Wafanyabiashara katika kituo kikuu cha mabasi Moshi wamegoma

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Wafanyabiashara wa maduka zaidi ya 150 katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wamegoma kufungua maduka wakipinga agizo la halmashauri ya manispaa ya Moshi ya kuwataka kulipa kodi ya shilingi laki nne hadi laki nne nusu kwa kila pango kutoka shilingi elfu 30 walizokuwa wanalipa awali.

Wafanyabiashara hao wamemuomba Rais Dk John Pombe Magufuli kuingilia kati kutokana na baadhi ya wafanyabishara kushindwa kuendelea na biashara na kulazimika kurudi nyumbani.

Wamesema ongezeko hilo ni kubwa sana hali ambayo inawakatisha tamaa kuendelea na biashara na kwamba fedha wanazozipata zinaishia kulipa kodi jambo hali inayowarudisha nyuma kiuchumi.

Akijibu malalamiko hayo Mkurugenzi wa halamashauri ya manispaa ya Moshi Bw.Michael Mwandezi amesema uamuzi wa kupandisha kodi hizo ulipitishwa na vikao vya baraza la madiwani.
 
Wafanyabiashara wa maduka zaidi ya 150 katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wamegoma kufungua maduka wakipinga agizo la halmashauri ya manispaa ya Moshi ya kuwataka kulipa kodi ya shilingi laki nne hadi laki nne nusu kwa kila pango kutoka shilingi elfu 30 walizokuwa wanalipa awali.

Wafanyabiashara hao wamemuomba Rais Dk John Pombe Magufuli kuingilia kati kutokana na baadhi ya wafanyabishara kushindwa kuendelea na biashara na kulazimika kurudi nyumbani.

Wamesema ongezeko hilo ni kubwa sana hali ambayo inawakatisha tamaa kuendelea na biashara na kwamba fedha wanazozipata zinaishia kulipa kodi jambo hali inayowarudisha nyuma kiuchumi.

Akijibu malalamiko hayo Mkurugenzi wa halamashauri ya manispaa ya Moshi Bw.Michael Mwandezi amesema uamuzi wa kupandisha kodi hizo ulipitishwa na vikao vya baraza la madiwani.
Stendi ni eneo nyeti kibiashara sawa na Soko la Kati, Mbuyuni, Double Rd, Market str n.k ambako vyumba vya biashara hutozwa kodi ya pango kati ya Laki 2 na Milioni 1 kwa mwezi kwa maana hiyo kodi ya Laki 4.5 ni sahihi kabisa;
Tatizo ni kuwa Wafanyabiashara hao wengi wao walichangia ujenzi wa stendi hiyo miaka 20 iliyopita kwa makubaliano ya kulipa pango la elfu 30 kila mwezi kwa miaka 10 ambayo imeisha;
Nawashauri Wafanyabiashara waende kupanga ktk majengo ya CCM mkoa na wilaya ambako pango ni kati ya Tshs elfu 30 hadi Laki moja kwa mwezi!
 
Wafanyabiashara wa maduka zaidi ya 150 katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wamegoma kufungua maduka wakipinga agizo la halmashauri ya manispaa ya Moshi ya kuwataka kulipa kodi ya shilingi laki nne hadi laki nne nusu kwa kila pango kutoka shilingi elfu 30 walizokuwa wanalipa awali.

Wafanyabiashara hao wamemuomba Rais Dk John Pombe Magufuli kuingilia kati kutokana na baadhi ya wafanyabishara kushindwa kuendelea na biashara na kulazimika kurudi nyumbani.

Wamesema ongezeko hilo ni kubwa sana hali ambayo inawakatisha tamaa kuendelea na biashara na kwamba fedha wanazozipata zinaishia kulipa kodi jambo hali inayowarudisha nyuma kiuchumi.

Akijibu malalamiko hayo Mkurugenzi wa halamashauri ya manispaa ya Moshi Bw.Michael Mwandezi amesema uamuzi wa kupandisha kodi hizo ulipitishwa na vikao vya baraza la madiwani.
Stendi ni eneo nyeti kibiashara sawa na Soko la Kati, Mbuyuni, Double Rd, Market str n.k ambako vyumba vya biashara hutozwa kodi ya pango kati ya Laki 2 na Milioni 1 kwa mwezi kwa maana hiyo kodi ya Laki 4.5 ni sahihi kabisa;
Tatizo ni kuwa Wafanyabiashara hao wengi wao walichangia ujenzi wa stendi hiyo miaka 20 iliyopita kwa makubaliano ya kulipa pango la elfu 30 kila mwezi kwa miaka 10 ambayo imeisha;
Nawashauri Wafanyabiashara waende kupanga ktk majengo ya CCM mkoa na wilaya ambako pango ni kati ya Tshs elfu 30 hadi Laki moja kwa mwezi!
 
Back
Top Bottom