Dejane
JF-Expert Member
- Jan 1, 2014
- 49,659
- 68,625
Jana tumeshuhudia kina mama wengi waliotelekezwa na watoto wakiwa kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar Mh. Makonda, ni jambo zuri lakini nadhani si zuri kivile maana sijajua kajipangaje ili uwe mpango wa kudumu ikiwezekana kina mama wasihangaike tena au kulalamika kuhusu kutelekezwa na kina baba.
Mimi nadhani hilo swala lisingekuwa la Dar peke yake tulifanye la Tanzania nzima, maana navyojua kuna wizara husika inahusika na hili na wala hawafatilii.
Kwanini Makonda asingejipanga hilo swala likajadiliwa upya bungeni na wizara husika ili kupanga mipango madhubuti ya kuwadhibiti wanaume/waume wanaokimbia familia zao au wanaozalisha hovyo hovyo, ikawekwa sheria kali ili mtoto apate haki zake za msingi na sio kutafuta kiki kwa muda mfupi inakuwa kama haijatusaidia wanawake.
Tunaomba wizara husika iangalie hili swala na sheria ziwe kali ili watoto watunzwe na wapangiwe kiasi cha kutoa kwa mwezi, sheria zibadilishwe maana hali ya maisha imezidi kuwa juu maisha yamekuwa magumu na wahitaji ni wanawake wa Tanzania nzima sio Dar tu tunaomba tueleweke kwa hili.
Serikali pia tunaomba iongeze somo la ziada na semina mbali mbali za kuwaelimisha watoto wa kike wajue wanatakiwa umri gani wawe na watoto, matumizi ya condom ikiwezekana watoto wanapovunja ungo waanze kugawiwa condom maana hata tusipowapa wanafanya wafundishwe mapema na kujiepusha na mapenzi katika umri mdogo basi wakizidiwa watumie zana, ili kujiepusha na magonjwa na mimba zisizotarajiwa.
Tukatae tukubali watoto wanafanya mapenzi wakienda tuition, shuleni, tukubali tu watumie condom tukiwaelewesha nadhani itasaidia ili tupunguze watoto wa sio na walezi wengi najua wengine mtaponda ila ukweli ndio hivyo hali ni mbaya mitaani kwenye jamii zetu watoto wengine sana mimba wakiwa wadogo unadhani watafanyaje mtoto anazaa mtoto mwenzie bora waelimishwe au kuna njia nyingi za kuzia mimba zifanywe kila mzazi atambue hilo tukiwaachia ni mimba tu .
Wanaume na nyie tumieni Condom mbona hamna huruma kabisa mnatembea na vitoto vidogo kama watoto wenu kwa kuvilaghai kutokana na umaskini wanaume Hamna huruma na upendo kabisa baadhi yenu, mkiwapa mimba watunzeni mpaka muitwe na Mkuu Mkoa jamani.
Wakuu wa mikoa mnahangaika kweli mwingine kaita wanawake, mwingine kaenda fundisha shuleni kazi ipo mwaka huu.
Bila kusahau na nyie wanawake msirubunike na msipende kutumiwa kwa muda mfupi.
Mimi nadhani hilo swala lisingekuwa la Dar peke yake tulifanye la Tanzania nzima, maana navyojua kuna wizara husika inahusika na hili na wala hawafatilii.
Kwanini Makonda asingejipanga hilo swala likajadiliwa upya bungeni na wizara husika ili kupanga mipango madhubuti ya kuwadhibiti wanaume/waume wanaokimbia familia zao au wanaozalisha hovyo hovyo, ikawekwa sheria kali ili mtoto apate haki zake za msingi na sio kutafuta kiki kwa muda mfupi inakuwa kama haijatusaidia wanawake.
Tunaomba wizara husika iangalie hili swala na sheria ziwe kali ili watoto watunzwe na wapangiwe kiasi cha kutoa kwa mwezi, sheria zibadilishwe maana hali ya maisha imezidi kuwa juu maisha yamekuwa magumu na wahitaji ni wanawake wa Tanzania nzima sio Dar tu tunaomba tueleweke kwa hili.
Serikali pia tunaomba iongeze somo la ziada na semina mbali mbali za kuwaelimisha watoto wa kike wajue wanatakiwa umri gani wawe na watoto, matumizi ya condom ikiwezekana watoto wanapovunja ungo waanze kugawiwa condom maana hata tusipowapa wanafanya wafundishwe mapema na kujiepusha na mapenzi katika umri mdogo basi wakizidiwa watumie zana, ili kujiepusha na magonjwa na mimba zisizotarajiwa.
Tukatae tukubali watoto wanafanya mapenzi wakienda tuition, shuleni, tukubali tu watumie condom tukiwaelewesha nadhani itasaidia ili tupunguze watoto wa sio na walezi wengi najua wengine mtaponda ila ukweli ndio hivyo hali ni mbaya mitaani kwenye jamii zetu watoto wengine sana mimba wakiwa wadogo unadhani watafanyaje mtoto anazaa mtoto mwenzie bora waelimishwe au kuna njia nyingi za kuzia mimba zifanywe kila mzazi atambue hilo tukiwaachia ni mimba tu .
Wanaume na nyie tumieni Condom mbona hamna huruma kabisa mnatembea na vitoto vidogo kama watoto wenu kwa kuvilaghai kutokana na umaskini wanaume Hamna huruma na upendo kabisa baadhi yenu, mkiwapa mimba watunzeni mpaka muitwe na Mkuu Mkoa jamani.
Wakuu wa mikoa mnahangaika kweli mwingine kaita wanawake, mwingine kaenda fundisha shuleni kazi ipo mwaka huu.
Bila kusahau na nyie wanawake msirubunike na msipende kutumiwa kwa muda mfupi.