bumper
Mimi kwa hiyo mita 60 gharama zote haikuzidi 4.5m
 
Back
Top Bottom