GE2025 Wakili Tumsifu Kweka, amechukua fomu kuwania Ubunge Jimbo la Siha Kupitia CCM

GE2025 Wakili Tumsifu Kweka, amechukua fomu kuwania Ubunge Jimbo la Siha Kupitia CCM

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Wakili wa kujitegemea Tumsifu Kweka, ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Kilimanjaro pamoja na Mkutano Mkuu wa CCM Taifa, leo amejitokeza rasmi kuchukua fomu za kuwania ubunge katika Jimbo la Siha kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Kweka alifika katika Ofisi za CCM wilaya ya Siha asubuhi ya leo akiwa ameongozana na mkewe, katika tukio lililoshuhudiwa na wanachama na wafuasi wa chama hicho, huku akipokelewa kwa shangwe na matumaini kutoka kwa baadhi ya wananchi waliohudhuria

Hatua ya Kweka kuingia katika kinyang’anyiro hicho inaongeza ushindani ndani ya CCM katika safari ya kutafuta mgombea atakayebeba bendera ya chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025

Soma pia:
Akizungumza kwa kifupi baada ya kuchukua fomu, Wakili Kweka alieleza kuwa amesukumwa na dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa Siha kwa kutumia weledi wake katika sheria na uzoefu wa kisiasa alionao ndani ya chama.
“Ni wakati wa kuunganisha nguvu za kijamii, kiuchumi na kisheria kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Siha,” alisema Kweka

Zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu linaendelea katika ofisi za CCM wilayani humo, huku wanachama na wafuasi wakifuatilia kwa karibu majina ya watia nia wanaojitokeza kutaka kuwania nafasi ya ubunge kupitia chama hicho tawala


 
Back
Top Bottom