Waliohamia CCM kwa kuunga juhudi wanajutia?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,288
12,579
Mwl. Nyerere alikuwa miongoni mwa vijana wanufaika wakuu wa Utawala wa Wakoloni. Alipata nafasi ya kusomeshwa hadi vyuo vikuu na alikuwa ana ajira kwenye serikali ya wakoloni na kupata mshahara. Hawa ndio waliopaswa kuunga juhudi kwelikweli za utawala wa mkoloni.

Uhuru wetu huenda ungechelewa sana kama akina Mzee Nyerere R.I.P wangekubali kuondoka TANU na kwenda kuunga juhudi za Governor katika kuwasomesha watoto wa machifu na kuwapatia ajira za kudumu.

Leo hii wako vijana ambao walipiganiwa kwa jasho na damu za wananchi wenzao wanaotafuta mabadiliko kwa njia za maumivu makubwa dhidi ya chama tawala ambao waliwasaliti wananchi hao na kurudi CCM kwa kisingizio cha kwenda kuunga juhudi hata kabla jasho, damu na majeraha ya walioumizwa wakati wa uchaguzi hayajakauka na kupona.

Sasa ni wakati wa chaguzi tena, hawa vijana hawako tena upande ule uliowafanya wajulikane, wako upande ule unaolalamikiwa na wapinzani kwa mambo mengi. Bahati mbaya wengi wa vijana hawa hawakukubalika mbele ya wajumbe wa chama tawala walikohamia, na hawana uhakakika kwamba wasiowapenda ni wajumbe tu au hata wana CCM na wanchi kwa ujumla.

Je, vijana hawa wanalifahamu kosa lao?
Je, vijana hawa wanaujuwa ukubwa wa kosa lao?
Je, vijana hawa wanajutia kosa lao au walichokipata wakati wa kuunga juhudi hakiwafanyi wajutie?
 
Njaa ukiichannganya na ubabaishaji halafu uingie kwenye siasa unaweza fanywa mboga
 
IMG_20200802_135940.jpg
 
Njaa ukiichannganya na ubabaishaji halafu uingie kwenye siasa unaweza fanywa mboga
Vijana ni kundi la watu kwenye taifa ambao wana kesho nyingi sana. Kama kijana ukiambiwa uchague kati ya hela na uaminifu chagua uaminifu, maana hela haitakupatia uwaminifu lakini uaminifu utakupatia hela na heshima ingawa inaweza kuwa kwa nyakati tofauti. vijana wetu wetu waliaminiwa na kupewa heshima kubwa sana na wananchi wenzao wakubwa na wadogo lakini wakachagua pesa kuliko heshima kwa kisingizio cha kuunga juhudi. Dhambi hii watagandamana nayo kwa muda mrefu sana.
 
Uzuri wa nchi yetu ina uhuru wa kila mtu kufanya kile anachoona ni sahihi kwake pasipo kuvunja sheria au kusigina katiba.

Kila mtu ashinde mechi zake
 
Wajumbe wanamchekea Magu na kukubali kila kitu machoni, moyoni wanamgomea.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawaeleki, waliimba hiyena hiyena kwenye awamu zote 5. Ni wanafiki, Wanashindwa kusema hapana waziwazi kwa wakubwa wao hata kama mambo hayaendi sawa. Wanasema hapana miyoni mwao. Wakati wapinzani wanasema hapana kwa mh. Makonda wao walikaa kimya, kumbe mioyoni mwao wana jambo, lakini wameshindwa kumweleza Mh. Rais
 
Atawapa nani u dc??? Nchi anaenda kukamata Tundu Antipas hii hapo October 2020. Mungu anaenda kuikomboa Tanzania rasmi
Mmmmh, eeee Lissu!! Atuambie kwanza ni mradi upi kati ya hii aliyoianzisha Rais Magufuli ataendelea nayo na ipi ataachana nayo (Kuhamia dodoma? kujenga flyovers?, kujenga reli ya sisasa?, kujenga bwawa la umeme Rufiji?, kupanua barabara? kuongeza ndege? kufufua reli?, kujenga viwanda? kununua meli mpya?, elimu bila mALIPO?, AU UPI?)
 
Back
Top Bottom