Wafuasi wa CHADEMA acheni uongo

Wafuasi wa CHADEMA acheni uongo

Kama Malaika Mkuu ndio wewe basi huu ulinwengu uko kwenye himaya ya shetani. Hivi huoni ccm imekufa tayari? Jana Pombe kawaambia wafanyabiashara hii ni serikali ya Magufuli, sasa tuje tusikie mtu anatamba eti "serikali ya ccm"! Huyo ni viboko tuu hata awe ni mwenyekiti wenu.
Kazi ya ccm ikiyobaki ni kuendesha mradi wa maegesho ya magari ya watu usiku kwa wale wasio na pa kuyahifadhi usiku

acha kuji inulia mgongo utaumbuka kijana, kwasasa ukawa miozo Hanna lolote Leo hili kesho lile, mlitegemea kuishi kwa matukio sasa matukio Hanna ,ajenda ya ufisadi kaa la moto hahah
 
Last edited by a moderator:
Hivi hawa mwaka huu walikuwa na ilani? je kati ya waliokuwa wanagombea kuna aliyewahi kupewa hiyo ilani kama walivyokuwa wakifanya CCM? No wapi Lowassa alisimama akainadi ilani ya Ukawa juu ya Ufisadi na Rushwa? Ukawa siasa zinaanza kuwatupa mkono na mtaisoma namba.

Hawa ni wachumia tumbo hawana lolote
 
Safi sana mleta uzi. Ni kweli chama chetu cha kijani kinapinga sana tu Ufisadi na kinafanya hivyo kwa vitendo. Kimekuwa kikipinga ufisadi na mafisadi hata bungeni, na wanachama wake hawajawahi kutuhumiwa kwa kashfa ya ufisadi. Tena kwa ukweli kabisa, chama hiki hakiwalindi mafisadi kabisa. Hata wale waliotuhumiwa kupewa miga ya fedha za mboga, kiliwaondoa kwenye michakato ya kugombea ubunge na sasa wanapiga miayo huko waliko. Chama chetu ni kina misingi imara sana na siku zote kinatetea wananchi wanyonge, tatizo kubwa kwa nchi hii ni hawa CHAMEMA na LOWASSA fisadi wao mkubwa......I hate political correctness. It has made people into a bunch of stupid brain dead idiots!

kamfulie kaptula JIZI LOWASA HUNA JIPYA
 
ukawa nilianza kuwadharau siku waliyompokea EDO but huyu dogo Salimu Mwalimu nimemdharau sana badala ya kuongea mambo ya maana anaongea pumba. Inaonyesha bado anadhani huu ni wakati wa kampeni.
 
Katika watu wanao mchukia MAgufuli kwa sasa ni baadhi ya wana CCM maaana kawazibia mianya yooote ya kupiga dili waliokuwa wamezoea Enzi za JK. Hakika CCM wanaisoma namba. Heko MAGUFULI kuwakomalia wezi ndani ya CCM
 
Hivi bandiko hili Ndugu yangu Malaika Mkuu lina tofauti gani na hili?

Tukienda moja kwa moja kwenye kichwa cha uzi,

Baada ya Magufuli kufanya anachofanya kumekua na dhana imeibuliwa na wanaukawa wengi tena wachambuzi maarufu kabisa humu jamvini wakisema Mr rais anaiga ilani ya UKAWA kitu ambacho ni upotishaji mkubwa sana , katika kampeni za kuomba ridhaa ya wananchi kwenye nafasi ya Raisi muheshimiwa Magufuli alijikita katika kupambana na ufisadi na akaahidi mpaka mahakama ya mafisadi, hivyo ufisadi ikawa agenda yake kuu.

Upande wa UKAWA wao ufisadi hawakuuweka mbele sana hata mgombea wao alipohojiwa na BBC na kuulizwa kuhusu atakavyoshughulikia ufisadi mkubwa hakua na jibu , nakumbuka sera kubwa ya UKAWA ilikua ELIMU ELIMU ELIMU pia mheshimiwa Lowassa akaongezea kidogo kua mwenye mbuzi mmoja atakua nao wawili , anaekula mlo mmoja atakula miwili nakadhalika nakadhalika leo Magufuli anaanza kutekeleza Sera zake za kuwashughulikia mafisadi wana UKAWA wanaanza kutupotosha kua anafuata ilani yao.

Wito kwa wana UKAWA tukubali tu kua kwa bahati nasibu au mpango wa Mungu tumepata raisi wa ndoto zetu AMEN
 
Last edited by a moderator:
ukawa hoja ya ufisadi aliondoka nayo Dr. Slaa ndio maana wakawa wanakumbatia mafisadi sasa mwaka 2020 sijui mtamsimamisha nani maana huyo mgombea wao hawezi kugombea si ajabu atakuwa kafungwa na jela ya mafisadi
 
acha kuji inulia mgongo utaumbuka kijana, kwasasa ukawa miozo Hanna lolote Leo hili kesho lile, mlitegemea kuishi kwa matukio sasa matukio Hanna ,ajenda ya ufisadi kaa la moto hahah
MOTOCHINI mie nimeshavuka kipengele cha kuitwa kijana hata kama muonekano wangu waweza kunidhania hivyo. Mie nakushangaa sana, kwa nini wewe na watu wengi wa Kigoma ambao ni wafuasi wa yule CEO fulani wa chama cha siasa chuki zao (tena za wazi) ni kwa Chadema?
 
Last edited by a moderator:
MOTOCHINI mie nimeshavuka kipengele cha kuitwa kijana hata kama muonekano wangu waweza kunidhania hivyo. Mie nakushangaa sana, kwa nini wewe na watu wengi wa Kigoma ambao ni wafuasi wa yule CEO fulani wa chama cha siasa chuki zao (tena za wazi) ni kwa Chadema?
Unapo kuwa mpinzani wewe unapaswa kuwa kioo cha jamii, unapo shauri jema anza kutenda mema wewekwanza, huwezi kuilaumu ccm ikiwa mwenyewe umejaa uozo, siasa mnazo fanya hapa ni kufuata mkumbo wala si siasa za kuchunguza ubora wa sera na matendo ya wanasiasa, nita pinga mwanzo mwisho siasa mnazo fanya za kuwapa UMUNGU MTU KINA MBOWE ikiwa si vizuri, Mbowe akilala akiamka na utumbo woote mnashangilia, leo anamwita Zitto msaliti kesho akisema ztt msafi hamhoji ilikuwaje aitwe msaliti. Kunawanasiasa wengi mliwatimua na hata kuwatukana leo malaika kama vile KAFULILA huyu alikuwa CHADEMA kwa ujuha wenu wakufuatafuata mkumbo mlimtimua lakin leo mtam, Chakaza CDM nzuri kam jina lakin wafuas wake MAZUZU
 
Last edited by a moderator:
Unapo kuwa mpinzani wewe unapaswa kuwa kioo cha jamii, unapo shauri jema anza kutenda mema wewekwanza, huwezi kuilaumu ccm ikiwa mwenyewe umejaa uozo, siasa mnazo fanya hapa ni kufuata mkumbo wala si siasa za kuchunguza ubora wa sera na matendo ya wanasiasa, nita pinga mwanzo mwisho siasa mnazo fanya za kuwapa UMUNGU MTU KINA MBOWE ikiwa si vizuri, Mbowe akilala akiamka na utumbo woote mnashangilia, leo anamwita Zitto msaliti kesho akisema ztt msafi hamhoji ilikuwaje aitwe msaliti. Kunawanasiasa wengi mliwatimua na hata kuwatukana leo malaika kama vile KAFULILA huyu alikuwa CHADEMA kwa ujuha wenu wakufuatafuata mkumbo mlimtimua lakin leo mtam, Chakaza CDM nzuri kam jina lakin wafuas wake MAZUZU
MOTOCHINI kwanza goodmorning. Pili ndugu yangu siasa haina chuki hata kidogo. Siasa haiangalii historia ya mtu bali yukoje kwa wakati husika. Hayo ya Mbowe na muono wako hebu tuyaache kwanza twende kwa Kafulila. Huyu kijana kuna wakati alienda tofauti na chama chake Chadema na wakamfukuza. Akaenda NCCR nako aka wakorofisha wakawa kwenye mchakato wa kumuadhibu akajirudi mapema akasamehewe yakaisha. Chadema wakaanza kumuunga mkono kwa vile alianza kutenda yale wanayoyakubali.
Hakuna ubaya katika siasa mtu kubadilika na hawezi kuhukumiwa kwa misimamo yake ya awali ya kupinga jambo. Umeona hata katika chama kikongwe kama ccm hayo yametokea. Yupo mtu kama Wassira aliondoka CCM tena kwa matusi na kashfa na kujiunga na NCCR, Lakini baadae karudi CCM na kuwa mtu wa muhimu huko kwa kiasi kikubwa kama tulivyoona.
Siasa haina kiporo brother, ya leo sio ya kesho. Malaika wa leo aweza kuwa shetani wa kesho hivyo hata shetani wa jana aweza kuwa malaika wa leo. Huoni mzee Pombe leo kawa lulu? Kwani ni malaika wa jana yule? Ukimchambua unaweza kuona alikuwa shetani jana. Lakini tunasahau hayo.
 
Last edited by a moderator:
😳CHADEMA😳
Nimeshtuka kuskia magufuli anatekeleza ilani na hoja za ukawa.

Kwasasa rais anashughurika sana na ufisadi na ubadilifu najiuliza niwapi mgombea wa ukawa lowassa alijipambanua anachukia mambo haya?

Kwa dakika 8 alizokua akiongea na hoja za babu seya, bodaboda na mamantilie leo wanasema magufuli anatekeleza hoja zao shame on u UKAWA.

Mabadiliko ndio haya sio yale yakuzungusha mikono.

Mnampinga Magufuli na kususia matokeo hotuba yake alafu saizi alafu mnajikomba kwamba anatekeleza hoja zenu Zipi?

Lini mlimkabidhi magufuli ilani yenu mlioiweka kwenye website badala ya kuigawa na kuinadi kwa watanzania shame on u ukawa.

Mpaka sasa wananchi wameishagundu siasa za ulaghai utapeli mnasema leo mtu huyu ni fisadi kesho mnasema msafi kisa amawewahonga billion ns.

Kashifa ya Stanbic wanaotajwa kuhusika ndio waliokua wanawafadhili kwenye campeni begabega mlitaka kugawana nchi hii lakini Mungu amemleta rais wa watanzania.

Ama kweli choo kimehamia chumbani sasa mnanuka shombo ya ufisadi na wizi.

M4C Magufuli for change.
Tulieni ivoivo dawa iwaingie.
Leo wanasema Samia anatekeleza ilani yao. Hawa jamaa akili hawana
 
Back
Top Bottom