Wagombea ndani ya CCM ni patashika

Wagombea ndani ya CCM ni patashika

Wasirra aliwahi kuiba kura za ubunge huko nyuma na kupewa adhabu ya kutogombea kwa kipindi fulani. Kwa hivyo anazo chembechembe za wizi kama walivyo wanaukoo wote wa ukoo wa panya.
Pia juzi tumebaini anataka kubinafisisha nyumba ya bodi ya sukari. Amejipigia debe ili arejeshwe kuwa waziri wa Kilimo na chakaula ili aweze kukamilisha mchakato huo kwa urahisi. Tunamwangalia kwa karibu. Hiyo nyumba ataisikia kwenye ndoto. Ni nyumba ya umma. Huyu ni kama wanaukoo wenzake - ukoo wa panya.
 
Hapo mwenye sifa za usafi na uadilifu mbele ya WanaCCM na Taifa ni Steven Wassira,huyu ndio mwenye uwezo wa kujenga hoja na kuukabili upinzani.
Hawa wengine waliobaki wooote ufisadi na ubadhilifu ndio vimewatawala...Staven Wassira mweupe dhidi ya kashfa

ila kakaa bure kwene nyumba watu bila kulipa kodi ya pango
 
Makundi ya kugombea uraisi yaiuwa ccm
 
KWA BARUA HII KWA MWIGULU,UPEPO WA URAIS NDANI YA CCM UMEBADILIKA

Siku kadhaa zilizopita tumeshuhudia Naibu Katibu Mkuu Mwigulu Nchemba akilimwa barua ya kumuamuru kusitisha "harakati" zake za kuzunguka mikoani kwa kofia ya unaibu Waziri na Unaibu Katibu Mkuu kujijenga kwa ajili ya mbio za Urais 2015.

Harakati zake zilihusisha matumizi ya chopa isiyokuwa na baraka za chama,mikutano yake iliibua hisia hasi na hali ya kutotambuliwa kwa viongozi wa kamati za siasa za mkoa,wilaya,kata na hata vijiji,kiufupi Mwigulu alivamia mikoa,Wilaya,Kata na Vijiji bila ruhusa maalumu toka kwa viongozi wa maeneo husika.Hali hii ilijenga mauzi na hasira kwa viongozi wengi wa kamati za siasa na kulifikisha swala hili kwa Kamaradi Kinana,ambaye bila woga alimuonya kwa maneno Mwigulu Nchemba,hata baada ya kukaidi na kuendelea na safari zake alipokea barua kali iliyoamuru asitishe hizo kampeni zake za urais kabla ya wakati.

Kwa sasa Mwigulu si sehemu ya watarajiwa wa ugombea urais ndani ya chama,harakati zake zimetulizwa kwa utovu wake wa nidhamu wa kutokumsikiliza katibu Mkuu ambaye ndiye Mtendaji Mkuu na boss wake ndani ya chama,utovu huu wa nidhamu wa Mwigulu kwa katibu Mkuu wake ni kigezo tosha cha kumuweka pembeni wakati ukifika.Huyu tunamwondoa kwa sasa katika list.


Lazaro Nyalandu,huyu ni "checkbob" tu,anayejitangaza kugombea urais ili nyota yake ya kisiasa isififie,hana uzito wowote na hata kauli yake ya kuutaka urais haikupewa uzito.Huyu anaamini Wamarekani wake alioishi nao ndio watampa urais.


Makamba Jnr hoja yake ilikuwa moja tu,ujana au umri,amepima upepo akakuta hoja hiyo haina mashiko,akaamua kuja kivingine..akajichimbia akaja na kitabu.analazimisha tukisome kwa kununua kurasa za magazeti na kukichapisha kama "Toleo Maalumu",kwa hali ndani ya chama kwa sasa,na upepo wa siasa za kitaifa,Makamba Jnr sio "candidate" mujarabu,labda ajijenge kwa msimu mwingine.


Hali iko hivyo kwa Bernard Membe,kada asiye na ushawishi ndani ya chama,sehemu ya watu wake wamekimbilia kambi ya "Team Sukari,Team asali"...Membe anatajwa kuwa mjivuni na nwenye maringo,anayeamini ameshakuwa rais hata kabla ya kuteuliwa na chama..kambi yake imevurugika na kutawanyika.Inaitaji mujiza kwa Membe kukubalika ndani ya chama,maana kwa CCM hachaguliwi Rais tu,bali mwenyekiti wa chama pia.Hulka ya Membe na ushawishi wake haumpi nafasi ya kupeperusha bendera hiyo,huyu anapewa lkn nafasi ya kuleta upinzani kwa Magwiji wa Chama kama Steven Wassira,Mizengo Pinda na Edward Lowassa.Tuisubiri May itatupa majibu


Edward Lowassa,huyu anatajwa kama kampeni zake zimelalia kwenye pesa,anamwaga pesa kama njugu,Kitengo cha Usalama ndani ya chama kinaendelea kukusanya ushahidi ndani ya harakati na kambi yake,ili wakati ukifika ziwekwe wazi na wanachama waamue,huyu anautaka urais kwa namna zote,ana kambi iliyotawanyika lkn unayofanya kazi kwa msukumo wa pesa na si mapenzi ya dhati kwa mgombea wao,hali yake ya afya pia imekuwa kikwazo,Wengi wa wanakambi wake wanapata wasiwasi juu ya afya yake,ukipata nafasi ya kuwa naye karibu wanakiri kuwa afya yake haiwezi mitikisiko.Siri zao zinavuja kwa sababu walioko huko wengi ni maslahi ya pesa,kambi yake inatumia nguvu kumsafisha na kashfa ya ufisadi.Upinzani wako kimyaa kwa Lowasa sabb wanaamini CCM ikimpitisha kwao itakuwa njia rahisi kuibomoa CCM kwa rekodi ya Lowassa huko nyuma.


Mizengo Pinda ...huyu kaibuka ghafla kama moto wa kifuu,hakuwa na ndoto hizo mpaka aliposhawishiwa na wapambe.Anahitaji nguvu Sana kueleweka kuwa Rais na Mwenyekiti wa CCM,hana ushawishi Mkubwa ndani ya chama,mpole,regerege na asiye mkali hata kwa walio chini yake,katika swala la Escrow hakusiikika kutoa kauli ya kiuongozi na kurudisha imani ya serikali na chama,kauli ya kukemea aliyoitoa Wasira bungeni wakati wa mjadala wa Escrow ilipaswa kutolewa na PM,walau Prof Mwandosya naye alionyesha uhai.CCM na wanachama wake hawatakuwa tayari kuongozwa na Mwenyekiti aina ya Pinda,huyu naye tumpe mda anaweza kutoa upinzani kwa Wassira na Lowassa.


Steven Masatu Wassira,huyu anatajwa na wanaCCM wengi kutaka kugombea urais,anaaminika ktk ujenzi wa hoja,kusimamia ukweli na kile anachokiamini,Alipita kwa kishindo mwaka 2012 katika uchaguzi ndani ya chama.Wanachama wengi wanamsifu kwa kujitoa muhanga ktk midahalo iliyowatisha wengi ndani ya CCM,alihudhuria na kubadili kabisa upepo.Anatajwa kuwa muadilifu asiye na kashfa za ufisadi na ubadhilifu wa Mali za umma.Kauli yake ndani ya Bunge juu ya sakata la Escrow ilifungua ukurasa Mpya kuwa ndani ya CCM kuna watu kama Wassira na Mwandosya wanaotaka wezi hao wawajibishwe,Katika harakati hizi za mabadiliko ya siasa ndani ya nchi,CCM wanaamini kuwa na mtu mwenye uwezo wa kujenga hoja,muadilifu na mwenye maono ya kiuongozi.Wapinzani wake wanatumia turufu ya yeye kuhama chama 1995 baada ya kufanyiwa zengwe ndani ya CCM,Sokomoko la nyumba ya bodi ya sukari iliyoanzishwa na wapinzani wake imeyeyuka,maana amerudishwa tena Wizara ya Kilimo na Chakula ambayo bodi ya sukari i chini yake.Huyu anapewa nafasi kubwa sanaa kutoana jasho na Lowassa,Membe na Mizengo Pinda,kinachowapa ugumu wapinzani wake ni kutokujuwa kambi yake imekaaje.

May hiyo ndio inakuja...Historia iandikwe...Kwa sasa CCM inahitaji mtu muadilifu,mwenye maono na mchapakazi.

Wasira hafiki kokote Kwani Kambi yake Ni wasanii watupu Na wana njaa hakuna mfano wakipewa pesa wanakula wenyewe huku Wasira Mwenyewe ni Kikongwe kama Mwai kibaki na Mugabe wa Zimbabwe, na Membe anasubiliwa kufikishwa Mahakama ya kimataifa juu ya wizi wa Pesa za Gadafi na Kifo cha utata Cha baloz wa libya , akina Jauary , mwigulu , mwandosya hao ni wasindikizaji tu Fainal lazima itakuwa Pinda vs Lowasa.
 
Uchambuzi umekaa vizuri but naomba ccm wamkate lowasa jina ili ukawa wapate njia laisi ya kufika ikulu kwani kutatokea mpasuko mkubwa sana pindi jina la lowasa litakapokatwa. Kumbuka lowasa amewekeza pesa njingi katika kufanikisha hadhima yake ya kufika ikulu. So wakimkata itakuwa neema kwa ukawa kwani ccm itakatika vipande vipande.

Wakimweka Membe kisha wakamshindanisha na kivuli lazima kivuli kitaibuka kidedea , Wasira, January , Mwigulu , mwandosya ni wasindikizaji tu, Hata wakagawa Mapesa watu watasunda na kujikausha , Ni pinda au Lowasa wanaweza kuwasumbua Ukawa , wengine wasubiri mwaka 2020 huko.
 
Just imagine kama wassira sasa ndiye raisi wa nchi hii halafu yuko UN anahutubia??

Mimi mwenyewe najiuliza hapa siujui zile picha za kwenye mabango ya kampeini yake yatakavyokuwa kituko mitaani. Watoto watakuwa wakikimbia wakiyaona kwakweli.
 
team wassira on duty... Mnamtetea kuwa hana historia ya ubadhirifu, lakini mnasahau kuwa pia hana historia ya utendaji kwa zaidi ya miaka 20 aliyohudumu kama waziri na mtendaji wa serikali.
Wanaccm hawatachagua tu mtu kwa kuwa hajawahi kuiba, bali kwa kuwa ana historia ya kuleta mabadiliko chanya kule alikohudumu.

Wassira hafai hata kuingia katika 20 bora za potential candidates wa ccm...

By the way, asipoteuliwa kugombea huu uraisi nadhani kama kawaida yake atahama chama akagombee na act nadhani..m

kweli mkuu hii ni team wasira at work hata mm nimeona. Yan mtu akijenga hoja zake utaona tu anavyoenda hadi mwisho utagundua nia yake thabiti nini.
 
Mimi mwenyewe najiuliza hapa siujui zile picha za kwenye mabango ya kampeini yake yatakavyokuwa kituko mitaani. Watoto watakuwa wakikimbia wakiyaona kwakweli.

Hujafa hujaumbika....Usitukane wakunga na uzazi ungalipo!!Hakuna Mwandamu aliyejiumba...Tafakari kauli zako.Hata kama humpendi,usitumie maumbile yake kumdhuhaki
 
Wasira licha ya kuwa ccm, mi ninamkubali ni mwanasiasa asiye teteleka pia ni mwanasiasa anayeweza kujenga hoja na ndiye msafi kwani wale wanasiasa mafisadi huwa hawapendi kuonekana mbele ya macho ya kuoga kuumbuliwa wasira amekuwa mpiganaji nyuma ya wananchi hivyo namuombea mambo yake yaende sawa ili aingoze tanzania
 
Wotemagarasa hakuna mwenye unafuu kweli CCM ya sasa imeishiwa huyu Wasira mpanga njama za kuuwa watu wapinzani akishirikiana na Mwigulu atatawala wapi

Alipanga njama gani mkuu mbona mi huwa namwonaga ni MZEE ambae Hana shida
 
Wakimweka Membe kisha wakamshindanisha na kivuli lazima kivuli kitaibuka kidedea , Wasira, January , Mwigulu , mwandosya ni wasindikizaji tu, Hata wakagawa Mapesa watu watasunda na kujikausha , Ni pinda au Lowasa wanaweza kuwasumbua Ukawa , wengine wasubiri mwaka 2020 huko.

Pinda yupi huyu Huyu lege lege au yupi?
Pinda Huyu anaewategemea akina bulembo au yupi
Bora WASIRA au Lowassa lakini sio huyo mfuga nyuki
 
Wasirra aliwahi kuiba kura za ubunge huko nyuma na kupewa adhabu ya kutogombea kwa kipindi fulani. Kwa hivyo anazo chembechembe za wizi kama walivyo wanaukoo wote wa ukoo wa panya.
Pia juzi tumebaini anataka kubinafisisha nyumba ya bodi ya sukari. Amejipigia debe ili arejeshwe kuwa waziri wa Kilimo na chakaula ili aweze kukamilisha mchakato huo kwa urahisi. Tunamwangalia kwa karibu. Hiyo nyumba ataisikia kwenye ndoto. Ni nyumba ya umma. Huyu ni kama wanaukoo wenzake - ukoo wa panya.

Unachembechembe za kike OVER
 
CCM haina mgombea anayefaa. Huu siyo uchaguzi kama wa 2005 ambapo mgombea alichaguliwa bila vigezo. Unafahamu kucheka na watu, unahudhuria misiba na kula nyama choma kwenye magenge na wananchi wa kawaida, tayari unafaa kuwa Rais.

Kwanza wananchi wote, hata tusiokuwa viongozi wa umma tunatakiwa kuwa waadilifu kwa maana ya kutokuwa na kashfa zinazokufanya uonekane ni mhalifu. Kutokuwa mwizi na kutokuwa na kashfa siyo sifa za kuwa Rais, hizo ni sifa za kuwa raia mwema.

Anayeutaka Urais, inabidi awaambie Watanzania amefanya nini cha pekee kila mahali alipokuwa tofauti na raia wengine wote, kiasi cha yeye kuona anafaa kuwa kiongozi mkuu, kuwazidi wengine wote. Kwangu mimi kwa hao uliowataja sijaona chochote:

1) January Makamba - Ni Naibu Waziri; amefanya nini cha pekee kwa nafasi aliyo nayo?

2) Bernard Membe - Business as usual; ana nini cha pekee?

3) Pinda - He is a below average performer, nafasi aliyo nayo ni kubwa mno ukilinganisha na uwezo wake

4) Nyalandu - Not worth for discussion; poor performer

5) Sumaye - Anaweza kubebwa na utendaji kazi wa Mkapa

6) Wasira - Hata jina lake likitajwa halileti ujumbe wowote wa kuelezea kitu anachosimamia

7) Lowasa - Sipendi Lowasa awe Rais but he was a leader. Jina lake likitajwa linaleta ujumbe/hisia katika moyo wako. Alisimamia sana masuala ya elimu, na pia ana ujasiri wa kutamka na kusimamia anachokiamini

Kiongozi mzuri anatoka nje ya CCM

1) Dr. Wilbroad Slaa - Likitajwa tu jina lake ujumbe unaoupata ni mtu jasiri, asiyeogopa chochote, mtu mwenye kujitofautisha kiutendaji kila mahali alipowahi kupewa nafasi. Alipokuwa kasisi wa Kanisa Katoliki, alionekana mapema na maaskofu kumwamini kuwa mtendaji mkuu wa Baraza la maaskofu. Waliokuwa ndani ya Kanisa wanajua mambo makubwa ya maendeleo aliyoyaleta ndani ya Kanisa. Hiyo ni sababu mojawapo, pamoja na Dr Slaa kuuacha upadre, hutamsikia padre yeyote au askofu akatamka lolote lenye kudharau mchango wa Dr. Slaa katika Kanisa.

Alipouacha upadre, hakwenda kukaa tu, kama raia wa kawaida alifanya kazi kubwa kwa kushirikiana na wananchi wa karatu katika miradi ya maji ili kuondosha tatizo la maji, ambalo lilikuwa ni tatizo kubwa kwa wilaya ya karatu. Wananchi wakamtaka awe mbunge wao.

Alipoingia bungeni na kupata platform ya kuongelea, ndiye aliyeisema wazi bila woga kashfa ya EPA, na kuwataja viongozi mafisadi. Akiwa M/Kiti wa kamati ya Bunge ya Serikali za mitaa, ni chini ya Dr. Slaa utaratibu wa ukaguzi wa matumizi ya pesa ulibadilika kutoka ukaaji mzuri wa mahesbu ya kihasibu mpaka 'value for money'.

Alipopewa na nafasi ya kugombea nafasi ya Urais alileta changamoto kubwa kwa wagombea wa CCM kiasi cha kufanya idadi ya wabunge wa CDM iongezeke maradufu na kuifanya CDM kuwa chama pinzani kiongozi Bungeni na nje ya Bunge.

Vigezo na mambo aliyoyafanya Dr Slaa ndiyo ishara ya kiongozi bora. Kiongozi bora na makini ana sifa moja kubwa, mahali popote utakapomweka, yeye ataonekana tofauti na wenzake. Hata ukimwambia afanye kazi ya ufagizi, eneo lake litakuwa safi kuliko ya wenzake.

Magufuli
Katika CCM angalao Magufuli ana sifa za kiuongozi. Kwenye ujenzi wa barabara, alipokuwa Shukuru Kawambwa (an example of poorest performers), km 1 ya barabara iligharimu TZS 1.2 billion na miradi ilisinzia sana. Magufuli alipoingia km 1 ikawa TZS 800 milioni na kazi zilienda kasi zaidi. Magufuli alipoenda samaki, wavuvi waliokuwa wakifanya uvuvi haramu walichemka kwelikweli.

Wanachama wa CCM waitazame Tanzania kwa jicho la utaifa, uzalendo na huruma. Wagombea wote waliojitokeza, hakuna mwenye kuleta kitu cha pekee. Wote, bila ya kuvutwa na hisia za kiitikadi tumchague Dr Slaa, mtu mwenye historia ya kuleta mabadiliko kila alipoenda, aibadilishe Tanzania na atuwekee msingi wa Taifa jipya kama alivyofanya George Washington kule Marekani. Ni rahisi sana kuiongoza nchi ambayo tayari misingi yake ipo. Tanzania ya sasa haina misingi imara ya kimfumo na kisheria inayomlazimisha kiongozi yeyote mahali popote alazimike kuwa mwadilifu na mbunifu. Ni lazima tutoke kwenye uongozi wa zawadi, hisani, shukrani na mazoea tuende kwenye uongozi unaozingatia tija (quality and perfection).
 
Uchambuzi umekaa vizuri but naomba ccm wamkate lowasa jina ili ukawa wapate njia laisi ya kufika ikulu kwani kutatokea mpasuko mkubwa sana pindi jina la lowasa litakapokatwa. Kumbuka lowasa amewekeza pesa njingi katika kufanikisha hadhima yake ya kufika ikulu. So wakimkata itakuwa neema kwa ukawa kwani ccm itakatika vipande vipande.

Lowasa hatakatwa jina kabisa ni kuwa hatachaguliwa na wajumbe wengi.
 
Kuhusu Membe, ni yuleyule kimvuli cha JK, HAFAI KABISA. nchi hii tuendako tunaihitaji mtu strong Nyanja zote, labda Wasira!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom