Kiroroma
JF-Expert Member
- Feb 6, 2009
- 370
- 114
Jamani naumia, naumia, naumia hata sijui nimlilie nani katika hili jambo nililoliona mchana wa leo !
Nilikuwa maeneo ya Kipawa karibu na Sido Mkoa nikashuhudia magari makubwa ya mizigo kibao yakitoka ndani ya godown zilizoko katika eneo hili ,Nikabainishwa kuwa hayo magari yamepakia marobota kede kede ya mitumba iliyoshushwa tangu Ijumaa kutoka kwenye kontena zipatazo hamsini za futi 40 zilizotarajiwa kupeleka nchi jirani za Rwanda, Burundi,Zambia na Congo.Kumbe ulikuwa ni mzigo wa transit sasa unauzwa locally!!Ni kiasi gani cha mabilioni ya Ushuru yamekwepwa katika hali hii?.Na nilipodadisi zaidi nikaambiwa maafisa wa TRA wakija huwa magari yanafungiwa ndani ya godown na watu kukitoa.Na huu ndo mchezo wa mahali hapa miaka nenda rudi.Tunalalamika miundo mbinu yetu mibovu hatuna hospitali za kutosha ,shule hazina vifaa nk nk.Lakini kumbe sisi wenyewe tunawasaidia wahindi kukwepa ushuru ambao ni mapato ya serikali ya kuweza kufanya yote hayo.Wadau nisaidieni kuwajulisha wahusika walau wawakamate tu tunusuru hayo mapato yanayopotea.
Nilikuwa maeneo ya Kipawa karibu na Sido Mkoa nikashuhudia magari makubwa ya mizigo kibao yakitoka ndani ya godown zilizoko katika eneo hili ,Nikabainishwa kuwa hayo magari yamepakia marobota kede kede ya mitumba iliyoshushwa tangu Ijumaa kutoka kwenye kontena zipatazo hamsini za futi 40 zilizotarajiwa kupeleka nchi jirani za Rwanda, Burundi,Zambia na Congo.Kumbe ulikuwa ni mzigo wa transit sasa unauzwa locally!!Ni kiasi gani cha mabilioni ya Ushuru yamekwepwa katika hali hii?.Na nilipodadisi zaidi nikaambiwa maafisa wa TRA wakija huwa magari yanafungiwa ndani ya godown na watu kukitoa.Na huu ndo mchezo wa mahali hapa miaka nenda rudi.Tunalalamika miundo mbinu yetu mibovu hatuna hospitali za kutosha ,shule hazina vifaa nk nk.Lakini kumbe sisi wenyewe tunawasaidia wahindi kukwepa ushuru ambao ni mapato ya serikali ya kuweza kufanya yote hayo.Wadau nisaidieni kuwajulisha wahusika walau wawakamate tu tunusuru hayo mapato yanayopotea.