Ndugu Wanajukwaa baada ya kuhitimisha sabato yangu Leo naomba kuzungumzia kinachoendelea Arusha kwasasa
Madiwani Wa chadema Arusha ndiyo wengi na vikao vya halmashauri ndiyo vinapanga mambo ya jiji madiwani walikaa na kupiga marufuku machinga mjini Kama ilivyoada Baraza likishaa tunga sheria na kuazimia Kazi ya watendaji na serikali ni kutekeleza
Madiwani Wa Chadema walipanga kuwaondoa machinga na wamama wanaouza vitu barabarani serikali sikivu ya ccm ilipoanza kutekeleza madiwani hao na Mbunge wao asiye elewa nini maana ya vikao vya halmashauri na sheria zake wanaanza kulalamika juu ya watu kuonewa wakati wao ndiyo wamepanga maonezi hayo
Leo kilichotokea bara bara ya uzunguni kinahuzunisha Sana maana Mbunge aliwadanganya wauza matunda wakaidi amri halali ya serikali kilichowapata matunda yametumpwa na meza zao kukamatwa
Poleni Sana wauza matunda Wa impalla Lema. Ndiye adui wakipato chetu machinga na wamama Wa sokoni
Yaelekea wewe ni sabato marejea wanaotaka kupanda ndege bila kulipa. Waadventista wa Sabato hawako hivi wala mambo yao hayako hivi. Sabato na ukada wa vyama vyenu ni mbalimbali.