Wahitimu wa Vyuo wanahitaji Msaada

Wahitimu wa Vyuo wanahitaji Msaada

Joined
Feb 4, 2023
Posts
39
Reaction score
75
Habarini wa JF,

Wazazi na ndugu wa karibu huenda walijitahidi kwa hali na mali na kujibangaiza kwa kidogo walichopata ili watoto wasome, na kweli watoto hawa walijitahidi kusoma kwa bidii mpaka kufikia ngazi za juu za elimu. ambapo kwa nchi yetu level yenye wasomi wengi zaidi ni Degree/bachelor.

kadri miaka inavyozidi kwenda ndio idadi ya wahitimu inaongezeka na graph ya wahitimu wa vyuo inapanda., mbaya zaidi watoto hawa wanahitimu huku wengi wao wakiwa hawajui waelekee wapi. na ukizingatia karibu 80% ya watoto hawa wametoka kaya masikini kiasi kwamba familia zao zinawatazama kwamba sasa huenda wakazikomboa familia zao.

Uwezekano wa kupata ajira ni mdogo, uwezekano wa kuweza kukidhi mahitaji yao wenyewe tu unaweza kuwa ni changamoto. nani awasaidie watoto hawa?.

Watoto hawa wanahitaji msaada wa kisaikolojia ili watulize akili wanapoingia mtaani, pia watoto hawa wanahitaji connections za michongo ili wajikwamue kiuchumi.

Wengi wao wamejawa na stress juu ya hatua gani wachukue kwa sasa wakiwa wanaelekea kumaliza mitihani yao ya mwisho. wengi wanajiuliza je warudi nyumbani kwao mikoani au wabaki kwenye miji ambayo wamesoma chuo waanze mihangaiko hapo?, wapo dilemma.

Na sio kweli kwamba watoto hawa hawataki kazi ngumu au biashara ndogondogo kisa wana elimu kubwa, la hasha.

Binafsi pia namaliza chuo kikuu mwaka huu,. degree ya mechanical engineering. nilianzisha kibiashara ambacho kimekuwa msaada mkubwa kwenye kunipatia mahitaji na hata uhakika wa kula na kulala. lakini biashara hii siyo mwisho wa malengo yangu, nahitaji fursa ya kunyanyuka na kuanza maisha mapya yenye muelekeo ulio thabiti.

Kiukweli wengi wa wahitimu huwa kazi walizozisomea hawazijui, na mimi nikiwemo, ili niwe engineer kamili ninahitaji muda wa kujifunza kwa kupitia internship na wengi mnajua hili. kama kuna nafasi ya internship sehemu basi nitashukuru sana nikipata.

Pia, sio lazima internship au kazi niliyosomea, hata kama kuna wazo ambalo sokoni linalipa kwa sasa naomba utuandikie hapa ili wengi tufaidike,. pia ushauri nao sio mbaya.

Mbarikiwe na iwe jumapili njema kwenu.
 
Tz inaraia waajabu sana, design kama tumerogwa hatujitambui.Imagine wahitimu wote wa Vyuo wasio na ajira wangeunga mkonoo Chadema au kuunda chama Chao kuiing'oa ccm 2025,yaani kama Aisha Hana ajira ukoo wake wote wamuunge mkono chama hicho.Mbona kiingeeleweka tu💪💪
 
Tz inaraia waajabu sana, design kama tumerogwa hatujitambui.Imagine wahitimu wote wa Vyuo wasio na ajira wangeunga mkonoo Chadema au kuunda chama Chao kuiing'oa ccm 2025,yaani kama Aisha Hana ajira ukoo wake wote wamuunge mkono chama hicho.Mbona kiingeeleweka tu💪💪
Changamoto iliyopo ni kuwa wazazi haohao wapo bize kuiunga mkono ccm, ninashangaa sana. ingawa hii ni tofauti kwa wazazi wangu
 
Tz inaraia waajabu sana, design kama tumerogwa hatujitambui.Imagine wahitimu wote wa Vyuo wasio na ajira wangeunga mkonoo Chadema au kuunda chama Chao kuiing'oa ccm 2025,yaani kama Aisha Hana ajira ukoo wake wote wamuunge mkono chama hicho.Mbona kiingeeleweka tu💪💪
🤣🤣 CCM unausika vipi na ajira
 
Maliza kwanza chuo ndo akili itakukaa sawa si ulipata boom ukaishia kushona vikaunda suti na kubadilisha simu kila toleo jipya likitoka. Mikopo mnayopata kupitia HESLB au hela za matumizi ni mitaji tosha ya kuingia mtaani kwa ajira binafsi ukisoma upepo wa maisha halisi
 
sasa ikiwa wahitumu wa vyuo wanahitaji msaada walioshia la saba? acheni kudekadeka nyie vijana
 
Maliza kwanza chuo ndo akili itakukaa sawa si ulipata boom ukaishia kushona vikaunda suti na kubadilisha simu kila toleo jipya likitoka. Mikopo mnayopata kupitia HESLB au hela za matumizi ni mitaji tosha ya kuingia mtaani kwa ajira binafsi ukisoma upepo wa maisha halisi
Umesoma vizuri nilichokiandika kuhusu mimi mwenyewe?
 
Ni kweli kabisa. Ila pia kati 10 kama 9 hawaajiriki kwenye sekta binafsi. Nilipambana ili angalau niajiri 10 nisaidie kuongeza ajira, nikaanzisha ka chimbo, nikaajiri 10 wakanifilisi kwa wizi na uzembe. Nikafunga, wote wakarudi mtaani kuendelea na zoezi la kutafuta kazi.
 
Ni kweli kabisa. Ila pia kati 10 kama 9 hawaajiriki kwenye sekta binafsi. Nilipambana ili angalau niajiri 10 nisaidie kuongeza ajira, nikaanzisha ka chimbo, nikaajiri 10 wakanifilisi kwa wizi na uzembe. Nikafunga, wote wakarudi mtaani kuendelea na zoezi la kutafuta kazi.
Wasomi wana malengo makubwa sana , wanapenda wizi sana na njia za mkato .
 
Usijipe tabu kuhusu future yako , maliza mitihani kama ni fungu lako utapata ...Rudini makwenu msije mkawa omba omba kwenye mikoa ya watu .
 
Ni kweli kabisa. Ila pia kati 10 kama 9 hawaajiriki kwenye sekta binafsi. Nilipambana ili angalau niajiri 10 nisaidie kuongeza ajira, nikaanzisha ka chimbo, nikaajiri 10 wakanifilisi kwa wizi na uzembe. Nikafunga, wote wakarudi mtaani kuendelea na zoezi la kutafuta kazi.
Hii ilikuwa mbaya, pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom