Waendesha bodaboda kutoa sight mirror na kukunja steering handle

Waendesha bodaboda kutoa sight mirror na kukunja steering handle

HARRISON ONE

Member
Joined
Jan 8, 2014
Posts
44
Reaction score
32
Wadau naona kuna tabia ya waendesha bodaboda ya kutoa sight mirror na kukunja steering ya pikipiki, hali ambayo kiukweli inahatarisha usalama wa yeye mwenyewe na hata pia abiria wake.

Mantinki ya kufanya hivyo Ni Nini hasa?
 
1. Muundo wa pikipiki ulivyokaa madereva wengi haupendi na unawaumiza sababu wanakitumia chombo kwa muda mrefu sasa ile kuinama muda wote mpaka jioni mgongo unauma.
2. Wanazipinda ili kutafuta pozi ambalo mabega na mgongo havitakuwa vimetanuka muda wote.
3. Side mirrors nyingi zinatolewa maeneo ya miji yenye foleni ili kuwasaidia kutogonga vyombo vingine vya usafiri wanapojipenyeza kwenye foleni.
4. Side mirrors ni sehemu pekee ya chombo isiyo na madhara kwenye chombo ikitolewa (ukiondoa usalama). ushawahi kuona pikipiki isyokuwa na headlamp, brake, bumper au mudguard?.
 
Kuna Kijiji hapo korogwe nilienda kinaitwa makole .....
Pikipiki nyingi Kama sio zote wametoa mirror nikauliza kulikoni, wakasema nyumba nyingi milango Ni membamba....(sio futi tatu 2.5 upana) hivyo inakua shida kuingiza chombo ndani.....
 
Na wale wa boxer kukunja number plate ya nyuma ili isisomeke vizuri
 
Kuhusu usukani; kupata pozi flani la kukusaidia mwili usijishughulishe sana
Kuhusu side mirrors; kupita sehemu ambazo ni finyu, mfano kuiingiza pikipiki geto, au kwenye miji yenye foleni kupita au kupishana bila shida
Pia yaweza kuwa ni fashion ya ujinga tu wa mtu bila kujua viliwekwa kwa vipimo
 
Back
Top Bottom