Wakati wa CCM unakaribia

Wakati wa CCM unakaribia

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
UKAWA msidhani hatuwaoni. Tunawaona ila tunawapa nafasi ya kutamba kwa namba. Kuonesha watu kuwa mna mafuriko popote apitapo mgombea wenu Lowassa. Huu ni wakati wenu kucheza scene yenu halafu nasi CCM tuanze scenes zetu. Kalikali. Za kiushindi. Tayari muda unakaribia. Muda wetu umepiga hodi na tunainuka kuufungulia. Muda umeshafika. Subirini muone.

Malizeni kuteua wagombea wenu wa Ubunge na Udiwani halafu tuwaoneshe mchezo. Tutawashawishi wagombea wenu ili wafanye 'mambo' na wetu wapite bila KUPINGWA. Mbele ya rupia,wapo watakaojaza hovyo fomu zao ili wawekewe mapingamizi na mwishoni kuondolewa. Wapo watakaochelewa makusudi kurudisha fomu na hivyo kujifuta kwenye kugombea. Wapo watakaotengeneza wenyewe filamu za kupotea.

Muda umefika huku ukiwa unahitajika. Wakati wa kupiga na kuhesabu kura pia hatuna wasiwasi. Tutafanya 'mambo' hata bila ya kuwatumia mgambo. Kitaeleweka tu mwaka huu. CCM itashinda kwa kishindo kikubwa kwakuwa ina nia na maarifa ya kufanya hivyo kama alivyodokeza Mwenyekti wetu alipohutubia hapa Lumumba siku Dr. Magufuli alipochukua fomu ya kugombea Urais. Tumejipanga.

CCM, mbele kwa mbele!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Sasa kama muda bado mihemko ya nini? Si usubiri tu muda wa scene zenu ufike ndo uandike. Kiherehere.
 
Pia walipita mitaani wakichukuwa namba za wanachama wao, sasa namba zao zimehakikiwa tayari kwa kupiga kura, ukawa wamejiandikisha lakini kura hawatapiga, hawapo kwenye daftari.
 
hayo maarifa mbona ya siku nyingi na WAKAWA wanayajua,kwani hamjabuni mbinu nyingine?
 
Mzee VUTA-NKUVUTE kuna uzi hapa unasema Nape amekatwa katika nafasi yake ya ukatibu mwenezi!

Je ni kweli? Tafadhali mwaga vitu!!!
 
Last edited by a moderator:
Pia walipita mitaani wakichukuwa namba za wanachama wao, sasa namba zao zimehakikiwa tayari kwa kupiga kura, ukawa wamejiandikisha lakini kura hawatapiga, hawapo kwenye daftari.

Piga *152*00# ili kuhakiki taarifa za kitambulisho chako cha kupigia kura.
 
Mpwa ni kweli hilo tunalitegemea sana ila ni wachache sana watakaonunuliwa na pesa za CCM. Ni kweli wapo! Ila tutashinda tu, hakuna jinsi mwaka huu
 
Mzee VUTA-NKUVUTE, UKAWA bado hatujaanza mbona? Hizo ulizoona ni rasha rasha tu..

Kipenga kikipulizwa Majukwaa mtayaona machungu.. andaeni majibu ya ESCROW- Ilikuwaje watu wakabeba mabilioni kwenye rumbesa na viroba, Marehemu kupiga kura BMK, Najua Rasimu ya Warioba majibu hamna... lakini mtuambie pia Twiga wetu wanapandishwa ndege kwa nauli ya nani na kwa maslahi ya nani, Na nani anahusika na ukatili wa tembo wetu.. Mtuambie pia Bilioni 250 wizara inayoongozwa na mgombea wenu zimeyeyukia wapi( refer CAG report)

Lakini msisahau kutuambia Budget ya Safari ya Amiri jeshi mkuu ya mwaka mzima inaishaje ndani ya miezi miwili? Inabidi Mjiandae sana aisee... Manake majuzi mmepitisha Miswada ya Gas ana mafuta kwa hati za dharura, mtuambie ni kwa maslahi ya nani na kwa kipi.

Mjiandae vizuri aisee na mtuambie pia Kwa nini huduma za afya bado ni hoi kuliko jana pia msisahau kutuambia Dr Ulimboka Aliteswa kwa Lipi na kwa maslahi ya nani.
 
Mzee VUTA-NKUVUTE, UKAWA bado hatujaanza mbona? Hizo ulizoona ni rasha rasha tu..

Kipenga kikipulizwa Majukwaa mtayaona machungu.. andaeni majibu ya ESCROW- Ilikuwaje watu wakabeba mabilioni kwenye rumbesa na viroba, Marehemu kupiga kura BMK, Najua Rasimu ya Warioba majibu hamna... lakini mtuambie pia Twiga wetu wanapandishwa ndege kwa nauli ya nani na kwa maslahi ya nani, Na nani anahusika na ukatili wa tembo wetu.. Mtuambie pia Bilioni 250 wizara inayoongozwa na mgombea wenu zimeyeyukia wapi( refer CAG report)

Lakini msisahau kutuambia Budget ya Safari ya Amiri jeshi mkuu ya mwaka mzima inaishaje ndani ya miezi miwili? Inabidi Mjiandae sana aisee... Manake majuzi mmepitisha Miswada ya Gas ana mafuta kwa hati za dharura, mtuambie ni kwa maslahi ya nani na kwa kipi.

Mjiandae vizuri aisee na mtuambie pia Kwa nini huduma za afya bado ni hoi kuliko jana pia msisahau kutuambia Dr Ulimboka Aliteswa kwa Lipi na kwa maslahi ya nani.

Kampeni za mwaka huu:A S confused::A S confused:
 
VUTA-NKUVUTE yote uliyoyasema mwaka huu yatakuwa kwa upande wenu adui wa watanzania sio mtu ni mfumo na huwez kupambana na mfumo kama ww c sehem ya mfumo sasa wapambanaji wa mfumo ni wale wale ma engeener wenu wa mambo yote ya kimafia sasa mjiandae kwan mwaka huu CCM watakuwa wa kwanza kulalamika kuwa ukawa wamewaibia kura
 
Last edited by a moderator:
Counter attack mnayoitegemea hamtaipata.
Ukawa wamekaba kila kona.
 
Tupatupa nakushauri mtenge fedha ya kutosha kuwagharamia hao watu watakao cheza hiyo filamu ya kujitafutia mapingamizi au kujiteka na kutoweka kabla ya kurudisha fomu kwenda kuishi nje ya nchi kukwepa hasira ya RAIA.
Kama RAIA wenye hasira Kali wanaweza kumchoma moto muiba simu Nokia touch ya 40000 itakuwaje yule anayesababisha shida kwa familia zao kwa miaka mitano?
Peleka salam kwao.
 
Patrobas Katambi ameanza. Ngoma inogile!

CCM mbele kwa mbele!

Mzee Tupatupa
 
Jamani wasiwatishe magamba hawana fedha benki kuu haina fedha halaf wahindi hawaelewi kama nan atashinda so hawaifadhili ccm hata vigogo wsuolipa kodi wana wasiwasi yaan ndani ya chama kwisha hata fedha za kuhingea hamna hilo ni pigo c unajua ukitaka kushindana kesi na tajiri lazma umfilisi kwanza na wotoke ccm you made us a simple fool
 
UKAWA msidhani hatuwaoni. Tunawaona ila tunawapa nafasi ya kutamba kwa namba. Kuonesha watu kuwa mna mafuriko popote apitapo mgombea wenu Lowassa. Huu ni wakati wenu kucheza scene yenu halafu nasi CCM tuanze scenes zetu. Kalikali. Za kiushindi. Tayari muda unakaribia. Muda wetu umepiga hodi na tunainuka kuufungulia. Muda umeshafika. Subirini muone.

Malizeni kuteua wagombea wenu wa Ubunge na Udiwani halafu tuwaoneshe mchezo. Tutawashawishi wagombea wenu ili wafanye 'mambo' na wetu wapite bila KUPINGWA. Mbele ya rupia,wapo watakaojaza hovyo fomu zao ili wawekewe mapingamizi na mwishoni kuondolewa. Wapo watakaochelewa makusudi kurudisha fomu na hivyo kujifuta kwenye kugombea. Wapo watakaotengeneza wenyewe filamu za kupotea.

Muda umefika huku ukiwa unahitajika. Wakati wa kupiga na kuhesabu kura pia hatuna wasiwasi. Tutafanya 'mambo' hata bila ya kuwatumia mgambo. Kitaeleweka tu mwaka huu. CCM itashinda kwa kishindo kikubwa kwakuwa ina nia na maarifa ya kufanya hivyo kama alivyodokeza Mwenyekti wetu alipohutubia hapa Lumumba siku Dr. Magufuli alipochukua fomu ya kugombea Urais. Tumejipanga.

CCM, mbele kwa mbele!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Hapo kwenye bold.. VUTA-NKUVUTE huwa hubahatishi. Tumeshaanza kuyaona. WAGOMBEA KUTEKWA!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom