Waislamu wa asili ya Kiarabu Tanzania wametajirika, kwanini mafanikio ya kiuchumi ya wenye asili ya Kiafrika bado yapo nyuma kuzidi hata wakristo ?

Waislamu wa asili ya Kiarabu Tanzania wametajirika, kwanini mafanikio ya kiuchumi ya wenye asili ya Kiafrika bado yapo nyuma kuzidi hata wakristo ?

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,451
Disclaimer: Chapisho hili ni kwa madhumuni ya mjadala wa kujifunza na kuelewa tofauti za maendeleo ya kiuchumi kwa jamii zetu, bila kuleta chuki, kupotosha au kushambulia.

Ni jambo lililo wazi kuwa baadhi ya Waislamu wa Kitanzania wenye asili ya Kiarabu wamepiga hatua kubwa kiuchumi—wakiwa na biashara kubwa, majengo ya kifahari, na ushawishi mkubwa kwenye sekta ya fedha.

Kwa upande mwingine, Waislamu wengi wa Kitanzania wenye asili ya Kiafrika bado wengi wao wanasalia nyuma kiuchumi.

Hali yao ya kimaendeleo inaonekana kuwa chini hata wakilinganishwa na Wakristo wanaofanana asili, mfano ukifuatilia kwa makini, jamii tano zinazoongoza katika biashara na uchumi (hata elimu) kwa Tanania Bara zina uwakilishi mkubwa wa Wakristo.

Sijawataja Wahindi anbao wengi wana dini zao, ni miongoni mwa matajiri wakubwa nchini Tanzania wanashikilia nafasi kubwa katika uchumi wa nchi lakini hatuna ukaribu nao wa kidini.
 
Disclaimer: Chapisho hili ni kwa madhumuni ya mjadala wa kujifunza na kuelewa tofauti za maendeleo ya kiuchumi kwa jamii zetu, bila kuleta chuki, kupotosha au kushambulia.

Ni jambo lililo wazi kuwa baadhi ya Waislamu wa Kitanzania wenye asili ya Kiarabu wamepiga hatua kubwa kiuchumi—wakiwa na biashara kubwa, majengo ya kifahari, na ushawishi mkubwa kwenye sekta ya fedha.

Kwa upande mwingine, Waislamu wengi wa Kitanzania wenye asili ya Kiafrika bado wengi wao wanasalia nyuma kiuchumi.

Hali yao ya kimaendeleo inaonekana kuwa chini hata wakilinganishwa na Wakristo wa asili hiyo hiyo ya Kiafrika.
Utafiti wako una mapungufu makubwa na sijui umetumia vigezo gani kutoa majumuisho yako
 
Naweza kulizungumzia kwa nadharia mbili mleta mada. Je naruhusiwa?
 
Utafiti wako una mapungufu makubwa na sijui umetumia vigezo gani kutoa majumuisho yako
Ndio ueleze wewe wapi utafiti una mapungufu na utoe hoja zako za kukosoa.

halafu usiangalie maendeleo ya mtu moja moja kusema kuna flani ana jumba la kifahari, biashara kubwa, n.k. pima kwa kigezo cha wastan.
 
Disclaimer: Chapisho hili ni kwa madhumuni ya mjadala wa kujifunza na kuelewa tofauti za maendeleo ya kiuchumi kwa jamii zetu, bila kuleta chuki, kupotosha au kushambulia.

Ni jambo lililo wazi kuwa baadhi ya Waislamu wa Kitanzania wenye asili ya Kiarabu wamepiga hatua kubwa kiuchumi—wakiwa na biashara kubwa, majengo ya kifahari, na ushawishi mkubwa kwenye sekta ya fedha.

Kwa upande mwingine, Waislamu wengi wa Kitanzania wenye asili ya Kiafrika bado wengi wao wanasalia nyuma kiuchumi.

Hali yao ya kimaendeleo inaonekana kuwa chini hata wakilinganishwa na Wakristo wanaofanana asili.
Muda na Elimu ya Mali.
Jamii za Asia zilijua biashara na ukusanyaji wa mali(accumulation of Wealth) mapema zaidi kuliko jamii za asili ya African Savanna.
 
Naweza kulizungumzia kwa nadharia mbili mleta mada. Je naruhusiwa?
Inaruhusiwa kabisa kutumia nadharia tofauti kadiri zinavyoweza kusaidia kuleta mitazamo mbalimbali katika mjadala.
 
Inaruhusiwa kabisa kutumia nadharia tofauti kadiri zinavyoweza kusaidia kuleta mitazamo mbalimbali katika mjadala.
Umetaja waarabu lakini katika nadharia zangu nataka niweke kundi la wahindi
 
Lakini ukiangalia hata katika jamii za kiafrika za hapa Tanzania kuna tofauti
Sababu ni hiyo hiyo. Mfano kwa Weusi Waislamu vs Weusi Wakristo, sababu kubwa ni madhara ya kikoloni wa mzungu. Wakristo waliendelezwa na kupendelewa kuliko Waislamu. Ikumbukwe kwamba mkoloni mkristo(European) walizikuta jamii za maeneo ya Pwani zikiwa tayari na dini na ustaarabu uliofungamabishwa na dini au sema utamaduni, mfano uvaaji, mfumo wa kuoana, nyimbo na music etc(Religion and cilivilization).
Jamii za bara zilikuwa bado wapagani kwa wingi.
 
Sababu ni hiyo hiyo. Mfano kwa Weusi Waislamu vs Weusi Wakristo, sababu kubwa ni madhara ya kikoloni wa mzungu. Wakristo waliendelezwa na kupendelewa kuliko Waislamu. Ikumbukwe kwamba mkoloni mkristo(European) walizikuta jamii za maeneo ya Pwani zikiwa tayari na dini na ustaarabu uliofungamabishwa na dini au sema utamaduni, mfano uvaaji, mfumo wa kuoana, nyimbo na music etc(Religion and cilivilization).
Jamii za bara zilikuwa bado wapagani kwa wingi.
Haikuwa rahisi kwa wakoloni wazungu hata kuanzisha shule zao maeneo ya Pwani, ambako dini ya Kiislam ilikuwa imeshajikita. Waliikataa elimu ya Magharibi (western education)kwa sababu waliiona kuwa inapingana na mafundisho ya dini. wazungu hawakuwa na budi kwenda maeneo mengine.
 
Disclaimer: Chapisho hili ni kwa madhumuni ya mjadala wa kujifunza na kuelewa tofauti za maendeleo ya kiuchumi kwa jamii zetu, bila kuleta chuki, kupotosha au kushambulia.

Ni jambo lililo wazi kuwa baadhi ya Waislamu wa Kitanzania wenye asili ya Kiarabu wamepiga hatua kubwa kiuchumi—wakiwa na biashara kubwa, majengo ya kifahari, na ushawishi mkubwa kwenye sekta ya fedha.

Kwa upande mwingine, Waislamu wengi wa Kitanzania wenye asili ya Kiafrika bado wengi wao wanasalia nyuma kiuchumi.

Hali yao ya kimaendeleo inaonekana kuwa chini hata wakilinganishwa na Wakristo wanaofanana asili.
kwa ushahidi upi?
 
Umetaja waarabu lakini katika nadharia zangu nataka niweke kundi la wahindi
Nimewataja Waislamu wa asili ya Kiarabu (wakiwemo pia baadhi ya Wahindi), kwa sababu dini ya Uislamu inajumuisha pia Watanzania waafrika wengi. Hii inaleta ukaribu wa kidini unaoweza kusaidia kufanikisha mjadala huu kwa upana zaidi.

Wahindi anbao wengi wana dini zao ni miongoni mwa matajiri wakubwa nchini Tanzania wanashikilia nafasi kubwa katika uchumi wa nchi lakini hatuna ukaribu nao wa kidini.
 
Disclaimer: Chapisho hili ni kwa madhumuni ya mjadala wa kujifunza na kuelewa tofauti za maendeleo ya kiuchumi kwa jamii zetu, bila kuleta chuki, kupotosha au kushambulia.

Ni jambo lililo wazi kuwa baadhi ya Waislamu wa Kitanzania wenye asili ya Kiarabu wamepiga hatua kubwa kiuchumi—wakiwa na biashara kubwa, majengo ya kifahari, na ushawishi mkubwa kwenye sekta ya fedha.

Kwa upande mwingine, Waislamu wengi wa Kitanzania wenye asili ya Kiafrika bado wengi wao wanasalia nyuma kiuchumi.

Hali yao ya kimaendeleo inaonekana kuwa chini hata wakilinganishwa na Wakristo wanaofanana asili.

Sijawataja Wahindi anbao wengi wana dini zao, ni miongoni mwa matajiri wakubwa nchini Tanzania wanashikilia nafasi kubwa katika uchumi wa nchi lakini hatuna ukaribu nao wa kidini.
Labda kwakuwa wakristo wanakamuliwa mno makanisani
 
Nadharia zangu ziko hivi;
  1. Jamii hizo utajiri wao , unatokana na utakatishaji fedha unaofanywa na viongozi wakuu serikalini. Mtu (kiongozi)anapora mabilioni ya pesa huko anaamua ku inject kwa mfanyabiashara (mhindi au mwarabu) maana akiwa nazo "Atamulikwa". Nadharia hii unaweza kuithibitisha hivi. Jaribu kuchunguza na kuangalia inner circles za baadhi ya watawala hapa nchini lazima kuwe na mu asia mmoja kama sio wawili.
  2. Biashara haramu(black market). Hawa jamaa Biashara zao ni za kimafia ndio maana zinafanywa kifamilia tu pekee. Hauwezi kukuta ngozi nyeusi kwenye equation ya business zao. Biashara hizi haramu ni kama vile za usafirishaji mafuta ,Biashara haramu za viungo vya watu, ukwepaji mkubwa wa kodi na kuzionga mamlaka za serikali madonge manono.... Kwa mfano kwenye Biashara haramu za viungo vya watu hufanyika sanasan kwenye private hospital zinazomilikiwa na hawa watu jamii ya Asia. Hapo kenya mbunge wa zamani wakati wa uhuru kenyatta Dr swarup Mishra ambaye ni mmiliki wa hospitali binafsi ya Mediheal akihusishwa na hii biashara ya viungo vya watu yupo kwenye radar za serikali ya Ruto akimulikwa na harakati zake.
 
Hili haliko kidini kuwa ni muislam au mkristo ila ni , jambo la taratibu katika jamii husika waarabu wana utamaduni wa kurithishana biashara na wao hupendelea biashara kuliko kuajiriwa sasa kwasababu biashara wazianza muda wanakuwa na faida zaidi , ila waafrika mambo ya kurithishana ndio kama yameanza na itachukua muda sana kuweza kufanikisha na wengi hupenda kusoma na kuajiriwa na wakipata mali huwa wanazitumia bila kuwaandalia kizazi kijacho
 
Hakuna mahusiano yoyote kati ya mafanikio ya mtu na dini yake.

Kati ya mikoa kumi yenye masikini wengi hapa tz saba yote ni ile ambayo wakristo wapo wengi.
Kati ya mikoa kumi ambayo inaongoza kwa utapiamlo na njaa hapa nchini minane yote ni ile yenye wakristo wengi.
Sasa sijui umetumia kipimo gani katika utafiti wako wa wakristo kuwa na maendeleo kuzidi waislam.

Kiufupi watz karibia wote ni masikini na wote tunabangaiza ilimradi siku ziende hakuna cha wakristo wala waislam.

Alafu hii mjadala inayo jadili mambo kwa misingi ya kidini huwa haina tija yeyote ile zaidi ya kuchochea chuki tu.
 
Back
Top Bottom