Wakenya na Watanzania, Njooni

Wakenya na Watanzania, Njooni

MwendaOmo

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2013
Posts
778
Reaction score
727
Hamjambo wana JF. Mie ni mwananchi wa Kenya na nina nia ya kuchangia mabadiliko kwenye sekta ya elimu nchini Kenya. Jambo la kwanza ambalo ningependa kuangazia ni lugha inayotumika kuwafundishia watoto.
Naamini kuwa ni vyema mtoto afundishwe kwa lugha anayoielewa vyema. Kwa maoni yangu, lugha Kamilifu (ideal,) ni ile ya mama; lakini ile inayowezekana (practical) ni lugha ya Kiswahili. Ingawa sera ya Wizara ya elimu ni kuwa lugha ya mama itumike vijijini na ile ya Kiswahili au kiingera vitumike mijini hadi darasa la tatu, hakuna vitabu vyovyote ambavy vimeandikwa kwenye lugha hizi. Jambo la ajabu ni kuwa hata yale makampuni ya kuchapisha vitabu ambavyo vinamilikiwa na serikali, Kama vile the Kenya Literature Bureau, na The Jomo Kenyatta Foundation, vinatoa vitabu ambavyo vimeandikwa kwa kiingeraza, isipokuwa vile vitabu vinavyo fundisha lugha hiyo kama somo.
Kwa hivyo, ninataka niandike vitabu vya darasa la kwanza vya Sayansi, Somo la Jamii, Somo La Dini (Christian Religious Education,) na Hesabu. Niko na changamoto kadhaa;


1. Mara nyingi mie nimehusiana na watoto na hao huniambia kuwa wana shida kusoma katika lugha ya Kiswahili. Hii ni kwa sababu Kiswahili, ingawa ni 100% phonetic, ni lugha amalgamated na kwa hivyo huwa na maneno marefu sana. Je, wale wantanzania ambao mlisomea lugha ya Kiswahili katika shule za msingi, kati ya kusoma kiingereza ambacho si 100% phonetic lakini sio amalgamated na kusoma Kiswahili ambacho ni 100% phonetic lakini ni amalgamated; ni gani heri?
2. Kwa watanzania waliotumia Kiswahili katika shule ya msingi, mlipoenda katika shule za upili, mlipata shida yoyote kuelewa vitabu vya kiingereza? Je, ikiwa ulipata shida hii, utailaumu medium of instruction ama utailaumu shule yako/mwalimu wako?


3. Kuna shida ya rote memorization katika shule nyingi za Kenya; naamini hii ni kwasababu ya kutumia lugha ya kiingeraza. Huko Tanzania, shida hii imekithiri? Na wale wlioelewa wakiwa shule ya msingi, walipofika shule za upili, walizidi kuelewa au walianza kukariri wasioelewa (intellectual vomit?)


4. Shule zinazotumia kiingereza (English medium) hao hufanya mtihani wa darasa la saba kwa kiingereza au Kiswahili?


5. Kuna software gani ya bure inayotumika kuhadhiri maandishi katika lugha ya Kiswahili?


6. Kwa mkenya ulio hapa, reaction yako itakuwa ipi ukiambiwa kuwa medium of instruction imebadilishwa hadi Kiswahili?


Asanteni sana kwa maoni yenyu.


P.S. Nitapachika hapa kijitabu ambacho natayari na nitaomba maoni yenyu
 
vitabu vya kiswahili vya science kwa shule ya msingi vipo vingi tu mimi mwenyewe nimevitumia wakati nasoma shule ya msingi...hujataka tu kuvitafuta
 
shule zinazotumia kiingereza (english medium) hufanya mtihani wa darasa la saba kwa kiingereza, huwa zinatafsiriwa to english, wale wanotumia kiswahili hufanya mitihani kwa kiswahili.
 
Fundisheni Kiswahili kama somo mpaka Chuo kikuu.
Acha watu waendelee kujifunza kwa kiingereza.
Wakati ukifika lugha imekua watajua cha kufanya.
 
Lugha ni tatizo sana, binafsi nilipokua shule ya msingi nilikuwa na uelewa mzuri kabisa, vitu nilivyosoma sijapata kuvisahahu mpaka leo. Shule ya msingi nimesoma mambo mengi sana ambayo sekondari wenda yanaenda kwa level ile ile, ila watu wanafeli tu kwa sababu ya lugha.

Mfano, shule ya msingi nimejibu maswali ya nini na wapi mwanamtapa? nimejibu dola ya mali, shona na zulu. Mfalme chaka, dola ya benin nk.
Wakati darasa la tano nimesoma nne jeografia ya Tanzania,jeografia ya Afrika darasa la tano, darasa la sita jeografia ya ulimwengu, na darasa la saba nimesoma afrika mashariki.

Sayansi nimesoma vitu vile vile wengi wakifika sekondari ama elimu ya pili uliyoiita vinawashinda. Mfano nimesoma mfumo wa umengenyaji, maumbile ya mtu wanyama mamaria, amfibia, leptilia nk.
Ama nimesoma Mchapuko = mwendokasi gawia mda yani acceleration = velocity over time. Nimesoma Uzito na tungamo yani weight and mass. Nimesoma, msongamano =tungamo gawia ujazo yani density = mass over volume.

Pia nimesoma mkondo wa umeme na tofauti za kipoteshali yani current and potential difference. Bila kusahau ile kitu ya muungano wa chembechembe ndogo sana .... yani atom.

Kwa kweli elimu ya msingi ilikuwa tamu sana na nilikuwa sihitaji kujisomea, kwa sababu mwalimu alikuwa akiongea nilikuwa na muelewa kwa ufasaha na hivyo sikuhitaji kujisomea badala yake nilipotoka skuli nilienda kupiga sembo yani mpira wa kujitengeneza wa karatasi na matambala.

Cha moto kwa kweli nilikiona ktk elimu ya sekondari, kwa sababu mwalimu alikuwa akiongea nilikuwa sielewi anaongea kwa undani nini anaongelea. Na material ya sekondari ni yaleyale tu ya shule ya msingi japo yame advance kidogo, kitu ambacho kilitakiwa kisiwe tatizo kabisa. Lakini cha maajabu kiligeuka kuwa tatizo kubwa ikabidi kuwa nalala darasani na maji kwenye karai na mbu kunikung'uta.

Mfano somo la jeografia kwa sekondari utakuta wamepiga picha wananchi wakivuna kakao ama karafuu harafu wanakuuliza unafikiri hilo ni zao gani na wanafany nini? ni swali lile lile ktk shule za msingi tulikokuwa tukiulizwa. Ama mfano sendondari watakuliza collapse of mwanamutapa empire--- kitu kile kile tulikuwa tunaulizwa darasa la tano sababu za kuanguka dola ya mwanamtapa. Kumbe tatizo linakuja kuwa na lugha.

Serikali za afrika nafikiri zinabidi zichague lugha ya kufundishia masomo yote kwa ngazi zote, na hiyo lugha lazima wahikikishe inaeleweka vyema toka chekechea ili kuweza kuwa na mabadiriko chanya ktk nyanja ya elimu. Studying by heart, hakutatunusuru kamwe.
 
Swala la lugha mbilii tofauti huko chini na huku juu its total nonsense, na ndio namba 1 cause ya watu kufeli tanzania, tukifika huku juu tunaanza kurudia ya nyuma na hapo ndipo watoto walisoma shule za bei kubwa magep yanapoanza since wako safi katika ngeli, kama ni ngeli basi weka chini hadi juu, likewise kama ni kiswahili the same thing ila tukiweka kiswahili tukumbuke kua tusitegemee vitabu tu, information nyingi tutashindwa kuzipata mfano kwenye internet, research watu tunachimba sana huku looking for answers, angalia vitu kama english documentaries za science, kama hujui ngeli hata kdg hutodaka term za kisayansi zile, bongo hatuweki info zozote kwenye net zinazohusu elimu, hatufanyi discussion ya topics nyingi, mfano bongo ulisikia wapi mtu anafundisha astronimy kwa kiswahili au hata kwa ngeli afu akaupload? tukiweka ngeli itarahisisha since resources zote zipo kwa lugha yao, kiswahili tutatumia nje tu ya darasa maana watu wataanza ohh lugha ya taifa, ohh uzalendo, english nani alikwambia ni lugha ya mwingereza au mmarekani? si waweke patent sasa mtu asitumie bila ruhusa yao? lugha ni ya binadamu full stop.
 
Swala la lugha mbilii tofauti huko chini na huku juu its total nonsense, na ndio namba 1 cause ya watu kufeli tanzania, tukifika huku juu tunaanza kurudia ya nyuma na hapo ndipo watoto walisoma shule za bei kubwa magep yanapoanza since wako safi katika ngeli, kama ni ngeli basi weka chini hadi juu, likewise kama ni kiswahili the same thing ila tukiweka kiswahili tukumbuke kua tusitegemee vitabu tu, information nyingi tutashindwa kuzipata mfano kwenye internet, research watu tunachimba sana huku looking for answers, angalia vitu kama english documentaries za science, kama hujui ngeli hata kdg hutodaka term za kisayansi zile, bongo hatuweki info zozote kwenye net zinazohusu elimu, hatufanyi discussion ya topics nyingi, mfano bongo ulisikia wapi mtu anafundisha astronimy kwa kiswahili au hata kwa ngeli afu akaupload? tukiweka ngeli itarahisisha since resources zote zipo kwa lugha yao, kiswahili tutatumia nje tu ya darasa maana watu wataanza ohh lugha ya taifa, ohh uzalendo, english nani alikwambia ni lugha ya mwingereza au mmarekani? si waweke patent sasa mtu asitumie bila ruhusa yao? lugha ni ya binadamu full stop.

Nafikiri hilo sio tatizo, kama wakiamua kwa kiswahili mabomba tunayapata. Mbona shule ya msingi kuna mabomba tu ya biologia na kemia? Siri sio kutengeneza mabomba yako bali unatumia hilo neno la kiingereza na kulibadirisha kuwa la kiswazi. Mfano unaposema neno "Komputa" kuna mtu haelewi kwa sababu ni neno la kiingereza?

Nchi ulaya wanaofundisha kwa kiingereza ni Uingereza na Ireland tu, na Sweeden kidogo sana. Wengine wanatumia lugha zao maneno ya kisayansi mengi wameya import hivyo hivyo hivyo kutoka kiigereza na kuyaandika kwa maneno ya lugha yao. Pia unaweza fundisha kiswahili lakini ukaweka mfumo wanafunzi lazima waongee kiingereza. Mfano holland, ujerumani, sweeden nk wanafundisha kwa lugha zao lakini wanafunzi karibu wote wanaweza kuongea kiingereza.
 
Kama basi ikubalike ni Kiswahili kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, kwetu Kenya hua watoto wetu wanaanzia kingereza chekechea hadi chuoni ila ningependa Kiswahili kitumike lakini kina mapungufu mengi. Mbona asisomee mtu fani kama udaktari, uhandisi nk bila kutumia neno hata moja la kingereza. Watanzania wengi wanaanzia chekechea wakitumia Kiswahili afu shule yote ya msingi vile vile mwishowe wanageuka na kuanza kingereza wanapofikia upili. Haifai kabisa, lugha inaeleweka vizuri mtu akijifunza kama bado mdogo. ndio maana wenngi wanabaki kua na jazba na chuki unapowaongelesha kwa kimombo.
Mimi kwa maoni yangu, EAC iamue mara moja lugha ya Kiswahili iboreshwe kiasi cha kutumika hadi mafunzo ya chuoni na nina uhakika kitakubalika.
 
hapa kwetu tz kukariri ni kawaida sana sekondari hasa kwa wenzangu tuliopita kayumba school na sababu kubwa ni ugumu wa lugha
 
Sijabobea katika lugha ila you sound like umelelewa na kukulia bongo!!
Kwa kweli Kiswahili kilinitatiza sana katika shule ya upili; haswa yale maneno ya ngeli:crazy:. wanafunzi wa siku hizi wana bahati kwa kuwa hao hufundishwa ngeli kwa kufuatilia viwakilishi na sio nomino kama siku zetu. Nilikuwa kwa kawaida baadhi ya watu watano wa mwisho kwa tulipokuwa tukifanya mitihani.
 
vitabu vya kiswahili vya science kwa shule ya msingi vipo vingi tu mimi mwenyewe nimevitumia wakati nasoma shule ya msingi...hujataka tu kuvitafuta

TZ ama Kenya? Kama ni Kenya sijaviona
 
Kwa Tz shida iliyopo ni shule ya msingi kutumika kiswahili na sekondari kutumika kiingereza. Kenya endeleeni hivyo hivyo, mkitaka fundisheni kwa kiswahili kuanzia awali mpaka chuo kikuu msije mkatuiga sisi mtapotea bure.
 
Lugha ni tatizo sana, binafsi nilipokua shule ya msingi nilikuwa na uelewa mzuri kabisa, vitu nilivyosoma sijapata kuvisahahu mpaka leo. Shule ya msingi nimesoma mambo mengi sana ambayo sekondari wenda yanaenda kwa level ile ile, ila watu wanafeli tu kwa sababu ya lugha.

Mfano, shule ya msingi nimejibu maswali ya nini na wapi mwanamtapa? nimejibu dola ya mali, shona na zulu. Mfalme chaka, dola ya benin nk.
Wakati darasa la tano nimesoma nne jeografia ya Tanzania,jeografia ya Afrika darasa la tano, darasa la sita jeografia ya ulimwengu, na darasa la saba nimesoma afrika mashariki.

Sayansi nimesoma vitu vile vile wengi wakifika sekondari ama elimu ya pili uliyoiita vinawashinda. Mfano nimesoma mfumo wa umengenyaji, maumbile ya mtu wanyama mamaria, amfibia, leptilia nk.
Ama nimesoma Mchapuko = mwendokasi gawia mda yani acceleration = velocity over time. Nimesoma Uzito na tungamo yani weight and mass. Nimesoma, msongamano =tungamo gawia ujazo yani density = mass over volume.

Pia nimesoma mkondo wa umeme na tofauti za kipoteshali yani current and potential difference. Bila kusahau ile kitu ya muungano wa chembechembe ndogo sana .... yani atom.

Kwa kweli elimu ya msingi ilikuwa tamu sana na nilikuwa sihitaji kujisomea, kwa sababu mwalimu alikuwa akiongea nilikuwa na muelewa kwa ufasaha na hivyo sikuhitaji kujisomea badala yake nilipotoka skuli nilienda kupiga sembo yani mpira wa kujitengeneza wa karatasi na matambala.

Cha moto kwa kweli nilikiona ktk elimu ya sekondari, kwa sababu mwalimu alikuwa akiongea nilikuwa sielewi anaongea kwa undani nini anaongelea. Na material ya sekondari ni yaleyale tu ya shule ya msingi japo yame advance kidogo, kitu ambacho kilitakiwa kisiwe tatizo kabisa. Lakini cha maajabu kiligeuka kuwa tatizo kubwa ikabidi kuwa nalala darasani na maji kwenye karai na mbu kunikung'uta.

Mfano somo la jeografia kwa sekondari utakuta wamepiga picha wananchi wakivuna kakao ama karafuu harafu wanakuuliza unafikiri hilo ni zao gani na wanafany nini? ni swali lile lile ktk shule za msingi tulikokuwa tukiulizwa. Ama mfano sendondari watakuliza collapse of mwanamutapa empire--- kitu kile kile tulikuwa tunaulizwa darasa la tano sababu za kuanguka dola ya mwanamtapa. Kumbe tatizo linakuja kuwa na lugha.

Serikali za afrika nafikiri zinabidi zichague lugha ya kufundishia masomo yote kwa ngazi zote, na hiyo lugha lazima wahikikishe inaeleweka vyema toka chekechea ili kuweza kuwa na mabadiriko chanya ktk nyanja ya elimu. Studying by heart, hakutatunusuru kamwe.

Asante sana kwa maoni yako. Kwa kweli, sielewi ni kwanini wakuu serikalini hawawezi kuona comon-sense issues kama hizi. Tuko na kasumba mbaya sana sisi waafrika. Itakuwaje nchi kama Iceland, inatumia lugha ya Icelandic inayoongelewa na watu 300,000 kutumia lugha hiyo kuanzia chekechea hadi chuo kikuu na ilhali sisi wenye lugha inayoongelwa na watu zaidi ya milioni mia moja kukidunisha?

Upuuzi wa kukariri hapa Kenya umezidi. Jambo la kukera zaidi ni kuona mtu anafikiri ya kuwa kujua kiingereza ndio kuelimika. Niliwezachakurachakura kwenye mtandao nikapata curriculum ya California ya sayansi ndiposa nikaelewa kwanini sisi ni nchi maskini. Yale mabo ambayo wanajifunza katika darasa la pili - kama photosynthesis, sisi tunaanzia darasa la tano au nne. Yale wanayosoma katika shule ya chekechea - kama vile evaporation, sisi hatuwezi tukasoma kwasababu mtoto mdogo hawezi kushika maana ya evaporate. Lakini, ukimuuliza vizuri, utapata kuwa yuajua maana yake, ila tu lugha ndio shida.

Ni lazima tujikomboe mawazo
 
Kwa Tz shida iliyopo ni shule ya msingi kutumika kiswahili na sekondari kutumika kiingereza. Kenya endeleeni hivyo hivyo, mkitaka fundisheni kwa kiswahili kuanzia awali mpaka chuo kikuu msije mkatuiga sisi mtapotea bure.

Kwa maoni yangu, shida ya TZ ni kama tu ya Kenya (ikikuja kwa lugha ya kiingereza.) Ingawa Kenya tuko mbele kidogo, naamini shida ya hizi nchi mbili zinafanana - ufundishaji mbaya wa lugha ya kiingereza. Itawezekanaje mtu kusoma lugha kwa zaidi ya miaka minane na bado anatapatapa? Kwenye shule ya upili, tulikuwa na masomo kama Kifaransa na Kijerumani. Baada ya miaka miwili tu hivi, watu waliweza kuongea Lugha hizi kwa kiwango cha kadri. Kwanini waTZ wengi hung'ang'ana na Kiingereza baada ya kukisoma kwa mda mrefu? Siamini shida ni medium bali, kuna mtindo mbaya wa kufundisha lugha hii.
 
Fundisheni Kiswahili kama somo mpaka Chuo kikuu.
Acha watu waendelee kujifunza kwa kiingereza.
Wakati ukifika lugha imekua watajua cha kufanya.

Tafadhali nieleze...utamfundishaje mtoto kwa lugha ambayo haelewi? Mtoto amekuja shuleni na miaka sita....Kiingereza hakijui...unataka kumfundisha..utafanyaje kama tu si kumpa maneno ya kukariri?
 
Asante sana kwa maoni yako. Kwa kweli, sielewi ni kwanini wakuu serikalini hawawezi kuona comon-sense issues kama hizi. Tuko na kasumba mbaya sana sisi waafrika. Itakuwaje nchi kama Iceland, inatumia lugha ya Icelandic inayoongelewa na watu 300,000 kutumia lugha hiyo kuanzia chekechea hadi chuo kikuu na ilhali sisi wenye lugha inayoongelwa na watu zaidi ya milioni mia moja kukidunisha?

Upuuzi wa kukariri hapa Kenya umezidi. Jambo la kukera zaidi ni kuona mtu anafikiri ya kuwa kujua kiingereza ndio kuelimika. Niliwezachakurachakura kwenye mtandao nikapata curriculum ya California ya sayansi ndiposa nikaelewa kwanini sisi ni nchi maskini. Yale mabo ambayo wanajifunza katika darasa la pili - kama photosynthesis, sisi tunaanzia darasa la tano au nne. Yale wanayosoma katika shule ya chekechea - kama vile evaporation, sisi hatuwezi tukasoma kwasababu mtoto mdogo hawezi kushika maana ya evaporate. Lakini, ukimuuliza vizuri, utapata kuwa yuajua maana yake, ila tu lugha ndio shida.

Ni lazima tujikomboe mawazo

Yeah, tatizo ni lugha. Mfano hata kama Kenya wanasoma kwa kiingereza kwa level zote lakini ukweli ni kwamba lugha ya kiingereza ni tatizo kwa wakenya pia.

Mfano, sie Tanzania tunaanza kupata tatizo Sekondari japo tunakuwa na msingi mzuri wa shule ya Msingi na kupelekea kusoma kwa kukariri kwa ngazi hiyo. Pia Kenya nafikiri nako kuna tatizo kubwa kwa sababu, wenda huwa shule ya msingi kwenye msingi hawakuelewa kitu na wanaanza kuelewa kutokea darasa na sita saba na nane kitu kinachowafanya waaanze kukariri tu.
Nasema hivi kwa sababu, nimesoma na Wakenya, waganda, waDRC na wengine wengi, kiukweli wengi wana matatizo makubwa sana ktk vitu vya msingi vidogovidogo, kwa kweli unaweza wakati mwingine kushangaa kwamba huyu anajiunga na chuo kikuu hata hiki hakifahamu? Tatizo ni kubwa kwa nchi za afrika na msingi wake mie naamini ni lugha.

Tanzania tunaathirika kwa level ya pili ila wenzetu wanaathirika toka awali, na ndiyo maana inabaki kuwa elimu ya by heart.
Angalieni Somalia kwa sababu wanasoma kwa lugha yao, na matatizo lukuki waliyonayo lakini bado vyuo vyao na waelimika hawashiki mkia.
USije kushangaa ukiambiwa illiterate Kenya ni kubwa kuliko ya Somalia. Hapa, natakusema kuwa Lugha ni mhimu sana ktk elimu, na kwa vile english haikwepeki basi nikuweka misingi tu kwamba mwanafunzi lazima aongee kiingereza lakini lugha ya kufundishia lazima iwe ile wanafunzi wanayoielewa kwa undani bila kufungua kamusi,

Hii Colonial mentality inatakiwa kui-ditch na tusonge mbele.
 
6. Kwa mkenya ulio hapa,
reaction yako itakuwa ipi ukiambiwa kuwa medium of
instruction imebadilishwa hadi
Kiswahili?

Basically,I'm here as a missionary kutoka Kenya.Huwa napata opportunity ya kufundisha Pre-Form One somo la English.I started in 2009.
Katika mwaka huo,nilikuwa nawafundisha wanafunzi kwa kiasi kikubwa in English only.They were able 2 do tough exercises with ease.Hali hiyo ikaendelea kudorora upto this year when nilipofundisha strictly in English,the students failed the exercises n homework.Surprisingly,if I'd teach them the same concept but in Kiswahili they would understand n perform excellently.I had 2 switch nw 2 explain the English in Kiswahili bt with much sorrow in my heart that what's going to happen to these future leader the moment they step into Secondary Schools.Really sad.Smh!
 
Back
Top Bottom