Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Ni jambo mojawapo linaoonyesha kwamba viongozi na watu wengi nchini Tanzania wamezama katika mawazo ya mwaka 47 ya zama za ujima pale wanapokuwa na msimamo mkali dhidi ya uraia pacha kwa watanzania ambao eidha wamechukua au wana nia ya kuchukua uraia katika mataifa mengine kwa ajili ya kurahisisha uwekezaji wao, ajira au masuala mengine yenye maslahi ya maendeleo ya kiuchumi kwao, ndugu zao na taifa kwa ujumla.
Sababu kubwa inayotolewa na wengi wanaopinga uraia pacha kwa watanzania wenzao eti ni kukosa uzaledo au masuala ya usalama, wakiashiria kwamba mafisadi wengi tulionao nchini ni wazalendo zaidi ya hao Watanzania wanaoomba Tanzania iwaruhusu kuwa na uraia pacha, angalau kwa watu wenye asili ya Tanzania kwa kuzaliwa au kurithi. wengine wanapinga kwa sababu za wivu tu usio na maana, daima hawataki kuona wenzao wakiedelea au kufaidika na jambo ambalo wao sio rahisi kupata.
Na ikumbukwe kwamba suala la uraia pacha sio geni. Jirani zetu Kenya, Uganda na Burundi wanaruhusu, vile vile nchi kama Afrika Kusini, Marekani, Botswana, Misri, Japan, Sierra Leone, Germany, Ghana, India, Uingereza, Sweden, Zimbabwe, Australia, Nigeria, Singapore, Namibia, Morocco nk, pamoja na hata taifa la United Arab Emirates!
Mara nyingine hata unajiuliza, hivi suala la usalama kwa Tanzania ni kubwa kuliko nchi zinazoruhusu uraia pacha, kama zilizotajwa hapo juu? Ni tishio gani la usalama lipo dhidi ya watu wenye asili ya Tanzania ambao wangependa kuwa na uraia pacha?
Wakati Tanzania tunaendeleza mawazo mgondo ya kupinga uraia pacha, ambayo mara nyingi n yanatolewa na watu ambao huenda hawajawahi hata kuishi nje ya Tanzania, nchi kama Mauritius, Dominica, Malta, Grenada, Cyprus nk zimeenda hatua mbele zaidi katika suala la uraia pacha, kwamba sio lazima uwe umeishi nchini mwao kupata uraia, bali ukiwekeza nchini kwa kiwango cha zaidi ya dola 200,000 basi unaweza kupata uraia wa nchi hizo.
Watanzania tuondokane na mawazo mgando ya mwaka 47!
Sababu kubwa inayotolewa na wengi wanaopinga uraia pacha kwa watanzania wenzao eti ni kukosa uzaledo au masuala ya usalama, wakiashiria kwamba mafisadi wengi tulionao nchini ni wazalendo zaidi ya hao Watanzania wanaoomba Tanzania iwaruhusu kuwa na uraia pacha, angalau kwa watu wenye asili ya Tanzania kwa kuzaliwa au kurithi. wengine wanapinga kwa sababu za wivu tu usio na maana, daima hawataki kuona wenzao wakiedelea au kufaidika na jambo ambalo wao sio rahisi kupata.
Na ikumbukwe kwamba suala la uraia pacha sio geni. Jirani zetu Kenya, Uganda na Burundi wanaruhusu, vile vile nchi kama Afrika Kusini, Marekani, Botswana, Misri, Japan, Sierra Leone, Germany, Ghana, India, Uingereza, Sweden, Zimbabwe, Australia, Nigeria, Singapore, Namibia, Morocco nk, pamoja na hata taifa la United Arab Emirates!
Mara nyingine hata unajiuliza, hivi suala la usalama kwa Tanzania ni kubwa kuliko nchi zinazoruhusu uraia pacha, kama zilizotajwa hapo juu? Ni tishio gani la usalama lipo dhidi ya watu wenye asili ya Tanzania ambao wangependa kuwa na uraia pacha?
Wakati Tanzania tunaendeleza mawazo mgondo ya kupinga uraia pacha, ambayo mara nyingi n yanatolewa na watu ambao huenda hawajawahi hata kuishi nje ya Tanzania, nchi kama Mauritius, Dominica, Malta, Grenada, Cyprus nk zimeenda hatua mbele zaidi katika suala la uraia pacha, kwamba sio lazima uwe umeishi nchini mwao kupata uraia, bali ukiwekeza nchini kwa kiwango cha zaidi ya dola 200,000 basi unaweza kupata uraia wa nchi hizo.
Watanzania tuondokane na mawazo mgando ya mwaka 47!