Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,608
Kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi nchini Uganda, kuna zaidi ya wapiga kura milioni 21 waliojisajiliwa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Januari 15, 2026. Wapiga kura wataamua ni nani watamchagua kati ya wagombea 8 wanaowania nafasi ya urais kutoka vyama mbalimbali nchini humo. Yoweri Kaguta Museveni kutoka chama cha NRM ambae ndie Rais wa sasa anatetea nafasi yake kwa mara ya saba.