Wakili msomi Joseph Kinango amesema Waziri Mwakyembe avuliwe ujumbe wa TLS

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Wakili msomi Joseph Kinango amesema tamko la Waziri Mwakyembe kuwa ataifuta TLS ni batili na halina mashiko kisheria. Kwa lugha ya kisheria "Its null and void abinitio" yani ni tamko batili hata kabla Mwakyembe hajalitamka. Yani wakati Mwakyembe anafikiria kutamka tayari lilikua batili.

Hii ni kwa sababu ili ufute TLS inabidi ufute sheria inayoanzisha TLS (The Tanganyika Law Society Act). Na sheria hiyo haiwezi kufutwa kienyeji. Inabidi ipelekwe bungeni na bunge liifute. Ikitokea hivyo athari zake ni kama ifuatavyo:

1. Mawakili wote nchini wanapoteza uhalali wa kuwa mawakili, maana sifa mojawapo ya kuwa wakili ni kuwa member wa TLS.

2. Sheria takribani 200 zinazotaja au kutambua uwepo wa mawakili inabidi zifutwe au zifanyiwe marekebisho ili kuondoa application ya mawakili katika sheria hizo.

3. Bodi za taasisi kadhaa nchini inabidi zifanyiwe marekebisho maana kuna bodi ambazo Rais wa TLS ni mjumbe.

4. Sifa za kumpata Gavana wa BOT inabidi zibadilishwe maana moja ya watu wanaoweza kuteuliwa kuwa Gavana ni pamoja na Wakili wa mahakama kuu.

5. Sifa za kuwapata majaji nchini inabidi ziwe reviewed maana mojawapo ya sifa ni kuwa wakili wa mahakama kuu (na mahakama zilizopo chini yake).

6. Chuo cha mafunzo ya sheria (School of Law) kinachofunza na kuandaa mawakili inabidi kifungwe maana hakitakuwa na tija tena kwa nchi.

[HASHTAG]#NiniKifanyike[/HASHTAG]:
1. Tamko la Waziri Mwakyembe linafaa kupuuzwa. Halina mantiki.

2. Waziri Mwakyembe avuliwe ujumbe wa TLS. Haiwezekani aendelee kuwa mjumbe wa Taasisi ambayo anafikiria kuifuta.

So jambo la kwanza kwa mawakili wakifika Arusha tar 17 March, kabla ya kupiga kura ya kumchagua Lissu kuwa Rais wao, wanapaswa wapige kura ya kumfuta uanachama wa TLS Mwakyembe.
 
Upo sahihi kwa nini mnawaita wakili msomi? kwani mtu anaweza kuwa wakili na asipitie shule? mbona hamsemi daktari msomi? wahasibu wasomi? wahandisi wasomi? rekebisheni naona mnakosea kuweka hicho kivumishi cha sifa katika fani ya Elimu...
 
Upo sahihi kwa nini mnawaita wakili msomi? kwani mtu anaweza kuwa wakili na asipitie shule? mbona hamsemi daktari msomi? wahasibu wasomi? wahandisi wasomi? rekebisheni naona mnakosea kuweka hicho kivumishi cha sifa katika fani ya Elimu...
wakili aliekua nakremu na haelewi ndo kama hawa sasa wanataka kujidelete wenyewe...utamwita mtu kama huyo msomi kweli???
 
Upo sahihi kwa nini mnawaita wakili msomi? kwani mtu anaweza kuwa wakili na asipitie shule? mbona hamsemi daktari msomi? wahasibu wasomi? wahandisi wasomi? rekebisheni naona mnakosea kuweka hicho kivumishi cha sifa katika fani ya Elimu...
Visifa vya:
Mwandamizi, Bingwa, Aliebobea nk. kama vinavyotumika kwa Wanataaluma anuai hamjawahi kuvisikia?

Huu ni Wivu tu.

Acheni wapambwe tu,

Kama unalichukia Hilo kula 'KONOKONO'.
 
Kuitwa mtu "Wakili Msomi" ni jina pendwa la kada ya uwakili. Sasa ukichukizwa hicho ni kijiba cha roho tu. Kila fani ina "teminolojiizz" zake. Wakili wa Sheria hapendi kujiita "lidokta lisomi"! Love it or hate it, it strikes while the iron still hot!
 
Wewe unajadili jina la Wakili Msomi au mada? Kasomee na wewe
Upo sahihi kwa nini mnawaita wakili msomi? kwani mtu anaweza kuwa wakili na asipitie shule? mbona hamsemi daktari msomi? wahasibu wasomi? wahandisi wasomi? rekebisheni naona mnakosea kuweka hicho kivumishi cha sifa katika fani ya Elimu...
 
Rudini kwenye hoja achaneni na huyu anayewatibua na chuki ya neno " wakili msomi"
 
Nimetokea kulichukia sana hili neno wakili msomi
Kwani wewe taaluma yako ni ipi?! Undeni kivumishi chenu nanyi mjisifie maana kuchukia hiki cha wenzio haikusaidii, utaendelea kukisikia na kukisoma mpaka unaondoka dunia hii!
 
Back
Top Bottom