Wachimbaji 25 wafukiwa Na Kifusi Baada ya Mgodi Kutitia Shinyanga

Wachimbaji 25 wafukiwa Na Kifusi Baada ya Mgodi Kutitia Shinyanga

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
780
Reaction score
1,831
Jumla ya wachimbaji wadogo 25 kutoka katika mgodi mdogo wa Nyandolwa unaomilikiwa na kikundi cha Wachapa Kazi, uliopo kijiji cha Mwongozo Halmashauri ya Shinyanga, wamefukiwa na kifusi baada ya mgodi kutitia.

shughuli ya uokoaji imefanywa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na wachimbaji katika eneo hilo, na tayari wachimbaji wawili wameokolewa.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro amesema kuwa wachimbaji hao walikuwa katika mashimo matatu tofauti, ikiwemo shimo la duara namba 106 lenye watu 6, 103 lenye watu 11, na duara namba 20 lenye watu 8. Juhudi za uokoaji zinaendelea.

Soma Pia: Shinyanga: Watu sita wafariki dunia kwa kufukiwa na kifusi mgodini 11 waokolea

Tukio la kutitia kwa mgodi huo limetokea Agosti 11, 2025 saa nne asubuhi, wakati shughuli za matengenezo ya maduara hayo zikiendelea.

Mtatiro amewasihi wachimbaji kuwa watulivu wakati jitihada za kuokoa uhai wa walioko chini zikiendelea
Azam TV
 
Mgodi unaomilikiwa na kikundi cha wachapakazi umetitia wakati eneo hilo lilipokuwa likifanyiwa ukarabati, huku watu 22 wamekwama na watatu kuokolewa ambapo hadi sasa na juhudi za uokoaji zinaendelea.

Soma pia: John Mafuru: Wafanyabiashara wa jengo lililoporomoka tunamsubiri Rais Samia ambaye atatupa hatima yetu na Mali zilizomo kwenye kifusi


Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro leo Agosti 12, 2025 baada ya kufika eneo la tukio.
 
Mgodi unaomilikiwa na kikundi cha wachapakazi umetitia wakati eneo hilo lilipokuwa likifanyiwa ukarabati, huku watu 22 wamekwama na watatu kuokolewa ambapo hadi sasa na juhudi za uokoaji zinaendelea.

Soma pia: John Mafuru: Wafanyabiashara wa jengo lililoporomoka tunamsubiri Rais Samia ambaye atatupa hatima yetu na Mali zilizomo kwenye kifusi

View attachment 3439259
Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro leo Agosti 12, 2025 baada ya kufika eneo la tukio.
Dah pole Yao Mungu awanusuri
 
Wanaojiuliza kama mimi JULIUS MTATIRO tangu lini ni mkuu wa wilaya Shinyanga tukutane kwa like.
 
Toshazoea hizo kila siku watu wanakufa na mgodi sema sitaji
 
Huo mgodi naujua unamilikiwa na evalian

Una madini ya dhahabu aina ya makinikia
Unachukua mchanga unapeleka plant
 
Back
Top Bottom