Wakati Tanzania Mtia Nia Anahimiza Rais Wa Utajiri, Dunia Ya Kwanza Wanahimiza Rais Wa Kawaida

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674

FIKRA ZA KIONGOZI WA TAIFA LANGU TANZANIA DUNIA YA TATU

Kweli wakati mwingine kuna mawazo ambayo wakati mwingine ukiyasikia na kuyapima kuwa yametoka kwa kiongozi wa juu kiwango hicho cha kuomba mamlaka ya juu ya Taifa...napata muwasho wa fikra za kujifikirisha ilikuwaje mtu wa hadhi hiyo kuwaza kuwa Taifa sasa linawaza kuwa na Rais mwenye Ukwasi bila kujali ukwasi wake umepatikanaje, kinachtakiwa ni Rais huyo apewe nafasi ya kuwatumikia umma hivyo umma huo utapata baraka ya Utajiri wa Rais huyo.Kwa mujibu wa maneno hayo kuwa anachukia umaskini...imenifikirisha sana na kunipa maswali mengi ya kujiuliza na kuwaza papo kwa papo nikiwaza hili na lile kama hivi

1:Huyu Kiongozi mwenye nia mpaka akawaza hivi...Je alimaanisha hivyo kweli?
2: Akiwa na kusudi lipi?
3: Kwa manufaa ya nani?
4: Je fikra zake hizo zina ukweli au ni uongo wa mchana kweupe kwa Wanataifa na nafsi yake?
5: Na Wananchi wanayapokea na kuyazingatia kwa dhati kama kauli thabiti na ya manufaa kwa maisha yao?
6: Je madhara ya kauli za namna hiyo kwa Taifa ni yepi?
7: Je ni haki kwa viongozi wetu kuwaza hivyo na kujalibu kutuaminisha hivyo kiuhalisia?
8: Nani anawajibu wa kuhakikisha viongozi hawatoi sumu ya maneno yasiyotimizika na hivyo kulaghai umma kwa kuwapa matarajio makubwa isivyostahiki na kufanya fikra za umma kuwazia yasiyowezekanika?
9: Nini funzo kwa Taifa na Umma kwenye kukumbatia kauli Tatanishi kama za namna hiyo?
10: Yale ambayo kiuhalisia hayatekelezeki yanapoletwa kwa umma kama matamanio na kuwaaminisha umma nini sifa yake kimaadili juu ya viongozi dhidi ya umma?Kwa kuwa umma uaminishwa kupitia Kiongozi na kiongozi anayotamka ynapokuja kuwa kinyume na UKWELI kwa kiwango kikubwa kwa Umma basi matamanio yaliyojengwa unakuwa ni UONGO na jamii kama Taifa HAIPASWI kujengwa kwa kuaminishwa UONGO kwa kuwa Kiongozi AKIWAONGOPEA UMMA ni mwanzo wa fikra zenye sura ya UONGO kustawi na kumea ...Je tunakubali Taifa kumea na kujitanabaisha kama Taifa la WAONGO?

FIKRA ZA KIONGOZI WA DUNIA YA KWANZA

Waziri Mkuu wa Uholanzi Bw. Mark Mutte akirejea nyumbani kwake toka kazini kwa kutumia usafiri wa baiskeli huku akimiminiwa saluti na walinzi wake. Hii hapa kwetu vipi

Uholanzi.jpg
 
Hawa wa kwetu landcruser tu hawataki wanataka kuweka heshima na maV8
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Hawa wa kwetu landcruser tu hawataki wanataka kuweka heshima na maV8
Simaanishi ndio tutumie baiskeli kihivyo kama wao basi tuwe na vipaumbele lakini si mambo ya starehe zilizopitiliza kesho tunaenda kuomba msaada kwa mtu ambae yeye anatupatia tukajenga hospitali wenye ufinyu wa fikra wananua mav8.Haaa hatuna hofu ya Mungu
 
Tatizo la mwafrica mtanzania tena viongozi. wanaona mwisho wa pua hizo V8 ni starehe tu na ufahari kwao kumbe kwa wenzetu huo ni ugonjwa non communicable diseases kulea vitambi na kuua uchumi wa taifa wao baiskel ni mazoezi na afya kwetu baiskel ni usafiri wa maskini na mkulima
 
Hii inaweza sababishwa na vitu kadhaa. Kuna jamii za kitanzania wao mwenye hela ndio bora haijalishi kazipataje. Kuna wengine wanaona atakayeingia ikulu atafanya hayahaya yanayofanyika sasa - hamna tofauti itakayojitokeza. Sasa afanyeje - bora aanze kula zake kabla hajaanza kufisidiwa
 
Mfumo ndio tatizo. Waziri analipwa mshahara wa zaidi ya milioni kumi kwa mwezi halafu anapewa gari la miliono 250 na dereva anayelipwa na serikali.
Mwalimu analipwa laki 2.5 kwa mwezi hapewi hata baskeli.

Kwa nini mawaziri na wakuu wa mikoa na wakuu wa idara zote wasinunue gari kwa pesa zao za mishahara. Wakishindwa wapande mabasi alimradi wafike ofisini kama wanavyofika wafanyakazi wengine wanaojitegemea.
 

FIKRA ZA KIONGOZI WA TAIFA LANGU TANZANIA DUNIA YA TATU

Kweli wakati mwingine kuna mawazo ambayo wakati mwingine ukiyasikia na kuyapima kuwa yametoka kwa kiongozi wa juu kiwango hicho cha kuomba mamlaka ya juu ya Taifa...napata muwasho wa fikra za kujifikirisha ilikuwaje mtu wa hadhi hiyo kuwaza kuwa Taifa sasa linawaza kuwa na Rais mwenye Ukwasi bila kujali ukwasi wake umepatikanaje, kinachtakiwa ni Rais huyo apewe nafasi ya kuwatumikia umma hivyo umma huo utapata baraka ya Utajiri wa Rais huyo.Kwa mujibu wa maneno hayo kuwa anachukia umaskini...imenifikirisha sana na kunipa maswali mengi ya kujiuliza na kuwaza papo kwa papo nikiwaza hili na lile kama hivi

1:Huyu Kiongozi mwenye nia mpaka akawaza hivi...Je alimaanisha hivyo kweli?
2: Akiwa na kusudi lipi?
3: Kwa manufaa ya nani?
4: Je fikra zake hizo zina ukweli au ni uongo wa mchana kweupe kwa Wanataifa na nafsi yake?
5: Na Wananchi wanayapokea na kuyazingatia kwa dhati kama kauli thabiti na ya manufaa kwa maisha yao?
6: Je madhara ya kauli za namna hiyo kwa Taifa ni yepi?
7: Je ni haki kwa viongozi wetu kuwaza hivyo na kujalibu kutuaminisha hivyo kiuhalisia?
8: Nani anawajibu wa kuhakikisha viongozi hawatoi sumu ya maneno yasiyotimizika na hivyo kulaghai umma kwa kuwapa matarajio makubwa isivyostahiki na kufanya fikra za umma kuwazia yasiyowezekanika?
9: Nini funzo kwa Taifa na Umma kwenye kukumbatia kauli Tatanishi kama za namna hiyo?
10: Yale ambayo kiuhalisia hayatekelezeki yanapoletwa kwa umma kama matamanio na kuwaaminisha umma nini sifa yake kimaadili juu ya viongozi dhidi ya umma?Kwa kuwa umma uaminishwa kupitia Kiongozi na kiongozi anayotamka ynapokuja kuwa kinyume na UKWELI kwa kiwango kikubwa kwa Umma basi matamanio yaliyojengwa unakuwa ni UONGO na jamii kama Taifa HAIPASWI kujengwa kwa kuaminishwa UONGO kwa kuwa Kiongozi AKIWAONGOPEA UMMA ni mwanzo wa fikra zenye sura ya UONGO kustawi na kumea ...Je tunakubali Taifa kumea na kujitanabaisha kama Taifa la WAONGO?

FIKRA ZA KIONGOZI WA DUNIA YA KWANZA

Waziri Mkuu wa Uholanzi Bw. Mark Mutte akirejea nyumbani kwake toka kazini kwa kutumia usafiri wa baiskeli huku akimiminiwa saluti na walinzi wake. Hii hapa kwetu vipi

View attachment 262704

Unajua kwanini kapanda baisikeli?ni rais yupi tanzania alitumia walau pikipiki,wewe unakumbatia umaskini kama sifa?tena kama sifa ya mtu kuingia ikulu?maisha bora kwa kila mtz yako wapi?msoga palikuwepo kabla jk hajaingia madarakani?riz alikuwa tajiri tangu zamani?fikra zako ni za mtu aliyejazwa upepo ktk ubongo kama tairi la gari.
 
Unajua kwanini kapanda baisikeli?ni rais yupi tanzania alitumia walau pikipiki,wewe unakumbatia umaskini kama sifa?tena kama sifa ya mtu kuingia ikulu?maisha bora kwa kila mtz yako wapi?msoga palikuwepo kabla jk hajaingia madarakani?riz alikuwa tajiri tangu zamani?fikra zako ni za mtu aliyejazwa upepo ktk ubongo kama tairi la gari.

Mawazo yako hatujayasoma bado. Either way hakunavanayepigia chapuo umasikini, ningeshauri uisome post upya.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Unajua kwanini kapanda baisikeli?ni rais yupi tanzania alitumia walau pikipiki,wewe unakumbatia umaskini kama sifa?tena kama sifa ya mtu kuingia ikulu?maisha bora kwa kila mtz yako wapi?msoga palikuwepo kabla jk hajaingia madarakani?riz alikuwa tajiri tangu zamani?fikra zako ni za mtu aliyejazwa upepo ktk ubongo kama tairi la gari.

Umekurupuka
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Sina tatizo na wanaochukia umasikini. Kuchukia umasikini bila kusema utauondoa vipi ni yale yale ya "Maisha Bora" katika Kifungashio kipya. Watanzania hatuhitaji kutolewa kwenye Umasikini, tunahitaji kuwekewa miundo mbinu sahihi, huduma sahihi za msingi zilinde afya ya mwili na akili. Tukipata hayo umasikini tutauondoa wenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Vitu vingi tunaviiga kwa wazungu - hasa hasa vya ovyo. Vya maana tunavitupilia mbali. Kuna haja gan ya kuwa na rais ambaye ni tajir Lakin hawezi simama hadharani akahadithia kinaga ubaya alivyoupata utajiri wake na jamii ikakubaliana nae? Rais wa aina hiyo ndio anakuwa role model - mfano bora katika jamii
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Vitu vingi tunaviiga kwa wazungu - hasa hasa vya ovyo. Vya maana tunavitupilia mbali. Kuna haja gan ya kuwa na rais ambaye ni tajir Lakin hawezi simama hadharani akahadithia kinaga ubaya alivyoupata utajiri wake na jamii ikakubaliana nae? Rais wa aina hiyo ndio anakuwa role model - mfano bora katika jamii

Mkuu umemaliza kila kitu. Ila kwa bahati mbaya sivyo ilvyo Tanzania.Matajiri wengi wa Bongo hata kwa mdomo wa mtutu hawawezi kusema walivyopata walivyonavyo
 
  • Thanks
Reactions: DSN
tatizo la umaskini limejenga chuki kubwa sana,mtu ukiona mwenye nazo anagombea nafasi roho inakuuma unataka maskini mwenzio,kwa style hii hamtafika,someni class position and class positioning by Karl Marx ndipo muache chuki binafsi
 
pato la mwaka south africa katika sector ya utalii pekee ni bajeti yetu sisi ya mwaka huu .wao wana artificial mbuga za wanyama sisi tuna natural resources nyingi .tanzania tuna mfumo mbovu unaoleta wasimamizi walafi na wasiowabunifu katika makusanyo na mipango kazi yenye kuleta matokeo chanya tunahitaji. tubadilishe hawa wamechoka.
 
DSN umeongea kifalsafa mno mpaka bigresult kashindwa kukuelewa ijapo kwa wenye uelewa umetusaidia sana. Waafirika nchi zetu ni tajiri sana ila tuna tatizo la asiri la kupata viongozi wasio na huruma kwa watu wao. Kwa hapa Tz tunaweza kuamua na kufata utaratibu fulani wa kiubinadamu kama tutaamua tukaanza mara hii, tayari kati ya watia nia tunao watu ambao walau wanawez kutuonesha aina ya uongozi wa kuondokana na sifa ambao unamfanya kiongozi ajitukuze na kujiona kama mfalme ama kama mkuu wa malaika Kyle peponi ...muda ni sasa wa kuamua na hatma ipo mikononi mwetu
 
Asante sana Mkuu DSN hakika uzi wako ni mzuri na una ujumbe mkubwa kwa Watanzania.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
DSN umeongea kifalsafa mno mpaka bigresult kashindwa kukuelewa ijapo kwa wenye uelewa umetusaidia sana. Waafirika nchi zetu ni tajiri sana ila tuna tatizo la asiri la kupata viongozi wasio na huruma kwa watu wao. Kwa hapa Tz tunaweza kuamua na kufata utaratibu fulani wa kiubinadamu kama tutaamua tukaanza mara hii, tayari kati ya watia nia tunao watu ambao walau wanawez kutuonesha aina ya uongozi wa kuondokana na sifa ambao unamfanya kiongozi ajitukuze na kujiona kama mfalme ama kama mkuu wa malaika Kyle peponi ...muda ni sasa wa kuamua na hatma ipo mikononi mwetu
Rweye tatizola kukumbatia wizi mpaka REALITY inatafuta uchochoro na kukaa ikisublia Mwanga uchomoze na kujitokeza hadharani.Fikra na Uchu ni wapangaji wa nyumba tofauti...fikra uzalisha mambo yenye kutaka hatima njema ..sio kila fikra njema uitwa fikra ///kitu kiiitwa fikra manake ni kitu chema,uwezi kuwa na fikra ya wizi tuseme katika uhalisia kuwa huyu ana fikra...bali tutasema huyu ni mwizi.Lakini waza mambo mema kioa aliyekuzunguka kwenye fikra hizo atasema huyu ana fikra..Na ndio maana watu waliokuwa wanafikiria toka enzi na enzi walipewa majina yya wanafalsafa kwa sababu ya kufikilia vyema.Sasa unapokutna na wapuuzi wa kupuuziwa na mawazo yao ya KIWIZi yanapotaka kufanywa na fikra basi hizo si fikra huo ni wizi.
 
Back
Top Bottom