harakat
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 2,887
- 1,359
Katika vuguvugu linalotokea sasa la wanasiasa wakongwe na baadhi yao vijana kushuhudiwa kutangaza nia imewafanya wanataaluma wa kada ya ualimu Mkoa wa Arusha kutumia fursa hiyo kumtaja mtu wanayemtaka.
Nikizungumza nao kwa pamoja walionyesha kuwa na imani ya hali ya juu kwa Mh. Lowassa na baadhi yao walikwenda mbali kwa kutoa takwimu za mambo aliyowahi kuyafanya ambayo yalisaidia kuinua elimu.
Mojawapo likiwa ni ujenzi wa shule za kata 1500 nchi nzima ambapo walidai baadhi yao wanafanya kazi huko.
Pili ni kwamba alipunguza tatizo la ajira kwa kada hiyo maaana shule zote hizo bado hazijapata waalimu wa kutosha hivyo kama sio jitihada zake tatizo la ajira kwa kada hiyo lingekua gumu na endelevu.
Pia waliendelea kusema alipunguza tatizo la watoto wa mitaani kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaa madarakani akiwa waziri mkuu na ndio maana miaka saba sasa toka astaafu kuna makundi kama panya road,Wamarekani weusi ambavyo ni vya kihalifu na hii ni kutokana na kuwa na watoto wa mitaani na ukosefu wa ajira.
Ukiachilia mbali masuala hayo pia walimsifu kwa utendaji wake na kwa kuwa na maamuzi magumu yasiyo tetereka na mwenye kujiamini achilia mbali misukosuko ya kisiasa aliyopitia ambayo ilipelekea kufanya maamuzi magumu ya kujiuzulu kunusuru chama na Taifa kwa ujumla wake.
Wakienda mbali zaidi walisema hata Kama itawezekana wao watahusika moja kwa moja kumchukulia fomu ya kugombea na kama ni kampeni watahakikisha wanakua nae pamoja kwani wanaamini Tanzania inamuhitaji yeye na so mtu mwingine kwa sasa.
Ikumbukwe kwamba Mwl. Ndiye aliyekuwa mkombozi wa Taifa hili kutoka kwa wakoloni hivyo ni jukumu la waalimu kuendelea kuhakikisha Taifa linakua ndani ya mikono salama.
Hayo yalisema na waalimu wa mkoa wa Arusha wakati wa maadhimisho ya miaka saba tika Mh.Lowassa ajiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu kutokana na makosa ya watendaji wa chini yake.
Nawasilisha
Nikizungumza nao kwa pamoja walionyesha kuwa na imani ya hali ya juu kwa Mh. Lowassa na baadhi yao walikwenda mbali kwa kutoa takwimu za mambo aliyowahi kuyafanya ambayo yalisaidia kuinua elimu.
Mojawapo likiwa ni ujenzi wa shule za kata 1500 nchi nzima ambapo walidai baadhi yao wanafanya kazi huko.
Pili ni kwamba alipunguza tatizo la ajira kwa kada hiyo maaana shule zote hizo bado hazijapata waalimu wa kutosha hivyo kama sio jitihada zake tatizo la ajira kwa kada hiyo lingekua gumu na endelevu.
Pia waliendelea kusema alipunguza tatizo la watoto wa mitaani kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaa madarakani akiwa waziri mkuu na ndio maana miaka saba sasa toka astaafu kuna makundi kama panya road,Wamarekani weusi ambavyo ni vya kihalifu na hii ni kutokana na kuwa na watoto wa mitaani na ukosefu wa ajira.
Ukiachilia mbali masuala hayo pia walimsifu kwa utendaji wake na kwa kuwa na maamuzi magumu yasiyo tetereka na mwenye kujiamini achilia mbali misukosuko ya kisiasa aliyopitia ambayo ilipelekea kufanya maamuzi magumu ya kujiuzulu kunusuru chama na Taifa kwa ujumla wake.
Wakienda mbali zaidi walisema hata Kama itawezekana wao watahusika moja kwa moja kumchukulia fomu ya kugombea na kama ni kampeni watahakikisha wanakua nae pamoja kwani wanaamini Tanzania inamuhitaji yeye na so mtu mwingine kwa sasa.
Ikumbukwe kwamba Mwl. Ndiye aliyekuwa mkombozi wa Taifa hili kutoka kwa wakoloni hivyo ni jukumu la waalimu kuendelea kuhakikisha Taifa linakua ndani ya mikono salama.
Hayo yalisema na waalimu wa mkoa wa Arusha wakati wa maadhimisho ya miaka saba tika Mh.Lowassa ajiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu kutokana na makosa ya watendaji wa chini yake.
Nawasilisha