Wakandarasi Wababaishaji Wasipewe Kazi: Waziri Bashungwa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,903
945
Waziri wa ujenzi, Innocent Bashungwa amemtaka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), kuhakikisha kuwa Wakandarasi wasumbufu na wababaishaji hawapewi kazi za ujenzi wa barabara nchini kote.

Akizungumza alipokagua Barabara ya Handeni - Mafuleta yenye kilometa 20, Bashungwa amesema ni aibu kuwa na mkandarasi msumbufu anaechelewesha kazi na bado kupewa miradi mingine hali inachelewesha maendeleo kwa wananchi.

"Mtendaji Mkuu nakuagiza kuhakikisha Mkandarasi huyu HHEG hapewi mradi mwingine wa km 30 mpaka nitakapojiridhisha na kasi yake ya ujenzi wa km 20 alizonazo sasa ifikapo Januari mwakani " amesema Bashungwa.

Amemtaka Mtendaji Mkuu wa TANROADS kujipanga vizuri na kusimamia wataalam wake ili Barabara ziweze kukamilika kwa wakati

Aidha, Bashungwa amezungumzia umuhimu wa wakandarasi kuwa na uhusiano mzuri na wananchi katika ni maeneo wanayofanyia kazi kwani kufanya hivyo ni sehemu ya ulinzi kwenye miradi wanayoitekeleza.

Amemuagiza Meneja wa TANROADS mkoa wa Tanga Eng. Eliazari Rweikiza kuhakikisha HHEG anayejenga Barabara ya Handeni-Mafuleta anaboresha barabara inayotumika kati ya Handeni na Kilindi ili kupunguza kero ya usafiri kwa wananchi.

Bashungwa amamuagiza Mtendaji Mkuu wa TANROADS kuhakikisha katika vipaumbele vyake vya barabara zitakazojengwa kwa lami iwe ni pamoja na barabara za Handeni-Mziha -Turiani( KM 108.2), Kiberashi-Songe (KM 33.5)na Songe-Gairo ili kuufungua vizuri mkoa wa Tanga hususan wilaya za Handeni na Kilindi.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Mohammed Besta amesema tayari TANROADS imeshawapanga mameneja wa miradi katika miradi yote 69 inayoendelea nchini.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Handeni mjini, Ruben Kwagirwa amepongeza Serikali kwa ujenzi kwa miradi mbalimbali ya barabara inayoendelea mkoani Tanga na kusisitiza kwamba kufunguka kwa barabara ya Mkata -Kwamsisi (Km 36), Handeni Turiani (KM 108.2), Handeni- Kiberashi- Singida, (KM434), Kiberashi- Songe ( KM 33.5) na Songe -Gairo kutaufungua vizuri mkoa wa Tanga na kuuunganisha na makao makuu ya nchi Dodoma kwa njia fupi.

Waziri Bashungwa yupo katika ziara ya kukagua athari za mvua za vuli mkoani Tanga na kukagua miradi ya ujenzi wa barabara na madaraja inayoendelea mkoani Tanga.

F_oTd2vXMAAuudP.jpg
 
Back
Top Bottom