Waliomshambulia Tundu Lissu yatambueni haya...

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Mnatumia nguvu nyingi sana kufifisha nguvu ya hili lakini nawaapia kwa jina la Mwenyezi Mungu hamuwezi. Tafadhalini sana tambueni haya;

1.Jipeni moyo lakini shambulio la Lissu lilikua la kihuni na la kigaidi, hakuna aliyependezwa nalo, alipigwa bila hatia. Lazima mtambue kua sio wote waliopendezwa nalo huenda hata watekelezaji wa mipango hawako pamoja.

2.Kama mtu hakufa kwa Risasi zote hizo,Mungu ana mkono wake na muda utazungmza, jipeni moyo mtatajana moja baada ya mwingine.

3.Lissu ni kiongozi na Msomi hawezi kunyamazia unyama huo, anajua ni ipi njia sahihi ya kuwaweka wazi. Amesema yeye sio sawa na MO Dewji au Roma.

4.Majibu ya ni vipi alishambuliwa yanatakiwa kutolewa na vyombo vya Uchunguzi na sio kina Lugola ambaye ni mbunge wa CCM.

5.Mnatambua kua kitendo kilichofanyika ni cha kinyama, ilimwagika damu ya binadamu asiyekua na hatia. Mmevuna laana itakayowatafuna na Mungu aliyewaumbeni ninyi atashughulika na ninyi. Nendeni mkatubu kisha mkamwombe Lissu radhi.
 
waliomshambulia walikuwa watu wema sana.ukikengeuka ukauza utuwako na uthamani wa taifa laima ufe.

lisu anajua makosa yake ila Mungu amempa muda wa kutubu

bora wachache wapotee taifa libaki salama
Ni kifungu gani cha sheria kilicho halalisha unyama huo?

Kama alikuwa anakosea kwa mujibu wa sheria kwa nini asihukumiwe kwa mujibu wa sheria?

Ni kundi Fulani liliathirika na mpaka sasa linaweweseka kwa matendo ya haki ya comrade TL,likaona haliwezi kutumia sheria kama fimbo kwa sababu hakuwa na hatia,

Ndugu zangu duniani hapa tunapita,kila Siku tunawazika ndugu zetu ambao tulikuwa nao pamoja,na sisi tutaondoka pia hivyo hivyo,hatuna sababu ya kuutumia wakati adimu tulionao kuhalalisha unyama,Leo katendewa TL kesho atatendewa ndugu yako,tuweni mashabiki wa haki.

Tumejaliwa neema sisi tulio hai,kwa sababu tunayo nafasi ya kutenda HAKI,wafu hawana nafasi hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
waliomshambulia walikuwa watu wema sana.ukikengeuka ukauza utuwako na uthamani wa taifa laima ufe.

lisu anajua makosa yake ila Mungu amempa muda wa kutubu

bora wachache wapotee taifa libaki salama
Aisee kuna watu wa ajabu sana hapa duniani, ila tambua kwamba Mungu yupo na malipo ni hapa hapa DUNIANI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
waliomshambulia walikuwa watu wema sana.ukikengeuka ukauza utuwako na uthamani wa taifa laima ufe.

lisu anajua makosa yake ila Mungu amempa muda wa kutubu

bora wachache wapotee taifa libaki salama
Kama ndivyo, kwanini wanajificha na kutumia nguvu kubwa sana kutangaza uongo wa kitoto ambao unawasababishia kudhalilika mbele ya watanzania na dunia kwa jumla!...Mungu hapendi unafiki mtaumbuka
 
Halafu kuna watu wanasema alikuwa anaropoka sana hivi kukoso ni kuropoka, Kwani nchi yetu si inafuata utawala wa sheria mbona kesi zote alikuwa ameshafunguliwa mahakamani mlijuwa hatapatikana na hatia ndo mkaona apigwe risasi. Kwani mtu asipopatikana na hatia maana yake si hana kosa. Yaani baadhi ya watanzania wamefikia hatua ya kushabikia assassination kabisa. Tena kwa wazi kabisa tunashabikia damu ya wenzetu inapomwagika bila vyombo vya Dolan kuchunguza. Hivi huo ni ubinadamu kweli, mtu mzima na msomo kabisa unaandika ati CHADEMA wamrudishe Lisu na dereva wahijiwe. Wakati hakuna hata mtu mmoja mwengine aliyehojiwa na shambulio lilifanyika mchana. Halafu nchi ikiingia kwenye machafuko tunaanza kujiuliza nini kimesababisha kweli. Linapotokea jambo kubwa kama hilo Halafu mamlaka hazifanyi upelezi si ni mbinu ya kutaka taifa letu liingia kwenye machafuko?
 
Back
Top Bottom