Kazi ipo!
Na hii ni kwa mujibu wa Kampuni / Taasisi ya Utafiti ya huko Ulaya iitwayo Charities Aid Foundation ( CAF ) ambao imedai kwamba Wakenya na nchi yao kwa ujumla ndiyo wanaongoza kwa kuwa na roho nzuri, ukarimu na huruma kuliko Waafrika wengine wote na wapo katika nafasi ya nane ( 8 ) Kidunia.
Nimejaribu kwa hali na mali kuitafuta nchi ya Tanzania hadi ' top 80 ' hadi hivi sasa sijaiona ila kama kuna Mwenzangu yoyote hapa aliyeiona Tanzania katika Utafiti huu anisaidie kuniambia ipo nafasi ya ngapi.
Hongereni sana na mno Wakenya na ama hakika kwa aina ya ' Matabasamu ' ya Rais wenu Uhuru Kenyatta na Makamu wake William Ruto na huku mara kwa mara wakionyesha ' Uungawana ' wao hadharani na kuwaunganisheni nyote bila kujali Dini zenu, Makabila yenu na tofauti zenu za Kisiasa hakika mnastahili.
Wewe kama kila siku tu Watu ni Kutekana, Kukomoana, Kupigana Majungu, Kutupana Baharini na Mitoni huku wengine wakipewa rushwa kuhama kutoka upande mmoja kuja mwingine na hapo hapo tena mara mwingine akigoma kuhamia upande fulani basi anabambikiwa Kesi ya ' Ufisadi ' na hujakaa sawa Mtu anaona raha kumuona Mwenzake akiwa na Shida na wala hapendi Kusaidia na Mwenyezi Mungu nae tumeshamsahau hiyo Roho Nzuri kama ya Wakenya tuitoe wapi?
Shikamooni Wakenya wote!
Source: Standard Digital.com
Nawasilisha.