Wakuu habari..

Political stability

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2021
Posts
905
Reaction score
1,410
Nimefungua sehem ya kuuza mayai ya kisasa na kienyeji, kwa bei ya leja leja na jumla..

Sasa, naomba ushahuri, bidhaa gani nyingine niweke kwenye , atleast ambayo itafanya ofisi iwe busy kidogo,

 
Uza na baadhi ya vifaa vinavyo hitajika katika kufuga kuku mfano ndoo za Maji...Kama kwenye attachment hapo chini.

Lakini pia unaweza kuanza kuuza vyakula vya kuku..more advanced na packed product na sio kumwaga mapumba...

Unaweza pia kuuza packed product za lishe kwa watoto...mfano unga wa ulezi ulio na sura nzuri.... Ila Jitahidi Sana duka liwe attractive kutokana na bidhaa zako.

Mwisho# angalia changamoto za wafugaji mtaa unaoishi.. zile simple product.
 
Mimi naona biashara ya mayai ukiongeza na uuzaji wa gesi itakuwa zinaendana mkuu!
Ningesema pia uweke na kizimba cha kuuzia kuku hapo nje lakini hapana.
 
Mimi naona biashara ya mayai ukiongeza na uuzaji wa gesi itakuwa zinaendana mkuu!
Ningesema pia uweke na kizimba cha kuuzia kuku hapo nje lakini hapana.
Big point hapo kwenye gas,

Kwanini hapana, kuweka kuku?
 
Big point hapo kwenye gas,

Kwanini hapana, kuweka kuku?
uuzaji wa kuku una changamoto zake mkuu, hasa kama soko lako si uhakika, wataakaa sana kwenye kizimba na itapelekea wapungue mno uzito, ila kama uhakika wa soko upo weka.
 
uuzaji wa kuku una changamoto zake mkuu, hasa kama soko lako si uhakika, wataakaa sana kwenye kizimba na itapelekea wapungue mno uzito, ila kama uhakika wa soko upo weka.
Labda nifanye hivi...mzigo unafikia home, nakuwa nachukua wachache naweka kwenye kizimba
 
Mimi naona biashara ya mayai ukiongeza na uuzaji wa gesi itakuwa zinaendana mkuu!
Ningesema pia uweke na kizimba cha kuuzia kuku hapo nje lakini hapana.
WAUZA GESI BANA UKIFUATILIA FAIDA WANAYOPATA UNAWEZA KULIA
 
WAUZA GESI BANA UKIFUATILIA FAIDA WANAYOPATA UNAWEZA KULIA

MTUNGI MDOGO WENYE UJAZO WA KILO 6,
FAIDA NI 2,500/-.

NA KWA JINSI BIASHARA HUSIKA ILIVYOKUWA SATURATED MTAANI,
KUNA UWEZEKANO WA KUKAA SIKU TANO HUJAPATA MTEJA.

AU NASEMA UONGO MKUU?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…