The Worshiper
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 302
- 89
Asilimia kubwa ya wakazi wenyeji wa mkoa wa Dodoma wanakaa vijijini,maeneo ambayo yamegubikwa na umasikini wa kutisha wa kimazingira na watu wenyewe.Ni maeneo ambayo hayana huduma muhimu za msingi za mwanadamu,mfano huduma za Maji , Afya, Miundombinu, barabara nk.Ndiyo mkoa unaosifika kwakujaza ombaomba karibu kila mitaa ya miji mbalimbali nchini (hicho ni kiashirio cha umasikini uliotopea na kutokombolewa kifikra).Baadhi ya makabila(wenyeji) ya mji huu ni Wagogo (hapa tulitambue kama kabila kuu),Warangi,wengine ni wanyambwa nk.
Mfumo wa elimu kuchelewa pamoja na huduma nyingine za msingi kwa wananchi zimeufanya mkoa huu uwe na wenyeji wasomi na wawakilishi wachache serikalini wasio majasiri.Viongozi hawa wachache waliopata nafasi za juu za uongozi na uwakilishi wa wananchi wamekuwa hawana lolote la maana wanalolifanya hasa katika kuwasaidia wenzao kufunguka na kuwakomboa kifikra na mtazamo, kutetea,kupigania na kuleta chachu ya mabadiliko na mapinduzi ya kimaendeleo hapa Dodoma.
Wengi wao(viongozi) ni waoga katika kupaza sauti zao ,si wajasiri kukemea,kuihoji serikali juu ya mipango mingi iliyododa na kulala katika mji huu pia karibu wote wanawekeza na makazi yao yapo Dar Es Salaam.Mbaya zaidi na cha kushangaza viongozi kutoka maeneo mengine ndiyo wamekuwa wakipaza sauti zao bungeni kuhusu kero zilizopo hapa Dodoma.
CCM imeshika hatamu Dodoma na kwa kutumia ujinga wa walio wengi wamekuwa wakiendeleza mfumo wa kuwapata viongozi kwa Ukabila.Kwa tatizo hili lililopo la kimfumo na kiutawala hapa Dodoma ni ngumu sana kuwapata viongozi majasiri na wenye nia thabiti (tofauti na makabila haya) kuuendeleza mkoa huu.Katika hali kama hii kamwe maendeleo hayawezi kuletwa na wenyeji kwakuwa wengi wao bado hawajakombolewa kifikra na mtazamo.Naamini Sisi wageni ndiyo tutakaoubadilisha na kuukomboa mji huu wa Dodoma.
Mfumo wa elimu kuchelewa pamoja na huduma nyingine za msingi kwa wananchi zimeufanya mkoa huu uwe na wenyeji wasomi na wawakilishi wachache serikalini wasio majasiri.Viongozi hawa wachache waliopata nafasi za juu za uongozi na uwakilishi wa wananchi wamekuwa hawana lolote la maana wanalolifanya hasa katika kuwasaidia wenzao kufunguka na kuwakomboa kifikra na mtazamo, kutetea,kupigania na kuleta chachu ya mabadiliko na mapinduzi ya kimaendeleo hapa Dodoma.
Wengi wao(viongozi) ni waoga katika kupaza sauti zao ,si wajasiri kukemea,kuihoji serikali juu ya mipango mingi iliyododa na kulala katika mji huu pia karibu wote wanawekeza na makazi yao yapo Dar Es Salaam.Mbaya zaidi na cha kushangaza viongozi kutoka maeneo mengine ndiyo wamekuwa wakipaza sauti zao bungeni kuhusu kero zilizopo hapa Dodoma.
CCM imeshika hatamu Dodoma na kwa kutumia ujinga wa walio wengi wamekuwa wakiendeleza mfumo wa kuwapata viongozi kwa Ukabila.Kwa tatizo hili lililopo la kimfumo na kiutawala hapa Dodoma ni ngumu sana kuwapata viongozi majasiri na wenye nia thabiti (tofauti na makabila haya) kuuendeleza mkoa huu.Katika hali kama hii kamwe maendeleo hayawezi kuletwa na wenyeji kwakuwa wengi wao bado hawajakombolewa kifikra na mtazamo.Naamini Sisi wageni ndiyo tutakaoubadilisha na kuukomboa mji huu wa Dodoma.