Wafuasi wa CHADEMA tujitathmini kwa hili...

Wafuasi wa CHADEMA tujitathmini kwa hili...

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
345
Reaction score
307
Nimekuwa nikitafakari hali ya kisiasa nchini hususan mambo yanayotokea katika chama kikuu cha upinzani kwa sasa hususan imani na matendo yanayofanywa na wanachama na wshabiki wao.

Nikianza na matukio ya kuwachukulia watu walio tofauti nao kuwa ni wasaliti wasio na uwezo wa kuongoza au kufanya jambo katika ulimwengu wa siasa.

Leo hii mtu anaweza kuwa bora zaidi ndani ya chama hicho na akapewa sifa zote za uungwana anaostahili mtu,anaweza akapambwa kwa kila sifa kwa kuwa yupo ndani ya chama,lakini mtu huyo huyo ambaye leo anaonekana shujaa ndani ya chama kesho anapokuwa nje ya chama unaweza ukasikia madhaifu yake kutoka kwa wale waliokuwa wakimsifu mpaka utashangaa ni namna gani waliweza kuishi naye na kumsifu kabla.

Hali hii kwa washabiki na wanachama kuamini aliye katika nafasi wanayoitaka ndiye bora na akitoka nje ule ubora wake hupotea ni kosa kubwa katika mustakabali mzima wa ushindani wa kisiasa, inaweza ikajenga hisia ya kuwa wote walio katika chama ni wabovu na kinachofanyika ni kusitiriana ili kufika wanapotaka kwenda.

Pia kushindwa kutafuta sababu ya kwanini tuliokuwa nao wanaondoka na kujipa matumaini kuwa kuondoka kwao si tatizo hilo ni tatizo lingine katika ujenzi wa umoja kwani tukumbuke mfano huu mmoja wa Nabii Issa (Yesu) kwamba mchungaji yupo tayari kuwaacha mbuzi 99 walio zizini salama na kwenda kumtafuta mmoja aliepotea na atakapomkosa masikitiko yake huwa ni makubwa.
 
chadema imechokwa na watanzania kwa ubaguzi wao wa kikanda,kidini na kikabila
 
ikumbukwe kuwa ss cdm tunaamn kusolve tatizo ni kuondoa mhusika na siyo kumrekebisha
 
Hiki ulichokiandika hakina tofauti na yaliyoandikwa kitambo na unachokifanya ni sawa na kila mara kubadilisha RADIO lakini CD unayotumia ni ile ile. Tumeishasikiliza sana nyimbo yenu lakini ili CHADEMA iwe salama ni lazima WASALITI wote waondoke kwani kuendelea kuwa nao ndani ya chama ni sawa na kuishi na nyoka ndani ya nyumba kitu ambacho lazima siku moja atakugonga tu.
 
ikumbukwe kuwa ss cdm tunaamn kusolve tatizo ni kuondoa mhusika na siyo kumrekebisha

na "kama wewe unataka marekebisho,kaanzishe chama chako urekebishe msaliti mkubwa wewe! na hatuna maridhiano na wasaliti
" Tuliojaribu kuhoji na kushauri hilo tulipewa majibu kama hayo!
 

Hiki ulichokiandika hakina tofauti na yaliyoandikwa kitambo na unachokifanya ni sawa na kila mara kubadilisha RADIO lakini CD unayotumia ni ile ile. Tumeishasikiliza sana nyimbo yenu lakini ili CHADEMA iwe salama ni lazima WASALITI wote waondoke kwani kuendelea kuwa nao ndani ya chama ni sawa na kuishi na nyoka ndani ya nyumba kitu ambacho lazima siku moja atakugonga tu.

mkuu watu wa dizaini yenu ni sehemu ya tatizo la msingi na shida zaidi ni kwamba hamko tayari kukubali.
 
Ccm imeoza ndo maana ina makundi,chadema 2napambana na waumiani na wahuni kama ZITTO na KITILA mapema
 
ukicheka na nyani utapata hasara kubwa sana , cdm haiwezi kuwaonea aibu wasaliti , lazima wang'olewe popote walipo .
 
Mleta hoja sidhani kama anajua lolote,ninashauri asome katiba ya chadema ibara kwa ibara aache kukurupuka.
 
Mleta hoja sidhani kama anajua lolote,ninashauri asome katiba ya chadema ibara kwa ibara aache kukurupuka.

Katiba sio msaafu kwamba haiwezi kufanyiwa mabadiliko kwa mahitaji kulingana na mabadiliko ya kijamii. kisiasa na kiuchumi.
 
Ushauri ni ushauri tu,hata kama mzuri au mbaya kiasi gani mwamuzi ni mshauriwa,kutenda au kutupilia mbali ushauri husika.
 
mkuu watu wa dizaini yenu ni sehemu ya tatizo la msingi na shida zaidi ni kwamba hamko tayari kukubali.
Wewe ungekuwa ni sehemu ya utatuzi wa matatizo ungekuwa kigeugeu ulijitanabaisha hapa JF kuwa unaachana na CCM na kujiunga Lasmi CHADEMA lakini umedumu kwa miezi 4 tu baada ya ZITTO kuvuliwa vyeo kila kukicha unaisakama CHADEMA na umebaki ukijichanganya mara CCM mara ACT haueleweki.
 
CHADEMA imefikia tamati, haiaminiki tena na watanzania walio wengi. Ulaghai, udini, ukanda, ufisadi, ufuska na ubaguzi umechangia kwa kiasi kikubwa kuwahisha hatma ya CHADEMA.
 
ikumbukwe kuwa ss cdm tunaamn kusolve tatizo ni kuondoa mhusika na siyo kumrekebisha

Mbona hamjamuondoa dr slaa bado anakadi ya ccm na anaendelea kuilipia anasema eti ukumbusho wake je, hiyo kadi angekuwa nayo mwingine angekufukuzwa kwa usaliti....inanitia mashaka kwa kweli
 
Back
Top Bottom