Sumba-Wanga
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 5,349
- 1,224
Ni kawaida sana kwa wakina mama kutimbana na wakwe zao. Hii nimeiona live wakati nasoma sekondari, niliwahi kukaa kwa dada yangu ambaye mama mkwe wake alikuwa ni moto, na bahati mbaya shemeji alikuwa hana msimamo!
mambo ya mama mke ni magumu sana. Mara utasikia wewe mwanamke gani hujui kumtunza mwanangu, mara hujafundwa kwenu. basi ni shida tu kati wanawake hawa wawili muhimu sana na kila mmoja ana umuhimu wake wa kipekee katika maisha ya kijana (mama na mke)! Achague wapi?
Hapo bado hatujawagusa mawifi, hasa wale kula kulala wasio na kazi, hawajaolewa na ambao ndoa zao zimewashinda! Kaka ndio mkombozi, basi wifi yupo kikaangoni! Utasikia mwanamke mbaya sana huyu, ana roho mbaya! Anakula tu pesa ya kaka yetu, toka aolewe hatuna amani kabisa humu ndani? Jamani! Nilikuwa najiuliza sana wakati nikiaa kwa dada yangu, Si ni kwake? Mnataka kulala na kaka yetu!! Nikawa sipati picha na mimi nikiolewa mambo ni haya haya!
Msumali wa mwisho kwenye jeneza ni pale mke asipojaliwa kupata mtoto, utasikia mwanamke gani huyo anatujazia choo tu hapa!
Habari nzuri, baba mkwe mara nyingi anakuwa hana taabu kabisa na mwali wake, lakini mama mkwe, ni chungu!
Jamani, hili jambo limefanya ndoa nyingi sana kuvunjia, mapenzi kupata machungu makubwa sana, watoto kuhangaika!
Ni nini hasa jamani? tufanye nini kuwasaidia walio kwenye huo moto? Wanandoa wanawezaje kukabiriana na hali hiyo? NIna wasi wasi kuwa wengine hata kabla ya kuletewa mkwe wameshagombana nae wanamsubiri kwa hamu! Kuna mtaalamu mmoja wa saikolojia aliwahi kusema kuwa chanzo kikubwa ni mapenzi ya mama kwa mwanae wa kiume, ambayo anaona kama mwanamke mwingine anaingilia kati......? Sina hakika.
Wa JF tuwasaidie wale waliopo kwenye janga hili. Kwa nini African families, upande wa mume wanakuwa wakorofi sana?
mambo ya mama mke ni magumu sana. Mara utasikia wewe mwanamke gani hujui kumtunza mwanangu, mara hujafundwa kwenu. basi ni shida tu kati wanawake hawa wawili muhimu sana na kila mmoja ana umuhimu wake wa kipekee katika maisha ya kijana (mama na mke)! Achague wapi?
Hapo bado hatujawagusa mawifi, hasa wale kula kulala wasio na kazi, hawajaolewa na ambao ndoa zao zimewashinda! Kaka ndio mkombozi, basi wifi yupo kikaangoni! Utasikia mwanamke mbaya sana huyu, ana roho mbaya! Anakula tu pesa ya kaka yetu, toka aolewe hatuna amani kabisa humu ndani? Jamani! Nilikuwa najiuliza sana wakati nikiaa kwa dada yangu, Si ni kwake? Mnataka kulala na kaka yetu!! Nikawa sipati picha na mimi nikiolewa mambo ni haya haya!
Msumali wa mwisho kwenye jeneza ni pale mke asipojaliwa kupata mtoto, utasikia mwanamke gani huyo anatujazia choo tu hapa!
Habari nzuri, baba mkwe mara nyingi anakuwa hana taabu kabisa na mwali wake, lakini mama mkwe, ni chungu!
Jamani, hili jambo limefanya ndoa nyingi sana kuvunjia, mapenzi kupata machungu makubwa sana, watoto kuhangaika!
Ni nini hasa jamani? tufanye nini kuwasaidia walio kwenye huo moto? Wanandoa wanawezaje kukabiriana na hali hiyo? NIna wasi wasi kuwa wengine hata kabla ya kuletewa mkwe wameshagombana nae wanamsubiri kwa hamu! Kuna mtaalamu mmoja wa saikolojia aliwahi kusema kuwa chanzo kikubwa ni mapenzi ya mama kwa mwanae wa kiume, ambayo anaona kama mwanamke mwingine anaingilia kati......? Sina hakika.
Wa JF tuwasaidie wale waliopo kwenye janga hili. Kwa nini African families, upande wa mume wanakuwa wakorofi sana?