Mbona mashambulizi yameelekezwa kwa mtoa mada? majipu yana ushirikiano sana pindi yanapoona mikasi na pini na iodine tinture ya kusafishia vidona vinapowekwa mezani. Magu kawafunga kamba hatoroki mtu. Mtatumbuliwa tu hata mkitoa povu humu.
Haya maswali yako yanapaswa kujibiwa na mleta mada (tetesi).
Mimi toka mwanzo nimemwambia kuwa hoja yake iko nusu nusu, haieleweki. Na kama ni mwanafunzi mtahaniwa, amejibu swali nusu na obvious hawezi kupata alama za swali hilo!!
Bahati mbaya sana kwake, badala atoe ufafanuzi tumwelewe ili tuchangie tukiwa tunaelewana, aliishia kuniambia nimekurupuka!!
Hoja yake ingekuwa clear kama ingejibu maswali haya;
• Ni wangapi hao walimu?
• Kwa nini walikuja kuhakikiwa kama wanajijua walishafukuzwa kazi?
• Nani alikuwa anachukua mishahara yao iwapo ilikuwa inakuja ili hali si watumishi tena?
Wahasibu wa wilaya walikuwa wanachukua wakishirikiana na maofisa wa utawala(Accoutants and human resource offcers) walikuwa wanachukua mishahara kwani pay points hujulikana.