Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM kutoka mkoa wa Kilimanjaro na Wakili wa Mahakama kuu Bw. Tumsifu Kweka, leo Jumanne Julai Mosi, 2025, amechukua fomu ya kuwania nafasi ya uteuzi wa kugombea ubunge katika Jimbo la Siha, akiahidi kuendeleza maendeleo ya wananchi na kusimamia itikadi ya chama endapo Chama chake kitampitisha.
Wakili Kweka amesema ametimiza haki yake yakidemokrasia ndani ya chama kwa kuchukua fomu ya kuwania ubunge katika Jimbo hilo, akiwaomba wananchi wa Siha kumpatia fursa ya kuwawakilisha na kushirikiana nao ili kuleta maendeleo katika jimbo la Siha.
Soma Pia: Uzi maalum wa wanaotia nia kugombea Ubunge Uchaguzi Mkuu 2025
Aidha amebainisha kuwa anatosha katika nafasi hiyo kutokana na uzoefu alionao pamoja na kuzijua fursa na changamoto za Jimbo hilo,akieleza kuwa amepata fursa ya kuisoma ilani ya CCM ya mwaka 2025/30 na hivyo inahitaji mtu ambae anaweza kukimbizana na maendeleo ya nchi lakini pia yeye sio muumini wa siasa za maneno bali yeye ni muumini wa siasa za vitendo.
Wakili Kweka amesema ametimiza haki yake yakidemokrasia ndani ya chama kwa kuchukua fomu ya kuwania ubunge katika Jimbo hilo, akiwaomba wananchi wa Siha kumpatia fursa ya kuwawakilisha na kushirikiana nao ili kuleta maendeleo katika jimbo la Siha.
Soma Pia: Uzi maalum wa wanaotia nia kugombea Ubunge Uchaguzi Mkuu 2025
Aidha amebainisha kuwa anatosha katika nafasi hiyo kutokana na uzoefu alionao pamoja na kuzijua fursa na changamoto za Jimbo hilo,akieleza kuwa amepata fursa ya kuisoma ilani ya CCM ya mwaka 2025/30 na hivyo inahitaji mtu ambae anaweza kukimbizana na maendeleo ya nchi lakini pia yeye sio muumini wa siasa za maneno bali yeye ni muumini wa siasa za vitendo.