Waislamu wa Africa(Tanzania) mbona hamlaani mashambulio yatokeayo Somalia?

edwayne

JF-Expert Member
Apr 5, 2013
8,879
9,678
Mimi nina swali dogo tu, mbona sijaona waislamu wa Tanzania na Africa kwa ujumla wakilaani haya mashambulio kwa watu weusi waislamu wenzao huko Somalia ila hupaza shingo na sauti kuhusu yanayotokea Palestina na Burma. Mbona waislamu wa africa ni wanafiki sana mnasikitisha sana. Humu sijaona uzi kuhusu huzuni za Somalia ila za Palestina na wale wa Burma.
 
Huna lolote ndo maana hujui unacho kiongea, unataka waisilam wapaze sauti ili nani asikie?" waisilamu hatunazo makelele maana sii wendawazim wakupayuka hovyo, Zaidi yakuongea na mwenyezi mungu subhana uwata allah
Unaona aibu wewe lini ulilalamika kuhusu Sudan au somalia ila yakitokea mambo nje ya Africa unalalamika kama wale ndugu zako penda waafrika wenzako
 
tunalaani vitendo vya kigaidi (ukhawarij) tunaliongea hilo kila siku au ulitaka mpaka tuweke press conference ...uislam ni dini yenye kumvuta aliye nje aingie ndani na kumfanya aliye ndani asitoke
Lini ulilaani vitendo hivyo kuhusu somalia wewe
 
Lini ulilaani vitendo hivyo kuhusu somalia wewe
Mtume (Saw) amesema pindi jambo baya linapofanywa, fanya yafuatayo kulirekebisha: lipiganie kwa nguvu, au likemee kwa sauti, au lichukie kutoka moyoni. Yeyote atakayetumia moja ya njia hizo yupo sahihi. Kwa hiyo lazima usikie sauti za kulaani kila tukio
 
nadhani utakua unatumia jamii forums tu, au kama unatumia na mitandao mingine ya kijamii bas utakua una kusudio lako unalolitafuta......
 
Husipende kuamini kitu husichokijua juu ya imani ya watu wengine ili kuepuka kuwa mjuvi wa mambo ikikupendeza jifunze /uliza/tafiti ili uwe mjuzi
 
nadhani utakua unatumia jamii forums tu, au kama unatumia na mitandao mingine ya kijamii bas utakua una kusudio lako unalolitafuta......
Natumia mitandao yote ya kijamii hakuna mnapokemea jambo la Somalia huo ni unafiki mkubwa wa waislamu wa Africa especially Tanzania humu JF mpaka uzi wa kuhusu Burma mlianzisha kulalamika ila waafrika wenzenu wakiuliwa mnajifanya hamuoni... acheni kujipendekeza kwa wengine wapendeni waafrika wenzenu kwanza
 
Michango inachangwa duniani na pole nyingi zimetoka mbona
Mengi huwa yanaenda kimya kimya
Account sio lazima iwe insta
Nazungumzia wa Africa... mwafrika amchangie mwenzake Hilo jambo ni lakusadikika kwakweli
 
Dini za watu hizo mkuu, sisi wa Africa yetu matambiko hahhaha u kristo na u wislam mhhh !
 
Kwani Somalia wanakaa wa Islam peke Yao. Au wanaokufa ni wa Islam peke Yao? Hakuna wakristo Somalia?
 
Unaona aibu wewe lini ulilalamika kuhusu Sudan au somalia ila yakitokea mambo nje ya Africa unalalamika kama wale ndugu zako penda waafrika wenzako
Waislamu wote ni ndugu na kulaani sio mpaka watu waone ulivyolaani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…