Waitaliano wanavyoiibia zanzibar

Kireka1980

JF-Expert Member
Mar 18, 2008
302
43
Hii sekta ya utalii Zanzibar inaingiza pesa nyingi sana, lakini maskini wa Mungu pesa yote (60%) inaenda Italy. Ukiangalia idadi kubwa ya watalii Znz ni kutoka Italy hawa wanakodi ndege toka kwao mfano Eurofly wakifika hapa tour inayowapokea ni ya Waitaly hoteli wanayofikia ni ya Waitaly. Kwa aliyewahi kufika hoteli za Shamba Znz atakubaliana na mimi kuwa zaidi ya nusu ya hotel ni mali ya Italian.
Hatuwezi kuwa na sheria ya kudhibiti hii hali!
Sisi Watanzania tunanufaika vipi hapo?
Mimi nina hasira sana!
 
je! management za hotel ni watu kutoka wapi? wote kutoka nje ya nchi....hotel zote za shamba....mtanzania yoyote anakuwa kabuku tu na kupokea dola nyingi 200....mpaka yule wa chini dola 70.....hii ni noma kwa taifa zima.....lakini wakubwa wanakula nafikiri hasa zanzibar...
 
Pole ndugu.
Hasira ni yetu wote.
Nchi inaliwa tukishuhudia.
Viongozi wamelala.
Mwaka kesho hao hao viongozi utasikia wameshinda uchaguzi kwa kishido.
Mimi sielewi.
 
Hii sekta ya utalii Zanzibar inaingiza pesa nyingi sana, lakini maskini wa Mungu pesa yote (60%) inaenda Italy. Ukiangalia idadi kubwa ya watalii Znz ni kutoka Italy hawa wanakodi ndege toka kwao mfano Eurofly wakifika hapa tour inayowapokea ni ya Waitaly hoteli wanayofikia ni ya Waitaly. Kwa aliyewahi kufika hoteli za Shamba Znz atakubaliana na mimi kuwa zaidi ya nusu ya hotel ni mali ya Italian.
Hatuwezi kuwa na sheria ya kudhibiti hii hali!
Sisi Watanzania tunanufaika vipi hapo?
Mimi nina hasira sana!

Wataliano ni wazungu wakorofi na wenye kujua jinsi gani ya kula rushwa.Hizo hoteli zote zilizopo Zanzibar, ndani huduma watalii wanalipa gharama kama wako western countries.Lakini wananchi au wafanya kazi wanalipwa mishahara duni ya kitanzania.

Kwa macho yangu nishakunywa drink hapo Nungwi kwa gharama kama niko ndani ya Europe.

Hakuna shaka, wataliana wanakula dili na wenye mahoteli.Mara nyengine rushwa yateketeza uchumi!!
 
Mimi nilifika Karafuu Beach Hotel kule Bwejuu...wageni wote wataliano...wafanyakazi wote pale wapole na wastarabu na inasikitisha kuona wagaeni wanavyo enjoy pale ZNZ wakati locals wanaumia..kuna hoteli imejengwa pale ZNZ kulala 1 night ni USD $1500..its juts for keeping locals away....
 
Back
Top Bottom