Walimu Mkoa wa Arusha Wamtaka Lowassa Agombee Urais

Walimu Mkoa wa Arusha Wamtaka Lowassa Agombee Urais

harakat

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
2,887
Reaction score
1,359
Katika vuguvugu linalotokea sasa la wanasiasa wakongwe na baadhi yao vijana kushuhudiwa kutangaza nia imewafanya wanataaluma wa kada ya ualimu Mkoa wa Arusha kutumia fursa hiyo kumtaja mtu wanayemtaka.

Nikizungumza nao kwa pamoja walionyesha kuwa na imani ya hali ya juu kwa Mh. Lowassa na baadhi yao walikwenda mbali kwa kutoa takwimu za mambo aliyowahi kuyafanya ambayo yalisaidia kuinua elimu.

Mojawapo likiwa ni ujenzi wa shule za kata 1500 nchi nzima ambapo walidai baadhi yao wanafanya kazi huko.

Pili ni kwamba alipunguza tatizo la ajira kwa kada hiyo maaana shule zote hizo bado hazijapata waalimu wa kutosha hivyo kama sio jitihada zake tatizo la ajira kwa kada hiyo lingekua gumu na endelevu.

Pia waliendelea kusema alipunguza tatizo la watoto wa mitaani kwa kipindi cha miaka miwili tu aliyokaa madarakani akiwa waziri mkuu na ndio maana miaka saba sasa toka astaafu kuna makundi kama panya road,Wamarekani weusi ambavyo ni vya kihalifu na hii ni kutokana na kuwa na watoto wa mitaani na ukosefu wa ajira.

Ukiachilia mbali masuala hayo pia walimsifu kwa utendaji wake na kwa kuwa na maamuzi magumu yasiyo tetereka na mwenye kujiamini achilia mbali misukosuko ya kisiasa aliyopitia ambayo ilipelekea kufanya maamuzi magumu ya kujiuzulu kunusuru chama na Taifa kwa ujumla wake.

Wakienda mbali zaidi walisema hata Kama itawezekana wao watahusika moja kwa moja kumchukulia fomu ya kugombea na kama ni kampeni watahakikisha wanakua nae pamoja kwani wanaamini Tanzania inamuhitaji yeye na so mtu mwingine kwa sasa.

Ikumbukwe kwamba Mwl. Ndiye aliyekuwa mkombozi wa Taifa hili kutoka kwa wakoloni hivyo ni jukumu la waalimu kuendelea kuhakikisha Taifa linakua ndani ya mikono salama.

Hayo yalisema na waalimu wa mkoa wa Arusha wakati wa maadhimisho ya miaka saba tika Mh.Lowassa ajiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu kutokana na makosa ya watendaji wa chini yake.

Nawasilisha
 
Umekazana sana kusema. Naomba utumie jitihada hizoizo kusema chanzo cha utajiri alionao huyu mheshimiwa. Maana mara ng'ombe, uridhi, ai sei noo
 
Waambieni walimu hao kwamba rais mzuri mwenye maadili ambaye atarudisha heshima ya taifa hili ameisha patikana, mda wa marais wahuni ambao huenda kupiga deal Ikulu haupo hivyo wamwambie huyo Lowassa wao atafute kazi ingine .Ikulu yetu imepata mwenyewe ambaye akitajwa kila mtu atasema yessssss.
 
Toa ujinga wako hapa. Usiwasemee walimu jambo ambalo hawajalisema. Walimu wana chama chao cha walimu na msemaji wao ni rais wa chama cha walimu ambaye ni Adrian Mukoba. Uchunguzi wa karibuni kabisa wa ndani ya CCM ulisema walimu wengi kwa sasa wanaunga mkono Upinzani(UKAWA).
 
Hao waalimu wamechagua fungu jema maana ktk wote wanaotaka kiti yy ndio haswa mwenye sifa za msingi na ikumbukwe kwamba waalimu ni kundi maalum ktk jamii
 
Mimi mwenyewe nataka Lowassa agombee urais,kugombea si kugombea tu hata kichaa rukhusa kugombea.
 
Walimu wapi hao, maana walimu wote awapo UKAWA
 
Raisi wa wezi na matapeli,aende akaongoze malaika band
 
Toa ujinga wako hapa. Usiwasemee walimu jambo ambalo hawajalisema. Walimu wana chama chao cha walimu na msemaji wao ni rais wa chama cha walimu ambaye ni Adrian Mukoba. Uchunguzi wa karibuni kabisa wa ndani ya CCM ulisema walimu wengi kwa sasa wanaunga mkono Upinzani(UKAWA).

Si kweli kuwa walimu ni UKAWA; wangekuwa huko CCM isingekuwepo madarakani. Walimu wengi ni CCM bwana...!
 
Hao waalimu wamechagua fungu jema maana ktk wote wanaotaka kiti yy ndio haswa mwenye sifa za msingi na ikumbukwe kwamba waalimu ni kundi maalum ktk jamii

Walimu hawadanganyiki tena mwendo no uleule Wa 2010. Mnawafanya mtaji wakati mlisema kura zao hamzitaki.
 
Mh.lowasa anazungumzia Elimu,elimu, elimu hapa ni kwamba lazima udeal na waalimu maana wao ndio key player kwenye hilo na si vinginevyo. Na wala hajawahi Lowasa kuwabeza waalimu hata siku moja na anawaheshimu na kuwapenda sana
 
naungana nao moja kwa moja bila kuchelewa,Edward anatosha 2015
 
Niko nawalimu hapa wanasema hili jungu limepikwa Munduli wamekata huu upuzi wao wapo ukawa wanajuta kitu ccm wanachowafanyia
 
Niko nawalimu hapa wanasema hili jungu limepikwa Munguli wamekata huu upuzi wao wapo ukawa wanajuta kitu ccm wanachowafanyia

Munguli ndio wapi?naomba urudi shule waalimu wakakufundishe ndio uje huku maana hata unavyoandika unaonekana una shida kubwa kimtizamo na kiakili
 
Back
Top Bottom