VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Wale wanafunzi kwa makumi waliofukuzwa au kusimamishwa masomo katika Chuo Kikuu cha Dodoma( UDOM) wako mbioni kurejeshwa.Taarifa nilizonazo zinaonesha kuwa hali hiyo inafuatia kuonekana kwa 'madudu' juu ya aliyewafukuza wanafunzi hao na kukiukwa kwa taratibu za kuwasimamisha/kuwafukuza.
Nyaraka nilizonazo zinaoonesha kuwa wanafunzi hao wamefukuzwa au kusimamishwa masomo na Wakuu wa Koleji au/na Kamati za Nidhamu za Koleji ambazo kisheria hazina mamlaka za kufanya hivyo. Nyaraka na sheria za Chuo zinaoonesha kuwa aliyepaswa kuwafukuza ni Kamati ya Nidhamu kwa Wanafunzi ya Chuo na si za Koleji.
Taarifa rasmi zinaoonesha kuwa tayari baadhi ya wanafunzi waliosimamishwa au kufukuzwa wameshafungua shauri Mahakama Kuu Dodoma kuiomba Mahakama hiyo kutengua amri batili ya kufukuzwa/kusimamishwa kwao. Wakati huo huo,uongozi wa UDOM umetakiwa kusawazisha mambo hayo nje ya Mahakama kwakuwa chuo kiliteleza kufikia maamuzi hayo. UDOM inapanga kujisahihisha ili kulinda heshima yake...
Nyaraka nilizonazo zinaoonesha kuwa wanafunzi hao wamefukuzwa au kusimamishwa masomo na Wakuu wa Koleji au/na Kamati za Nidhamu za Koleji ambazo kisheria hazina mamlaka za kufanya hivyo. Nyaraka na sheria za Chuo zinaoonesha kuwa aliyepaswa kuwafukuza ni Kamati ya Nidhamu kwa Wanafunzi ya Chuo na si za Koleji.
Taarifa rasmi zinaoonesha kuwa tayari baadhi ya wanafunzi waliosimamishwa au kufukuzwa wameshafungua shauri Mahakama Kuu Dodoma kuiomba Mahakama hiyo kutengua amri batili ya kufukuzwa/kusimamishwa kwao. Wakati huo huo,uongozi wa UDOM umetakiwa kusawazisha mambo hayo nje ya Mahakama kwakuwa chuo kiliteleza kufikia maamuzi hayo. UDOM inapanga kujisahihisha ili kulinda heshima yake...