GE2025 Wakili William Maduhu: Tunakwenda kwenye Uchaguzi ikiwa bado kuna Vilio vya Kutotendewa haki, uchaguzi wa Mwaka huu hauna Uhalali wa Kisiasa

GE2025 Wakili William Maduhu: Tunakwenda kwenye Uchaguzi ikiwa bado kuna Vilio vya Kutotendewa haki, uchaguzi wa Mwaka huu hauna Uhalali wa Kisiasa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Wakili William Maduhu Mchambuzi wa Masuala ya Kisiasa akizungumza katika Mdahalo wa Jicho la Wanasheria Uchaguzi Mkuu 2025 kipindi cha Star TV ameelezea Taswira halisi kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 kwamba bado kuna vilio vingi sana na malalamiko ya wadau wengine kutotendewa haki na waliopo Madrakani, ikizingatia sifa kuu za uchaguzi ambazo ni Uhalali wa kisheria na kikatiba (Legal legitimacy) na uhalali wa kisiasa

Pia ameshauri Serikali kutopuuza au kudharau Sauti na maoni ya Wananchi kwani Wananchi ndiyo Serikali


 
Hawa wahuni wanajua vizuri sana na wameonywa na watu mbalimbali na karibuni Bw.Polepole lakini wamekataa katakata ,kwa hili la political legitimacy haliwashughulishi
 
Hapo nyuma nimewahi kusema kwamba CCM wajuavyo wao wanaimiliki nchi hii kama wanavyoumiliki Uwanja wa CCM Kirumba. Hakuna wa kuwapangia cha kufanya!
 
Tanzania hatuuhitaji uhalali wa KISIASA. Tunahitaji Uhalali wa KIKATIBA na KISHERIA. Waliogomea kisiasa wasubiri mchakato wa KISIASA baada ya uchaguzi tujadiliane Kwa sasa haiwezekani!!😩😩
 
Back
Top Bottom