Walimu wanaisoma namba kimya kimya! Maisha magumu (Elimu bure)

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,252
8,003
Naomba walimu wanisamehe bure maana huu ndio ukweli wenyewe halisi wa hali ilivyo mtaani.

Zamani walimu Walizoea kukusanya pesa kutoka kwa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya ziada yaani tuition. Sasa kufuatia agizo la serikali kwa agizo lake la Elimu bure na hakuna mwanafunzi atayechangishwa mchango wa aina yeyote imekua ni mwiba mkali sana kwa walimu hali inayowapelekea kuishi maisha magumu tofauti na awali.


Nimekutana na walimu watatu wakilia kwa sauti zinazofanana juu ya uamuzi huu wa serili na kuona ualimu ni kama kazi ya adhabu! Sasa wengine wanafikiria hata kutafuta madarasa nje ya shule na kuwatangazia wanafunzi hao hao wakutane nao huko huko.

" Kama darasa Lina wanafunzi 200 inamaana ukichangisha sh 1000 kilamwanafunzi kila mwezi inamaana utapata sh200,000 ambayo inakusaidia kwa mahitaji yako mengine,lakini sasa hatuna namna maisha yamekua magumu mno" hii ilikua ni kauli ya mwalimu moja wa shule moja ya sekondari hapa mkoani!

Kwa hali hii serikali iwafikirie wafanyakazi hawa zaidi maana kwa sasa hawana amani kabisa na maisha yao na wala hawafurahii kazi yao kama wafanyakazi wengine.
 
Tuition nafikiri ni maamuzi ya mwanafunzi na wazazi. Tatizo ni wasemewe kama hawafundishi inavyotakiwa darasani.

Zamani shule zilisomwa bila tabu na bila kuwepo tamaa za uroho wa pesa za walimu asilimia kubwa sanaaaaa.
 
Tuition nafikiri ni maamuzi ya mwanafunzi na wazazi. Tatizo ni wasemewe kama hawafundishi inavyotakiwa darasani.

Zamani shule zilisomwa bila tabu na bila kuwepo tamaa za uroho wa pesa za walimu asilimia kubwa sanaaaaa.
Kwa sasa unaambiwa maafisa Elimu hawataki kusikia kitu kinaitwa mchango kwa mwanafunzi! Hayo makubaliano yanafanyika wapi? Kuna afisa elim yeyote atakayekua tayari kupoteza nafasi yake ya kazi kwa kuona watoto wanachangishwa pesa za tuition? Wazazi wangapi wataokubaliana na hilo?
 
walimu waligeuza tuition ni miradi yao na wanafunzi wasiochangia walipea adhabu matokeo yake wanafunzi wasio na uwezo walikacha shule sababu wanazotoa ni za kijinga
 
Ila si mshahara umepanda tena au
Kupanda kwenyewe degree ni laki saba na certificate ni laki 4? Lakini kwa kazi yenyewe haifananii na mishahara hiyo maana na tunakoelea huko kubana matumizi ....
 
Mwalimu kakosa mtetezi na siku zote mbaya Wa mwalimu ni mwalimu mwenyewe a fisa elimu nae alikuwa mwalimu lakini akipewa hiko cheo nae anakuwa mtawalawa Wa kuwakandamiza walimu hakumbuki tena maslahi ya mwalimu mwenzie. Juzi jaji mkuu kalilia maslahi ya mahakimu na rais kaahidi kumpa hela ndani ya siku cha che je Mwl nani atamsemea
?
 
hili suala halihitaji ushabiki mi siwatetei waalimu lakini mtoto wangu hawezi acha kusoma tuition kwani hata hao wanaopigia chapuo elimu bure watoto wao hawasomi kwenye shule zenye wanafunzi 200 darasa moja kifupi ni kwamba wajinga ndio waliwao
 
Baadhi ya walimu wa shule kadhaa walikuwa wanacheza upatu na kila baada ya miezi miwili mmoja anatwaa mkoko, spacio, vitz, passo nk, hivo hao wanaolia na kulalamika as wale jamaa wa DECI ni kutokana na kujua washaliwa.
 
Thred za kijinga jinga kama hizi asbh asbh. Kunywa uji kwanza ujaze hilo tumbo akili ikae sawa uweze kuandika vya maana
 
hili suala halihitaji ushabiki mi siwatetei waalimu lakini mtoto wangu hawezi acha kusoma tuition kwani hata hao wanaopigia chapuo elimu bure watoto wao hawasomi kwenye shule zenye wanafunzi 200 darasa moja kifupi ni kwamba wajinga ndio waliwao
Shule zetu ni bora na zimeboreshwa. Hakuna sabb ya tuition. Huo ni wizi
 
Mwalimu kakosa mtetezi na siku zote mbaya Wa mwalimu ni mwalimu mwenyewe a fisa elimu nae alikuwa mwalimu lakini akipewa hiko cheo nae anakuwa mtawalawa Wa kuwakandamiza walimu hakumbuki tena maslahi ya mwalimu mwenzie. Juzi jaji mkuu kalilia maslahi ya mahakimu na rais kaahidi kumpa hela ndani ya siku cha che je Mwl nani atamsemea
?

Kweli Mkuu! hajawahi kutokea mtawala Mwalimu akawanufaisha Walimu. Adui wa mwlm ni mwlm.
 
Watanzania tunashangaza sana,sijui ni uwezo mdogo wa kufikiria au ni kukosa elimu ya kujitambua.
Hivi inakuwaje mzazi unafurahia mwanasiasa anayekwambia anatoa elimu bure,pasipo kukuhakikishia mazingira bora ya mwanao kujisomea ili aelimike,wakati huo mwanasiasa huyo huyo watoto wake kawapeleka shule binafsi na anagharamia mamilioni ya pesa,ili mwanaye apate elimu bora.Ajabu,mtanzania mwenzangu unafurahia wakati hali ya elimu inazidi kuwa mbaya kabisa!!
Kimsingi sipingi elimu kutolewa bure,inawezekana kabisa kutokana na rasilimali tulizonazo,lakini kabla ya kutangaza elimu kuwa bure,serikali ingetumia angalau mwaka mmoja kushughulikia matatizo ya msingi katika elimu,kwa mfano,wakati wazazi wakichangia uendeshaji wa shule kwa kiwango Fulani,serikali ingejikita kuhakikisha majengo ya kutosha yanajengwa,(kwa ubora),madawati yananunuliwa ya kutosha,na kushughulikia madai sugu ya walimu,(tukumbuke waziri ulisema walimu wanaidai serikali takribani bilioni 42,ingekuwa vema zile bilioni 100 na ushee zilizopelekwa kugharamia elimu bure kila mwezi,zingelipa madeni haya ya walimu).
Michango hii ingefutwa rasmi baada ya serikali kuwa imekusanya mapato ya kutosha,na kufanya utafiti wa kina katika sekta hii,lakini kwa hali ilivyo sasa nina mashaka makubwa kama tunachokifurahia kinakwenda kutupa matokeo chanya,tusubiri.
 
hili suala halihitaji ushabiki mi siwatetei waalimu lakini mtoto wangu hawezi acha kusoma tuition kwani hata hao wanaopigia chapuo elimu bure watoto wao hawasomi kwenye shule zenye wanafunzi 200 darasa moja kifupi ni kwamba wajinga ndio waliwao
mkuu umenena mambo machache lakini ya msing sana....

Wengi wa wanaopiga porojo, huenda watoto Wao wanasoma shule bnafsi zenye kila aina ya michango....lakini hawalalamiki...

Kiukweli mdogo wangu anaesoma form 3 staacha kumlipia hela ya tuition... kwa kuwa najua walim wa sayans ni wachache na hata form six leavers waliokuwa wanasaidia...wameachishwa kazi kwa shule kukosa hela za kuwalipa....
 
Mkuu wangu mleta mada umelenga mlemle....yani kati ya watu wanaoisoma namba in walimu...

Mm nmeshuhudia mmoja akimuombea magufuli are mapema!

Kuna shule walikuwa wanatoza 15,000 kwa kila mwanafunzi kwa mwezi....na asipolipa anarudishiwa had I alete....na wazazi nao walivyo kuwa mazuzu walikuwa wanalipa tena kwa lazima wakati twisheni ni hiari.

Ilifika mahala walimu hawaingii kwenye vipindi vya kawaida wanategea mda wa twisheni wapige hela..
 
Back
Top Bottom