Waliosoma Diploma ya mifugo wapigwa chini

Waliosoma Diploma ya mifugo wapigwa chini

Jarateng

Senior Member
Joined
May 4, 2012
Posts
105
Reaction score
47
Sasa ni dhahiri kwamba serikali kupitia NACTE imewanyima nafasi ya kusoma vyuo vikuu wahitimu wa Diploma kutoka vyuo vya mifugo nchini! Hii ni hatari kwa sekta hiyo na wanafunzi hao ambao wanalazimika kusubiri hadi mwakani.

Wahitimu hao ambao wamesoma vyuo vya Tengeru, Mpwapwa, Morogoro, Madaba na kile cha Tanga; mpaka leo hii matokeo yao hayajathibitishwa na NACTE na hivyo hayajaingizwa kwenye mfumo wa udahili kwasababu maofisa wa NACTE hawana nafasi.

Awali nilikuwa nikifuatilia suala hili lakini majibu ya NACTE yalikuwa kwamba hawajapokea matokeo kutoka vyuo husika au kupitia wakala (LITA). Lakini nilipoanza kufuatilia kwa kufika ofisi husika nikianzia na TCU, NACTE, LITA na baadaye NACTE, nimegundua kuwa NACTE ilipokea matokeo hayo mapema mwezi Agosti lakini hadi leo wameshindwa kuitisha baraza lao ili kuyathibitisha na kuyaingiza kwenye mfumo ili wanafunzi waweze kuomba kudahiliwa. Ofisa mmoja wa NACTE niliyezungumza naye jana amenithibitishia kuwa licha ya kupokea matokeo kutoka LITA lakini hawajaitisha baraza lao kuyathibitisha na kuyaingiza kwenye mfumo.\

"Muda hautoshi kuitisha baraza, kuthibitisha matokeo na kuyaingiza kwenye mfumo kwasababu mfumo wa udahili unafungwa kesho (leo)" Na nilipomuuliza hatma ya wahitimu hao alinijibu kuwa kama haiwezekani hadi kesho wasubiri mwakani.... Dah hii ndiyo Tanzania ya Magufuli, huo ndio uwajibikaji. Inakuwaje fani nyeti kama hilo lisipewe kipaumbele mmmmhh.
 
Poleni vijana wa stashahada ya mifugo.

Hii ndiyo Tanzania ya magufuli vumilieni tu.
 
Mkuu ukiwa na elimu ya ufugaji na kilimo kichwani kwako, unachohitaji ni hekima tu ili kuwa tajiri, hakuna msaada mwingine unaohitaji.
 
Hii ni nchi ya viwanda,tunataka wafanyakaz wadogo wadogo kama nyiny wenye elimu
 
Mkuu ukiwa na elimu ya ufugaji na kilimo kichwani kwako, unachohitaji ni hekima tu ili kuwa tajiri, hakuna msaada mwingine unaohitaji.
Hawa hawahitaji msaada.

Wanahitaji kuendelea na masomo ya elimu ya juu kwa ngazi ya shahada.

Au ni dhambi kwa mtu aliye na stashahada kusoma elimu ya juu kwa ngazi ya shahada?.
 
Kwa nini hukulalamika kusoma diploma Mwaka 1? Big result now ndo Matokeo Yake . watu wa DAHP mna hali ngumu sana ata ki practical mko ovyo sana Na ndo mnapiga kelele . mfano . medicine 1, medicine 2 . pharmacology . systemic pathology . microbiology . anatomy & physiology & histology .surgery reproduction & obstetrical . parasitology . agribusiness 1. Agribusiness 11. Animal breeding . n.k diploma za sasa aya masomo ni ndoto kwenu . credit hrs ni ndogo ndo maana imeleta mkanganyiko nacte Na TCU . mwambie mr njaani mkurugenzi wa vyuo vya Mifugo afanye recup.
Mdawa wa elimu tz
 
Kwa nini hukulalamika kusoma diploma Mwaka 1? Big result now ndo Matokeo Yake . watu wa DAHP mna hali ngumu sana ata ki practical mko ovyo sana Na ndo mnapiga kelele . mfano . medicine 1, medicine 2 . pharmacology . systemic pathology . microbiology . anatomy & physiology & histology .surgery reproduction & obstetrical . parasitology . agribusiness 1. Agribusiness 11. Animal breeding . n.k diploma za sasa aya masomo ni ndoto kwenu . credit hrs ni ndogo ndo maana imeleta mkanganyiko nacte Na TCU . mwambie mr njaani mkurugenzi wa vyuo vya Mifugo afanye recup.
Mdawa wa elimu tz

Certificate tumesoma miaka miwili, iweje Diploma pia tusome miaka miwili?
 
Nendeni mkawashitaki.

Nakumbuka mwaka jana nilikua namsaidia mtu application, alisoma Diploma ya maendeleo ya jamii, Tengeru.

Nilihangaika sana, kumbe NACTE hawajaingiza matokeo ya wanafunzi wa Diploma 2014 kutoka Tengeru kwenye system...... Nilikomaa hadi nikaenda kwenye chumba chao cha watu wa IT, ndio wakaanza kutafuta CD ya matokeo..... Halafu eti wanaona uvivu kuyaingiza kwenye system, just ku upload data kwenye system ilikua shida.


INAWEZEKANA HAWAKUYAINGIZA MAANA HATA MWAKA HUU TUMEJARIBU KU APPLY, Kwenye system ya TCU hawana Diploma kutoka Tengeru ya 2014
 
Kwa nini hukulalamika kusoma diploma Mwaka 1? Big result now ndo Matokeo Yake . watu wa DAHP mna hali ngumu sana ata ki practical mko ovyo sana Na ndo mnapiga kelele . mfano . medicine 1, medicine 2 . pharmacology . systemic pathology . microbiology . anatomy & physiology & histology .surgery reproduction & obstetrical . parasitology . agribusiness 1. Agribusiness 11. Animal breeding . n.k diploma za sasa aya masomo ni ndoto kwenu . credit hrs ni ndogo ndo maana imeleta mkanganyiko nacte Na TCU . mwambie mr njaani mkurugenzi wa vyuo vya Mifugo afanye recup.
Mdawa wa elimu tz
Wewe umeenda Mzumbe umekuta wanasoma LAW miaka mitatu, uanze kulalamika why Tumaini wanasoma miaka minne.... Please

Kosa sio lao bali ni la wenye wizara na vyuo
 
Kwa nini hukulalamika kusoma diploma Mwaka 1? Big result now ndo Matokeo Yake . watu wa DAHP mna hali ngumu sana ata ki practical mko ovyo sana Na ndo mnapiga kelele . mfano . medicine 1, medicine 2 . pharmacology . systemic pathology . microbiology . anatomy & physiology & histology .surgery reproduction & obstetrical . parasitology . agribusiness 1. Agribusiness 11. Animal breeding . n.k diploma za sasa aya masomo ni ndoto kwenu . credit hrs ni ndogo ndo maana imeleta mkanganyiko nacte Na TCU . mwambie mr njaani mkurugenzi wa vyuo vya Mifugo afanye recup.
Mdawa wa elimu tz
Nani kasema hatujayasoma?... Sasa hio pathology tumesoma applied pathology..eti animal breeding...sasa mkuu utasomaje diploma ya mifugo kama huna animal breeding?...hilo tumelisima bana...hayo masomo yote unayoyataja tushayasoma...kwa taarifa tu...anatomy kwa diploma inaitwa developmental anatomy and physiology...sasa ukisema hatujasoma nakushangaa...
 
Nani kasema hatujayasoma?... Sasa hio pathology tumesoma applied pathology..eti animal breeding...sasa mkuu utasomaje diploma ya mifugo kama huna animal breeding?...hilo tumelisima bana...hayo masomo yote unayoyataja tushayasoma...kwa taarifa tu...anatomy kwa diploma inaitwa developmental anatomy and physiology...sasa ukisema hatujasoma nakushangaa...

Huyo sio wa kubishana naye, anahitaji kuombewa!
 
Back
Top Bottom