Wajane mliwaita Dodoma kuwadhihaki? Makamba na CCM waombeni radhi rasmi!

voicer

JF-Expert Member
Jul 13, 2020
5,553
11,885
Wafuatao umewatonesha majeraha makubwa sana Mioyoni mwao.

Umewadhalilisha mbele ya Umati.
Umewafedhehesha mbele ya Umati.

Mama Anna Mkapa!
Mama Janeth Magufuli!
Mama Fatma Karume!
Mama Maria Nyerere!
Mama Gracial Machel & Mandela!

Kwamba waume zao walikufa mapema shauri ya ubaya wao?

Makamba Mzee!
Imekuwaje Uzee wako Umezeeka Busara badala ya Akili?

Kwamba mnawaalika wajane kuja kuwadhihaki kuhusu vifo vya waume zao?

Umeshindwa kujua "KIFO" sio bahati bali ni lazima!

Umeshindwa kujua "KIFO" hakina Mwenyewe wala hakina Mwenyekiti!

Umemkufuru "MUNGU"mbele ya maelfu ya Mashahidi.

Umeshindwa kujua
"DUNIA NI MAPITO"

Mzee Makamba, hata wewe iko siku yako ya kufa pia!

Na niseme tu kwamba mzee elewa haya maneno!

Kwamba Duniani hapa woote tunapita.

Haijalishi wewe ni nani!

1. Ukiwa mwoga utakufa
2. Ukiwa jasiri utakufa
3. Ukipambana utakufa
4. Ukikimbia mapambano utakufa
5. Ukiwa mgonjwa utakufa
6. Ukiwa na afya njema utakufa
7. Ukinyanyasa utakufa
8. Ukinyanyaswa utakufa
9. Ukiwa mjinga utakufa
10. Ukiwa na akili utakufa
11. Ukiandamana utakufa
12. Usipoandamana pia utakufa
13. Ukiwa na ulinzi utakufa
14. Usipokuwa na ulinzi utakufa
15. Ukiwa rais wa nchi utakufa
16. Ukiwa Huna cheo utakufa
17. Ukiwa MWEMA utakufa
18. Ukiwa mdhambi utakufa pia
19. Ukiwa unajulikana utakufa
20. Ukiwa hujulikani kama Mimi pia utakufa.

Na Mimi voicer ninaandika nikijua siku zangu zikitimia Nitakufa!

Na Wewe unaesoma kimya kimya,labda ukiogopa "kufa" usijulikane kama unasapoti huu ukweli utakufaaaa n.k

Mantiki iko Wapi?
Kufa kila mtu atakufa. Yaani mtu asikutishie "kifo" ambacho lazima kitakupata.

Mtu akutishie kwamba atakulinda usife kabisa.

Wala asikusifie kwa kutumia mifano ya kifo na wewe ukachekelea kama alivyofanya Mzee Makamba na Meza kuu ya CCM leo DODOMA.

Yaani uishi uishi na kuishi Mpaka milele.

Hapo tishika kabisa, tena tetemeka hadi jasho la kucha litoke.

kwa sababu mwisho wa siku utabaki mwenyewe Huku duniani sisi wengine tukishakufa.

Tukumbuke kwamba tutakufa. . .
Tunakufa tukiacha kumbukumbu zipi ?

" Alikuwa mwoga, Au alikuwa jasiri, Au alikuwa dikteta uchwara.

Au alikuwa MWEMA, au alikuwa katili, au alikuwa "Mshauri", au alikuwa "Mwizi", au alikuwa "Myenyekevu", au alikuwa mnafiki, au alikuwa "Mshenzi. . .

Kumbukumbu Ya kifo chako unaiandaa Wewe.

Suala umekufaje Si la msingi. Uwe umechuchumaa, au umesimama, uwe umepata ajali au umeuawa, uwe umekufa kama mateka wa kisiasa au kwa malaria.

Unaacha nini cha kujifunza ukishafukiwa kaburini?

MAkaMBA!

Tafakari juu ya fumbo la kifo, ufufuko wa wafu, maisha na uzima wa milele!

KANISA!

Nasadiki kwa Ufufuko wa mwili: Kanisa lina amini na kutumaini kwa uthabiti kabisa kama vile Kristo Yesu alivyofufuka kweli kutoka wafu na anaishi daima, vivyo hivyo wenye haki baada ya kifo chao, wataishi daima na Kristo Yesu Mfufuka, naye atawafufua siku ya mwisho. Ufufuko wa waamini ni kazi ya Fumbo la Utatu Mtakatifu. Neno mwili, linamwelezea mtu katika hali yake ya udhaifu! KIFO.

Kilio ni lugha inayozungumzwa na kueleweka na wote wakati wa ajali na kifo. Binadamu anasononeka sana na kujiuliza, kwa nini maisha yanakoma.

Namna mbalimbali za kutafuta ufumbuzi wa fumbo la kifo unajieleza katika Ngano, katika sanaa hata katika ngoma za makabila yetu. Ngano na sanaa mbalimbali zinafumba siri kuu ya uzima na tamati ya binadamu yaani kifo.

Kutokana na imani hiyo kwa Mungu na Mahoka,

○"Mbantu"
anatambua kwamba tunapokufa tunarudi nyumbani kujiunga na Muumbaji wetu pamoja na mahoka waliotutangulia. Jibu hili nalo lina udhaifu mkubwa kwa vile hatujui huko nyumbani ni wapi na kupoje.

○"Wamisri"
walijaribu kulipatia utatuzi suala la kifo kwa kuyahifadhi maiti isioze. Wakayaita Mumiani. Lengo lao kuu ni kukisimanga kifo. Kwamba hata kama kimemchukua mpendwa wao, lakini wao wanaweza bado kumhifadhi na kuendelea kukaa na mfu wao (maiti).
Kwa hiyo kifo kimekula kwake! Lakini wasijue kwa kufanya hivyo ndiyo kwanza walikuwa wanakienzi kifo kwa kukijengea makumbusho au sanamu.

○" Wasumeri"
na "Wamesopotamia"
wao walikuwa na Ngano (myths) walizosimuliana ili kujaribu kujua kinatokea nini baada ya kifo.
Wao waliamini kwamba mtu akifa na kuiacha dunia hii anaenda katika ulimwengu ambao hawezi tena kurudi duniani. Lakini hawakujua anaenda wapi na ulimwengu huo hawakujua uko wapi.

○"Wabudha"
wanaamini kuwa kifo ni mzunguko wa maisha, yaani kufa na kuzaliwa tena.
Lakini kuhusu mahali na namna ya kuzaliwa inategemea unavyoishi sasa kama vizuri au vibaya.
Fikra hizi ni sawa na Ngano za kukitania kifo. Hakuna anayeweza kuzishuhuda kwa maisha halisi.

Ngano (myth) za...
"Wagiriki" zinasimulia juu ya mtu wa ajabu aitwaye Orfeo. Huyo "Orfeo"alikuwa mwanamuziki mahili. Aliweza kupiga kinubi na kuvuta milima, mawe, miti, wanyama, ndege hata wadudu kufika kumsikiliza na kucheza muziki wake. Lakini "Orfeo" mwenyewe baadaye alikufa akashindwa kabisa kukitawala kifo.
Fasihi yake ni kwamba binadamu anaweza kutumia ufundi wake wote kuvuta na kutawala akili na kukonga vionjo vya watu na viumbe vyote vikavutika kwake.
Lakini hawezi kamwe kukitawala kifo.

Kadhalika Wanafalsafa wa Kigiriki kama vile "Sokrates" na "Aristotle"
walishindwa kulijibu swali hili, bali walijua hatima yao ni kaburi!.

○"Wayahudi"
(Israeli) walijua kwamba baada ya kufa watu wanashuka kuzimu Sheol au Shaal maana yake kuita. Sheol kuna mizimu na maisha yake hayana maana kwani huko huwezi kumsifu Mungu. Wayahudi wanamwabudu Mungu kusudi awaongoze na kuwapa furaha hapahapa ulimwenguni.

Fikra hii inatufundisha jinsi gani inatubidi kuyapatia umuhimu maisha ya ulimwengu huu. Kwa mara ya kwanza wazo la Ufufuko kwa Wayahudi linaibuka katika Kitabu cha Danieli (170 KK) walipoanza kuzungumza juu ya hatima ya mashahidi na watu wenye haki yaani walioshika Tora kiaminifu na hatima ya waovu atakapofika Masiha.
Jibu likawa kwamba wenye haki watafufuka kutoka sheol na kushiriki furaha ya ufalme wa Mungu lakini katika maisha haya haya. Waovu wataachwa wasote huko huko sheol. Ndivyo alivyofahamu Mafarisayo hata Marta alipomjibu Yesu:
"Mimi ninajua kwamba kaka yangu Lazaro atafufuka siku ya "MWISHO"

Nimalizie kwa kusema kwamba...

MAKAMBA mzee!
Umewasikitisha na kuwasononesha sana Watanzania kwa kufanya dhihaka,kwa waliokwisha tangulia mbele za haki, kwa mapenzi ya MUNGU!

Iko siku isiyo na jina kwa ila italipata siku yakikupata!

Alamsikhi.
10101.
View attachment 2440167
 
KANISA!

Nasadiki kwa Ufufuko wa mwili: Kanisa lina amini na kutumaini kwa uthabiti kabisa kama vile Kristo Yesu alivyofufuka kweli kutoka wafu na anaishi daima, vivyo hivyo wenye haki baada ya kifo chao, wataishi daima na Kristo Yesu Mfufuka, naye atawafufua siku ya mwisho. Ufufuko wa waamini ni kazi ya Fumbo la Utatu Mtakatifu. Neno mwili, linamwelezea mtu katika hali yake ya udhaifu! KIFO!
Mtazamo na Voicer leo injili inamwagika kama tuko Yerusalem😅😅
 
Mikutano ya ccm huwa ni kama sherehe au jukwaa la kufanya kufuru kwa Muumba, kupitia maneno yao na vitendo..ndiyo maana wanaalikana ili kusifiana na kujaribu kuonyesha wanazo nguvu nyingi kumshinda hata aliyewaumba..tawala nyingi zamani zilifanya kama wanavyofanya ccm sasa..lakini ni siku moja tu tena sekunde, meza (high table) huwa inapinduliwa, kibaya ni kwamba washiriki wote wa sherehe wengine hata huwa watazamaji tu huwa wanaangamia wote inabaki historia..wanao muda na nafasi kujirudi kama wanaelewa.
 
Mikutano ya ccm huwa ni kama sherehe au jukwaa la kufanya kufuru kwa Muumba, kupitia maneno yao na vitendo..ndiyo maana wanaalikana ili kusifiana na kujaribu kuonyesha wanazo nguvu nyingi kumshinda hata aliyewaumba..tawala nyingi zamani zilifanya kama wanavyofanya ccm sasa..lakini ni siku moja tu tena sekunde, meza (high table) huwa inapinduliwa, kibaya ni kwamba washiriki wote wa sherehe wengine hata huwa watazamaji tu huwa wanaangamia wote inabaki historia..wanao muda na nafasi kujirudi kama wanaelewa.
Well said,na usishangae Mungu kuwajibu muda ukitimia!
 
Heri kijana masikini mwenye hekima kuliko mfalme mzee mpumbavu ambaye hajui tena kupokea maonyo.

Mhubiri 4: 13
Katika Biblia neno mpumbavu linaonekana katika Zaburi 14:1 na katika Zaburi 53:1 linapoonekana
"mpumbavu husema moyoni mwake hakuna Mungu", katika muktadha huu neno mpumbavu linaonyesha kuwa watu wasio na maadili humkataa Mungu na kumkataa. sio watu wenye akili duni kama watu wengine wanavyotaja.
mzee Makamba amevimbewa!
 
Back
Top Bottom