Wale tuliowahi kuishiwa nauli katika mishemishe tukutane hapa tuelezee tulifanyaje tukapata nauli

Nimetoka Dar nimeahidiwa tumiwa nauli, nikazama Darlux la Arusha nikamwambia Konda mpaka Chalinze nauli fresh!

Kibaha hola, naanza tetemeka, sina vocha sina kitu, wala message, aliyeahidi kimya, nikashushwa chalinze, nikatafuta mahali nikakaa!

Nimekaa mpaka saa 12 sijawa, sijanywa sina Vocha’s sina kitu, akatokea Mzee akanambia Kijana Nimekuona toka asubuhi shida nini?

Nikamweleza, akanambia chukua bag twende, kudadadeki, kanipeleka Guest kalipa 25,000/- nikaanza ogopa, akanipa cash 40,000/- akanambia Safari njema kesho!

Kaondoka, nikasema hapa yaweza kuwa msala siamini amini, cha kwanza nikahama Chumba, cha pili nikaenda tafuta chakula!

Sikuwahi mwona tena yule Mzee mpaka Leo wala hakurudi!
ilikuwa mwaka gani?
 
Nili print kutoka Kariakoo mpaka Kinondoni Studio...

Ilikua ni utoto, hela niliimaliza kununulia mazaga huku naona kabisa ikiwa inaisha, sababu nilikua mdogo na sijawahi kupata shida yoyote ya kiuchumi, basi nilihisi mtoto mdogo hawezi kua na shida popote wakubwa wakamuacha......
Yani niliamini tuu wakiniona natembea kwa mguu wataniuliza halafu nikiwaambia nitapata msaada...kuomba niliona aibu sana, lakini pia inahitaji timing la sivyo nita aibika zaidi.

Shaaabash, labda wakubwa wa peponi.....

Nikaenda kwenye duka la Anko (ilikua nikienda na bimkubwa hua tunapitia hivyo nikawa napafahamu) kufika kashafunga maana ilikua 12 jioni,
Nikaenda kwa rafiki yake mzee, kufika napo chenga....

Sasa hapa ndio utoto ukaanza kunitoka,

Kumbuka hapo kinachonitesa eti ni Sh 100 ya nauli ya mwanafunzi, na kilichonipeleka k.koo ni kwenda mchikichini kununua notes na mazaga mengine ya shule,
Hela iliyobaki ndio nikaitumia kipuuzi...

Kuomba nako nahisi aibuuu,

Kwa ufupi Nikakanyaga raba, Mbaya zaidi njiani nikakutana na vibaka wakapita na yale mazaga yote ambayo ndio yaliyonifanya ni nitembee (ilikua nguo na viatu) halafu wakaniachia yale mahitaji yaliyonipeleka Kariakoo(vitabu, daftari n.k) tena walitaka wapite na begi lote ila sijui wakashauriana nini, basi mmoja akaniita halafu akanirushia begi maana nilishaakimbia.

Kwa ufupi nilikaribishwa ukubwani kwa Tanzania Shilling Mia moja( 100)..
ikawaje mwisho wake?
 
Mara mbili nimepata huo msukosuko wa kuishiwa nauli.
1. Nikiwa mdogo kama wa miaka12 nilikuwa naishi na mama nilikwenda Tabata kutoka Manzese kumsalimia baba ( kwa sasa ni marehemu). Kumbe baba alisafiri na familia yote mimi sikujua kumbuka kipindi hicho simu za mkononi hakuna, nikapewa nauli na jirani yake baba na kipindi hicho nauli ya mwanafunzi sh.tano. Alinipa sh.20, baadae yule alienipa nauli alikuja kumuoa mtoto wa kufikia wa Baba, nikajiongeza kuwa ile nauli ilikuwa na maana kubwa kwangu.
2. Napenda sana mpira wa miguu na Yanga ndio timu niipendayo, mwaka 2001 Yanga ilikuwa inarejea kutoka Zimbabwe baada ya kupata ushindi hivyo yaliandaliwa mapokezi makubwa. Nikaenda club Jangwani kuvizia mabasi ya bure yalioandaliwa kupeleka mashabiki nikakosa nafasi. Mfukoni nina sh.100 tu na kipindi hicho nauli ya mwanafunzi sh. 50, nilikuwa form four. Nikafikiria nikisema niende Uwanja wa ndege wakati wa kurudi nitakosa nauli ya kutoka kariakoo hadi nyumbani.
Nikaona kuliko nikose haya mapokezi acha tuu niende nitajua huko huko, nikaenda Airport tukaipokea timu mida ya saa mbili usiku. Wakati wa kurudi ndio akili ikakaa sawa nina sh. 50 tu ya kunifikisha kariakoo na muda huo ni kama saa tatu hivi. Nikapanda Hiace ya kariakoo, mule ndani ya gari kulikuwa na jamaa nikaona acha nimwambie ukweli nisije kuumbuka leo. Nilivyomuhadithia alicheka sana akasema nyie watu wa Yanga mna matatizo sana. Akaniambia haya tulia mtani mi Simba utafika tu nyumbani. Kumbe na yeye anaelekea Ubungo hivyo tukapanda gari moja akanilipia nauli na akanipa sh. Mia.
 
Hahaha zamani nilikuwa napenda kuzuzura mno hiyo hali imenitokea mara mbili ila utoto raha unaogopa kuomba hela lakini baadaye yanakushinda unajikuta umeomba tu .
 
Kuishiwa nauli hilo ni jambo la kawaida sana,sema vijana wa sikuhizi wamekuwa wavivu sana kutembea!
Yaani unataka kuniambia kwamba endapo kwa bahati mbaya umepoteza/kupungukiwa nauli halafu na wewe labda unakaa kimara na wakati huo upo kwenye mizunguko yako kariakoo utashindwa kutembea kutoka kkoo mpaka kimara?
Vijana hebu punguzeni uvivu!!
 
Siji sahau kidato cha tano, uko katavi tumefanya mgomo baada ya kikao cha bodi wanafunzi wote tukafukuzwa apo sina hata mia nikauza memory nauli inatosha mpaka sumbawanga mjini apo sina ndugu wala mtu ninaye mfahamu ila nilifika mbeya mungu mkuu.
 
Nimetoka Dar nimeahidiwa tumiwa nauli, nikazama Darlux la Arusha nikamwambia Konda mpaka Chalinze nauli fresh!

Kibaha hola, naanza tetemeka, sina vocha sina kitu, wala message, aliyeahidi kimya, nikashushwa chalinze, nikatafuta mahali nikakaa!

Nimekaa mpaka saa 12 sijawa, sijanywa sina Vocha’s sina kitu, akatokea Mzee akanambia Kijana Nimekuona toka asubuhi shida nini?

Nikamweleza, akanambia chukua bag twende, kudadadeki, kanipeleka Guest kalipa 25,000/- nikaanza ogopa, akanipa cash 40,000/- akanambia Safari njema kesho!

Kaondoka, nikasema hapa yaweza kuwa msala siamini amini, cha kwanza nikahama Chumba, cha pili nikaenda tafuta chakula!

Sikuwahi mwona tena yule Mzee mpaka Leo wala hakurudi!
Mtu Kama huyo niliwahi kutana nae nikiwa kwenye hood ya Iringa-Moshi enzi hizo zinapita Morogoro. Wenye roho za namna hii wabarikiwe Sana.
 
Sijui kama ni wewe japo sikumbuki vizuri kuna jamaa alikuwa kabeba bag akaniomba nauli kapungukiwa nkampa buku tuliomba chenji kwa muuza machungwa na alinikuta naongea na simu
 
Sijui kama ni wewe japo sikumbuki vizuri kuna jamaa alikuwa kabeba bag akaniomba nauli kapungukiwa nkampa buku tuliomba chenji kwa muuza machungwa na alinikuta naongea na simu
Unakumbuka ulikuwa unatoka wapi
 
Ni mida ya jioni nashuka kwenye boti ya Azam kutoka bongo Islamic state (Zanzibar).​

Mfukoni nimebakiwa na Shilingi mia tano huku Safari yangu inabidi nielekee Mbezi Kimara, simu imezima chaji lakini pia safari yangu toka Bongo Islamic state ikiwa ni ya shida maana nilienda kiutafutaji huko Zenji nimefika Zenji ikawa magumashi nikaamua kugeuza dsm baada ya kukosa mishe na sehemu ya kukaa.​

Niliposhuka kwenye boti nikatembea mpaka mnazi mmoja huku nawaza nafikaje mbezi.​

Basi nikasimama pale mnazi najiuliza hapa nimuombe nani daah nikakumbuka katika mishemishe zangu mjini hapa nilishwahi kutana na watu mbalimbali wamepungukiwa nauli na unakuta yupo smart kimuonekano anakuomba umuongezee nauli nikawa nafikiri Ni matapeli.​

Leo nami nikasema hamna namna hapa nimueleze mtu yeyote anisaidie japo elfu moja ili niongezee nauli.​

Basi nikamuona kijana anaongea na simu pale baada ya kumaliza nikamface nikamweleze shida yangu mshikaji akazama mfukoni akanipatia elfu moja nilimshukuru sana yule kijana hakika umeniokoa Mungu akubariki sana.​

Hakika watu wema bado wapo kijana umenisaidia sana.​
Unakosaje sehemu ya kukaa Zenji? Kwani hauna makalio? Zenji Kinyeo mtaji bro hujakitumia vizuri ungeweza hata kumiliki Alphard.siku nyingine tumia mtaji wa tako Bro
 
Unakosaje sehemu ya kukaa Zenji? Kwani hauna makalio? Zenji Kinyeo mtaji bro hujakitumia vizuri ungeweza hata kumiliki Alphard.siku nyingine tumia mtaji wa tako Bro
[/QUOTE
Koment hii mbaya Sana kwenye Uzi wangu natamani ningekuwa na uwezo ningeifuta.
Kichwa chako kimejaa mavi huna akili hata avatar yako inaonesha kabisa.
 
Mimi nakumbuka tulikuwa matembezini na rafiki na ghafla wallet yangu nikaiacha kwenye handbag yake..nimeshuka gari nipande gari ya kwenda kwetu naangalia kwenye pochi sioni wallet..duh!!..nikicheki mkononi Nina 150 na nauli 400..nikakaa kituoni nikaona upuuzi..nikamfuata konda nikamuelezea ukweli akaniruhusu nipande gari..dah!! Ila nikikumbuka nacheka sana
 
Nimetoka Dar nimeahidiwa tumiwa nauli, nikazama Darlux la Arusha nikamwambia Konda mpaka Chalinze nauli fresh!

Kibaha hola, naanza tetemeka, sina vocha sina kitu, wala message, aliyeahidi kimya, nikashushwa chalinze, nikatafuta mahali nikakaa!

Nimekaa mpaka saa 12 sijawa, sijanywa sina Vocha’s sina kitu, akatokea Mzee akanambia Kijana Nimekuona toka asubuhi shida nini?

Nikamweleza, akanambia chukua bag twende, kudadadeki, kanipeleka Guest kalipa 25,000/- nikaanza ogopa, akanipa cash 40,000/- akanambia Safari njema kesho!

Kaondoka, nikasema hapa yaweza kuwa msala siamini amini, cha kwanza nikahama Chumba, cha pili nikaenda tafuta chakula!

Sikuwahi mwona tena yule Mzee mpaka Leo wala hakurudi!
Malaika wapo mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom