Walimu Mkoa wa Arusha Wamtaka Lowassa Agombee Urais

Walimu Mkoa wa Arusha Wamtaka Lowassa Agombee Urais

Waalimu hawakuzungumzia CCM WALA CDM walizungumzia Suala la kumuunga mkono Mh. Lowasa kitu ambacho hata sehemu kubwa ya wapinzani wanamuunga mkono
 
Hao watakuwa walimu wa UPE, tena wale ambao ukiwazawadia vichupi wanaweza kukugeuza Mungu wao
 
Katika vuguvugu linalotokea sasa la wanasiasa wakongwe na baadhi yao vijana kushuhudiwa kutangaza nia imewafanya wanataaluma wa kada ya ualimu Mkoa wa Arusha kutumia fursa hiyo kumtaja mtu wanayemtaka.

Nikizungumza nao kwa pamoja walionyesha kuwa na imani ya hali ya juu kwa Mh. Lowassa na baadhi yao walikwenda mbali kwa kutoa takwimu za mambo aliyowahi kuyafanya ambayo yalisaidia kuinua elimu.

Mojawapo likiwa ni ujenzi wa shule za kata 1500 nchi nzima ambapo walidai baadhi yao wanafanya kazi huko.

Pili ni kwamba alipunguza tatizo la ajira kwa kada hiyo maaana shule zote hizo bado hazijapata waalimu wa kutosha hivyo kama sio jitihada zake tatizo la ajira kwa kada hiyo lingekua gumu na endelevu.

Pia waliendelea kusema alipunguza tatizo la watoto wa mitaani kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaa madarakani akiwa waziri mkuu na ndio maana miaka saba sasa toka astaafu kuna makundi kama panya road,Wamarekani weusi ambavyo ni vya kihalifu na hii ni kutokana na kuwa na watoto wa mitaani na ukosefu wa ajira.

Ukiachilia mbali masuala hayo pia walimsifu kwa utendaji wake na kwa kuwa na maamuzi magumu yasiyo tetereka na mwenye kujiamini achilia mbali misukosuko ya kisiasa aliyopitia ambayo ilipelekea kufanya maamuzi magumu ya kujiuzulu kunusuru chama na Taifa kwa ujumla wake.

Wakienda mbali zaidi walisema hata Kama itawezekana wao watahusika moja kwa moja kumchukulia fomu ya kugombea na kama ni kampeni watahakikisha wanakua nae pamoja kwani wanaamini Tanzania inamuhitaji yeye na so mtu mwingine kwa sasa.

Ikumbukwe kwamba Mwl. Ndiye aliyekuwa mkombozi wa Taifa hili kutoka kwa wakoloni hivyo ni jukumu la waalimu kuendelea kuhakikisha Taifa linakua ndani ya mikono salama.

Hayo yalisema na waalimu wa mkoa wa Arusha wakati wa maadhimisho ya miaka saba tika Mh.Lowassa ajiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu kutokana na makosa ya watendaji wa chini yake.

Nawasilisha

90%ya walimu nchi hii ni ukawa,hao waliobaki hawajielewi na wengi wao ndio wanastaafu!

Serikali haiwajali walimu hivyo hakuna mwalimu anayesapoti CCM
 
Hao watakuwa walimu wa UPE, tena wale ambao ukiwazawadia vichupi wanaweza kukugeuza Mungu wao

Sidhani kama waalimu wa UPE bado wapo labda uje na takwimu kutuonyesha kama bado wapo
 
Si kweli kuwa walimu ni UKAWA; wangekuwa huko CCM isingekuwepo madarakani. Walimu wengi ni CCM bwana...!


ndugu takwimu gan ulzotumia? au kutoka chanzo kip cha taarifa?

hiyo taarfa ya kwamba walmu wamesema wapo tayar kumuunga mkono na ikibid kumchukulia fomu ni za kizush na za kupuuzwa.
mwalimu ni mtumish wa umma asiyetakiwa kujiusisha na siasa,labda kupiga kura tu_____na walimu wa sasa si sawa na walimu enz za mwalm____kwa hiyo usitegemee unayofikiria kutoka kwa walim ambapo mlikuwa mnawaburuza mnavyo taka.
 
Subirini april 30 ndio mtajua waalimu ni ukawa au ccm,ndio mtapata majibu sahihi kwamba walimu wa sasa wamepinda,wamekatika au ni legelege,nadhani mtoa mada hata vyombo vya habari hufuatilii maana hata yale maazimio na msimamo wa walimu uliotolewa mwishoni mwa wiki iliyopita huna habari kabisa..
 
ndugu takwimu gan ulzotumia? au kutoka chanzo kip cha taarifa?

hiyo taarfa ya kwamba walmu wamesema wapo tayar kumuunga mkono na ikibid kumchukulia fomu ni za kizush na za kupuuzwa.
mwalimu ni mtumish wa umma asiyetakiwa kujiusisha na siasa,labda kupiga kura tu_____na walimu wa sasa si sawa na walimu enz za mwalm____kwa hiyo usitegemee unayofikiria kutoka kwa walim ambapo mlikuwa mnawaburuza mnavyo taka.

Ww nani kakuambia hawatakiwi kujihusisha na mustakabali wa Nchi hii? Mbona kitila mkumbo ni mtumishi wa Umma pia hapa ni nyadhifa ndio hazitakiwi kwa kuwa kutakua na conflict of interest waalimu wameamka ss wamechoka kulalama wanafanya vitendo
 
Niko nawalimu hapa wanasema hili jungu limepikwa Munduli wamekata huu upuzi wao wapo ukawa wanajuta kitu ccm wanachowafanyia

Walimu wa monduli wa wamesema hao. Unategemea waseme nini kwenye jimbo la fisadi?
 
Bila ubishi Mhe LOWASA ana sifa za kuongoza kitaifa na kimataifa. Mimi naahidi kumtolea milioni moja ya kuchukua fomu ya kugombea URAIS ndani ya chama kubwa CCM
 
Bila ubishi Mhe LOWASA ana sifa za kuongoza kitaifa na kimataifa. Mimi naahidi kumtolea milioni moja ya kuchukua fomu ya kugombea URAIS ndani ya chama kubwa CCM

Ndio muda ukifika tutaungana pamoja kwa hilo" maamuzi na tumaini jipya na Edward Lowassa 2015"
 
Ww nani kakuambia hawatakiwi kujihusisha na mustakabali wa Nchi hii? Mbona kitila mkumbo ni mtumishi wa Umma pia hapa ni nyadhifa ndio hazitakiwi kwa kuwa kutakua na conflict of interest waalimu wameamka ss wamechoka kulalama wanafanya vitendo


usibwabwaje tu, we fuatilia kitabu cha "code of conducts" kwa mtumishi wa uma, mstakabali wa nchi ni pamoja na ufundishaji na majukumu mengine yote ya shuleni. Mtumish wa umma ukitaka kutekeleza siasa sharti uache kazi hiyo ya utumishi wa umma ndipo ukapifanikishe siasa zako.Kitila mkumbo alikumbana na mshikemshike ktk kujihusisha kwake na siasa, lakin hatima ya mshike mshike ndo sijajua.

Wewe kama ni mwalimu wa kawaida nakushauri usijaribu kamwe kujihusiha na au kushiriki siasa, sababu kanuni na taratibu za utumishi wa umma mara nyingi zinafanya kazi [ziko strict] kwa wadogo {watumish wa umma vidagaa} na si watumishi wa umma vigogo,kuthibitisha hilo ni nafasi ya wakuu wa mikoa na wilaya ambao kwa upande mmoja wa shilingi ni wajumbe ktk vikao vya vyama-CCM wakati upande mwingine wa shilingi ni watumishi wa umma. Na kanuni na taratibu za utumishi wa umma haziwagusi. :A S-frusty2:
 
Back
Top Bottom